Usahihi kuhusu BRELA

Usahihi kuhusu BRELA

hili ni jipu na wanatuchelewesha na urasimu
Tangu lini ku search for simple info watu wakafanya registration? wanataka namba za sim, majina na verification ndio naweza kusearch business name online

Imagine google wakwambie kuwa kabla hujafanya search lazima uweke namba zako za sim majina yako nk ndio utaweza kufanya business name search...ontop unalipishwa elf 20

ningekuwa na register kampuni au nafanya returns au nabadili jina la kampuni I would have understood the concept of registration na kuweka personal details zangu

MFANO HUU HAPA CHINI NIMEINGIA KWENYE WEBSITE YA SEC YA USA AMBAYO UNAWEZA KU SEARCH MAJINA YA KAMPUNI ZOZOTE BILA KUAMBIWA UWEKE PRIVATE INFO

USHAHIDI HUUU HAPA:

http://www.sec.gov/edgar/searchedgar/companysearch.html

Mkuu huna hoja unalalamika tu bure. Na ni kwa nini hutaki kufanya registration, unaogopa nini kuweka details zako, au sio msafi katika shughuli zako?
 
Wakuu Hekima Kwanza na Denis, mimi ninakubaliana na hoja zenu, lakini si katika kiwango cha kuwaona BRELA ni JIPU! Binafsi ni mdau wa BRELA, nikilinganisha na huko tulikotoka naona kuna mabadiliko makubwa. Kweli kuna changamoto, zingine za mfanyakazi mmoja mmoja na sio BRELA kama taasisi. Mfano, nina zaidi ya miezi miwili niliandikisha jina la biashara lakini utashangaa hadi leo kuna jamaa hajanitumia cheti changu cha usajili, hili siwezi kuliita ni tatizo la BRELA bali la huyo mtu ambaye mimi nahurumia mkewe na watoto iwapo nitamharibia kazi.

Zaidi ya miaka minane iliyopita nilisajili kampuni mapito niliyoyapita hadi kupata cheti cha usajili nikilinganisha na sasa, naona BRELA kuna mabadiliko makubwa sana. Niwaombe tu tukubaliane kwamba matumizi ya mtandao hapa kwetu bado nayo ni changamoto. Na kwa uhakika, ni maoni yangu kwamba kama tusingekuwa na changamoto kwenye matumizi ya mtandao sioni hata sababu ya kutumia muda na gharama kubwa kuhamishia makao makuu Dodoma leo kama tunaendelea kutumia hoja ya Nyerere katika uamuzi huo. Hoja kuu ya Nyerere (japo inapotoshwa) ilikuwa kwamba, kuhamishia makao makuu Dodoma ingesaidia kuharakisha maendeleo katika mikoa mingine kwa kuwa Dodoma ni katikati ya nchi.Je, katika karne hii ya dunia kuwa ni kijiji tunahitaji watu kubebana kwenda Dodoma ili kuleta maendeleo katika mikoa mingine? Hivyo hivyo, tukubali kwamba teknolojia bado ni changamoto kwetu, na BRELA tusiwalaumu sana bali tuwaunge mkono!
Hivi unajua mfanyakazi unapoharibu unaharibu image nzima ya kampuni/taasisi mana nawe unakuwa upo ndani ya system
 
kweli bana hata mimi nimewaona kwenye tovuti yao. wapo Simuyi waelimisha, kuhamasisha kurasimisha biashara na pia wasajili papo kwa hapo. pia nimeona simu zao zipo kwenye tovuti. big up! ila wakaze buti bado
 
Imani iwe kwenu Wakuu!

Baada ya mdau moja kuleta uzi leo kuhusu BRELA, naomba nisaidie kuweka record sahihi. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mimi ni mteja wa BRELA wa miaka mingi, ukweli ni kwamba BRELA ile ya enzi zile siyo hii ya sasa. BRELA ya sasa wanajitahidi sana kwenda na wakati hususani siku za karibuni

Kwa sasa huduma ya kusajili jina la biashara hutolewa kwa njia ya mtandao kwa Tsh. 20,000 tu, popote ulipo Tanzania, awali ilikuwa inakulazimu kusafiri kwenda Dar es Salaam kusajili jina la biashara

Pia, kupata taarifa za makampuni hususani, majina ya wanahisa, wakurugenzi, ofisi za kampuni na mtaji wa kampuni huduma hizo sasa inapatikana kwa njia ya mtandao

Vile vile ukitaka kusajili kampuni awali ilikulazimu kuandika barua na kupeleka kwenye ofisi za BRELA (DSM) kuomba jina hilo unalotaka kusajili kuhakikiwa kama hakuna kampuni nyingine iliyosajiliwa kwa jina hilo hilo, sasa hivi huduma hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao na ni bure, ila ukiwa unapenda jina hilo litunzwe kwa muda wa siku 60 itakulazimu kulipa nafkiri Tsh. 50,000 tu. Na hii ni kwa mujibu wa sheria za makampuni

Pia, malipo ya huduma zote za usajili sikuhizi hulipwa kwa njia ya mtandao; Mpesa, Tigopesa, Fahari huduma, Simbanking, Mobile banking, matawi yote ya CRDB, matawi yote ya NMB Tanzania nzima.

Mwisho, naomba niwasihi wana Jukwaa hili na wananchi wote, kwa kuepuka upotoshaji kama ulivyoletwa humu JF kwa makusudi yake binafsi, ni vyema tujenge tabia ya kupata taarifa zaidi za usajili wa makampuni kwa kuwatembelea ofisini kwao moja kwa moja ama kwa njia ya mtandao www.brela.go.tz (Hapo utapata kila kitu, na sio ule upotoshwaji uliofanya na member mwenzetu wa JF)..

Asanteni!
Umenena kweli kabisa mkuu kwani brella kupo safi sana huduma ni bora kabisa.
 
hili ni jipu na wanatuchelewesha na urasimu
Tangu lini ku search for simple info watu wakafanya registration? wanataka namba za sim, majina na verification ndio naweza kusearch business name online

Imagine google wakwambie kuwa kabla hujafanya search lazima uweke namba zako za sim majina yako nk ndio utaweza kufanya business name search...ontop unalipishwa elf 20

ningekuwa na register kampuni au nafanya returns au nabadili jina la kampuni I would have understood the concept of registration na kuweka personal details zangu

MFANO HUU HAPA CHINI NIMEINGIA KWENYE WEBSITE YA SEC YA USA AMBAYO UNAWEZA KU SEARCH MAJINA YA KAMPUNI ZOZOTE BILA KUAMBIWA UWEKE PRIVATE INFO

USHAHIDI HUUU HAPA:

http://www.sec.gov/edgar/searchedgar/companysearch.html
Kwanza zile verifications ilikuwa ni source yao ya rushwa! Unakuta ukipeleka docs officially... na makaratasi matupu bila senti ya chai; unaweza kusubiria miezi kadhaa bila kurudishiwa majibu lakini mfanyabiashara akiamua kwenda mwenyewe kufuatilia, anaipata ndani ya wiki moja!! Kwahiyo tulikuwa tunalazimika kuwaambia ukweli kwamba wale jamaa ukiwapelekea docs, sahau lakini kama utaweza ku-push; do it! Na kweli wakifanya hivyo tu; mzigo huo hapo!
 
BRELA acheni WIZI
kwanini msitumbuliwe
Wizara ya Viwanda na Biashara imehamia Dodoma ninyi bado mpo Dar na hata Mikoani hampo
Fomu zenu za Online hazifanyi kazi kabisa
Process ni ndefu maana unatakiwa ujiunge kwanza Online na password
sasa Wafanyabiashara ndogondogo wanaanzisha vikundi kupata tu jina kazi
jirekebisheni au MTUMBULIWE
 
b8b7d751-64a7-4f60-aba9-e26ef1a41fd4.jpg
 
Back
Top Bottom