Usafiri wa UDA kutoka Mnazi mmoja kwenda Kivukoni

Boniphace Bembele Ng'wita

JF-Expert Member
Dec 25, 2013
3,446
1,812
Ni kwa nini UDA pekee wanaruhusiwa kupeleka abiria Posta kwa yale magari yanayotokea Temeke kuishia mnazi mmoja


Ndugu zangu najua hata nikisema hakitabadilika kitu lakini bora niseme ili nitoe lililopo moyoni mwangu. Hapa ninapoongea niko Mnazi mmoja naenda Feri lakini cha kusikitisha, hawa UDA wenye dhamana ya kutupeleka Feri wanaamua wao wanavyotaka.

Kilichonikera zaidi wanaamua kuishia posta alafu wakifika posta wanashusha na kupakia tena abiria wa ferry.

Maanake ni kwamba abiria kama unaenda Feri basi unalazimika kulipa nauli mara mbili ili ufike Feri. Wahusika mlioamua kutoa kazi hii kwa UDA basi ninaomba mlifuatilie hili ili kuondoa kero hii kwa maana wananchi mnatutwisha mzigo sana.

Fikiria mm naishi kitunda, nilizoea kupanda gari mbili + kivuko mpaka nafika kigamboni (kitunda- banana- kivuko) lakini sasa napanda magari manne (kitunda-banana-mnazi mmoja-posta-kivukoni-kivuko).

Kweli sisi masikini tutajikwamua?





Daladala kurejea Posta, Kivukoni


MAMLAKA ya Usafirishaji Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imetangaza kurejesha safari za daladala kwenda Kivukoni mwishoni mwa mwezi huu.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam juzi, Ofisa Mfawidhi Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, alisema daladala zote ambazo zilikuwa zimesitishwa kutoa huduma za usafiri zitaanza kufanya hivyo kutokana na ujenzi wa barabara kumalizika.

Shio alisema wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake ambao muda mrefu walikuwa wakipata adha ya usafiri, hususani waliokuwa wakienda Kigamboni, watakuwa wameepukana na adha hiyo.

Mamlaka hiyo ilisitisha daladala kutoa huduma za usafirishaji abiria wanaokwenda Posta na Kivukoni Septemba 30, mwaka jana, kabla ya kuja kuliruhusu Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA) kutoa huduma maeneo hayo, hali iliyosababisha malalamiko kutoka kwa wamiliki wa daladala, wakidai shirika hilo linapendelewa na mamlaka hiyo.

daladala_2.jpg





CHANZO:
TANZANIA DAIMA (13/07/2014)
 
Mimi nilifikiri Taifa letu lina ruhusu Biashara Huria, sasa linapo kuja suala la UDA nabaki njia panda: Kwanza kuna kila dalili la kuonyesha wamepania kuwaodoa washindani wao kwenye SOKO kwa kutumia mbinu za kimafia, wanataka wabaki wao tu! Hawakuishia hapo nina wasi wasi hata Bajaj kukatazwa zisi ingie mjini katika ni moja ya mbinu zao za kutaka kuua biashara za walala hoi, nani ambaye hajui Bajaj zilikuwa zinaleta ajila kwa vijana wengi katika jiji la DSM.

Mikakati hii ya UDA ya kutaka ku-monopolise sekta ya usafirishaji ndani ya jiji - utakuja kuleta vurugu siku za usoni - Kampuni ya UDA ya sasa hivi isitumie jeuri ya fedha kuwanyanyasa wafanya biashara wadogo walio jikita katika biashara ya usafirishaji - Wakumbuke UDA ilipokuwa taabani kifedha ni wafanya biashara binafsi ndio walikomboa wakazi wa DSM kwa kuwapatia usafiri wa kuaminika.

Binafsi sipendi kabisa watu kutumia nguvu za fedha kuwanyanyasa wafanya biashara wadogo wadogo ambao wamedunduliza vijisenti vyao kununua Bajaj na bodaboda ili wajikimu/ajili, alafu mtu anakuja na visingizio mbali mbali mbali vya kuuua USHINDANI, mbona Mataifa mengine yanaruhusu usafiri wowote - anaye hamua apande usafiri hupi ni mteja.
 
Ni kwa nini UDA pekee wanaruhusiwa kupeleka abIria Posta kwa yale magari yanayotokea Temeke kuishia mnazi mmoja
Swali lako linaweza kusababisha ukatolewa kucha kwa koleo, bila kupigwa ganzi.

Huoni mazingira hayo ambayo UDA wanapewa upendeleo wa wazi, kulinganisha na daladala nyingine, kuwa ni ushahidi pasipo shaka yoyote, kuwa lazima kutakuwa na mikono ya wakubwa, katika umiliki wa kampuni hiyo ya mabasi.

Kama lengo lako ni kuwa dumped, kule kwenye misitu ya Mabwepande, ukiwa umeng'olewa meno, bila kuhudhuria dental clinic, basi endelea kudodosa, 'ulaji' wa wazito, ambao wanatambulika kwa aka ya UNTOUCHABLES!
 
Hata sumatra washa tubu mbele ya UDA,UDA ndiyo wanaongoza kwa kukatiza route,hawa hawa hawana vibao wanatoka wapi na wanaenda wapi lakini yanapeta tu,sheria za nchi yetu hazina msimamizi kabisa,bora liende.
 
Nitarejea bidae bana hii ndo tz vigogo hooooyee. Zidumu fikra sahihi za wabunge walio wengi.
 
Mkurugenzi wa UDA alimchapa makonde OCD wa Maswa na hakufanywa lolote seuze Sumatra
 
Ni kwa nini UDA pekee wanaruhusiwa kupeleka abiria Posta kwa yale magari yanayotokea Temeke kuishia mnazi mmoja

Swali lako linaweza kusababisha ukatolewa kucha kwa koleo, bila kupigwa ganzi.

Huoni mazingira hayo ambayo UDA wanapewa upendeleo wa wazi, kulinganisha na daladala nyingine, kuwa ni ushahidi pasipo shaka yoyote, kuwa lazima kutakuwa na mikono ya wakubwa, katika umiliki wa kampuni hiyo ya mabasi.

Kama lengo lako ni kuwa dumped, kule kwenye misitu ya Mabwepande, ukiwa umeng'olewa meno, bila kuhudhuria dental clinic, basi endelea kudodosa, 'ulaji' wa wazito, ambao wanatambulika kwa aka ya UNTOUCHABLES!

Kweli aisee bora kuremain silent
 
Ndugu zangu najua hata nikisema hakitabadilika kitu lakini bora niseme ili nitoe lililopo moyoni mwangu. Hapa ninapoongea niko mnazi mmoja naenda ferry lakini cha kusikitisha, hawa UDA wenye dhamana ya kutupeleka ferry wanaamua wao wanavyotaka.

Kilichonikera zaidi wanaamua kuishia posta alafu wakifika posta wanashusha na kupakia tena abiria wa ferry.

Maanake ni kwamba abiria kama unaenda ferry basi unalazimika kulipa nauli mara mbili ili ufike ferry. Wahusika mlioamua kutoa kazi hii kwa UDA basi ninaomba mlifuatilie hili ili kuondoa kero hii kwa maana wananchi mnatutwisha mzigo sana.

Fikiria mm naishi kitunda, nilizoea kupanda gari mbili + kivuko mpaka nafika kigamboni (kitunda- banana- kivuko) lakini sasa napanda magari manne (kitunda-banana-mnazi mmoja-posta-kivukoni-kivuko).

Kweli sisi masikini tutajikwamua?
 
pole sana MKUU sio ww tuu.hiyo nitabia yao na sifa kubwa ya UDA ndio maana wadau wanalalama kila siku kuwa nao wapige mkanda. yaani njia 1 wao wanaweza wakapakia Mara 4.kunasiku nilitoka gongo la mboto nilipanda UDA konda akawa anasema mwisho buguruni kweli alivyofika buguruni abilia tukashuka wakati tunashangaa shangaa akaanza kupakia UBUNGO tena anasema kabisa mwisho ubungo watu tukapanda mpaka ubungo wakshusha kama kawaida pale ubungo darajani akaanza kuita MWENGE tukapanda mpaka MWENGE mpakani pale akawa anapakia MAKUMBUSHO mia 300..ukigeuka buguruni inamaana kama unakwenda buguruni yakubidi ulipe sh 700 ss fikiria hapo unakwenda gongo la mboto?? inamaana itabidi ulipe tena 400.
 
Lakini haya mambo yanatokana na uongozi mbaya tulonao. Kwa maana viongozi wakubwa wa serikali ndo wanakuwa wafanya biashara. Kwa hiyo kama ni biashara yenye mkono wa mkubwa basi ujue ni ngumu sana kufuata sheria.
 
pole sana MKUU sio ww tuu.hiyo nitabia yao na sifa kubwa ya UDA ndio maana wadau wanalalama kila siku kuwa nao wapige mkanda. yaani njia 1 wao wanaweza wakapakia Mara 4.kunasiku nilitoka gongo la mboto nilipanda UDA konda akawa anasema mwisho buguruni kweli alivyofika buguruni abilia tukashuka wakati tunashangaa shangaa akaanza kupakia UBUNGO tena anasema kabisa mwisho ubungo watu tukapanda mpaka ubungo wakshusha kama kawaida pale ubungo darajani akaanza kuita MWENGE tukapanda mpaka MWENGE mpakani pale akawa anapakia MAKUMBUSHO mia 300..ukigeuka buguruni inamaana kama unakwenda buguruni yakubidi ulipe sh 700 ss fikiria hapo unakwenda gongo la mboto?? inamaana itabidi ulipe tena 400.

shamba la bwana heri, kosa la bwana heri, kesi ya bwana heri, hakimu bwana heri, shahidi bwana heri...Lol Yote heri
 
Hakuna sababu ya UDA kuwekewa masharti tofauti na mabasi mengine yanayotoa huduma ya usafiri jijini,badala yakutakiwa kutumia vibao vinavyoonyesha njia wanazokwenda,wanapashwa kuyandika ubavuni kama daladala nyingine,maana vibao hawavibandiki,na wengine kuwa na vibao zaidi ya kimoja vinavyoonyesha njia tofauti,na hivyo kuwafanya kutofuata route zao.
Baya zaidi usiku wanapandisha nauli kinyume na nauli zilizopangwa na Sumatra,sheria inapashwa kufuatwa,na wahusika waiwajibishe UDA kwa kukihuka masharti ya usafirishaji wa abiria kwa mjibu wa leseni zao
 
Yaani CCM inatutesa kwa kweli sijui hata lini watampa mwingine.
 
Back
Top Bottom