Usafiri Dar - Mtwara, King Yassin Tours hongera

Usafiri Dar - Mtwara, King Yassin Tours hongera

vamda

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
919
Reaction score
599
Habari wana JF,

Moja kwa moja nijikite kwenye mada.

Hivi karibuni nilipata safari ya kwenda Mtwara kutokea Dar. Nilifurahishwa na huduma za kampuni ya mabasi ya King Yassin Tours.

Kila kituo tulichosimama abaria tulitangaziwa kupitia kipaza sauti kilichopo ndani ya basi. Tulipewa huduma ya chai, vitafunwa pamoja na vinywaji humo humo ndani ya basi. Wafakazi waje wanaamini abiria na hata tulipofika mwisho wa kituo (Mtwara) abiria tuliombwa radhi endapo tuliona mapungufu yeyote.

Abaria tulipata huduma nzuri kwa nauli sawa na mabasi mengine. Hili ni fundisho kwa kampuni za mabasi mengine. Waache kufanya kazi kwa mazoea. Waige kampuni mpya ya King Yassin Tours.

MUHIMU: Sina maslahi yeyote na kampuni hiyo bali kama abiria nimefurahishwa na huduma zao. Hongera King Yassin Tours mnajua kufurahisha wateja
 
Huduma kama hizi hata mabasi mengine huko nyuma walikuwa wanazifanya, tatizo huwa haziwi endelevu, ila sema wateja hendelea na mwangwi ambao wenye basi huwa ni faida kwake, kwani huendelea kupata abilia kwa vigezo vya historia.
 
King Yassin bado ni kampuni changa kusini, Inabembeleza wateja waiamini,

Kuna kitu Maning ning, Maning Nice huyu ndiyo mwamba wa kusini, Gari hata iwe na abiria watano muda wa kuondoka ukifika Haina kulemba Pira linawashwa linatembea.

Hasa root ya Mtwara Morogoro. Braza hizi siyo enzi za kusifia chai Bali muda. King Yassin, Bado Bora hata Buti la zungu , Ila Maning Nice Babalao.
images (16).jpeg
Cheki pira Hilo kibati kiasi chake mchawi tochi.
 
Hawaja wapeleka kwnye hotel zao zenye chakula. bei ghari na chakula kibovu hahahha👉👉👉👉😀😀💯💥
 
Kila siku napanda hzo gari ila cjawahi kuona wakigawa chai,
Apa umeongopa,
Suala la kutangaza kila kituo ni kweli ila kuhusu chai uongo
Nimewahi kupewa chai na maandazi kweli hili basi. Wanahuduma nzuri sana kwa kweli.
 
Naona umekuja na staili ya ki abiria ila tumeelewa..wewe ni marketing officer fanya tu ulipie tangazo...
Hao jamaa wanajitahidi kwa huduma , kusini mikoa ya mtwara na Lindi bado kunahitaji ukombozi mkubwa sana kwa biashara ya abiria maana ni kama ndo wanaaanza.

Abiria kule hana haki zake za msingi , kumbuka hawana hata Miaka 10 ya mabasi mazuri ,kwa sababu njia ilisumbua sana kule,
Usishangae unapanda Basi halafu konda anakuomba pesa ya begi ulilobeba Kama mzigo mbali na nauli .
 
Hawaja wapeleka kwnye hotel zao zenye chakula. bei ghari na chakula kibovu hahahha[emoji117][emoji117][emoji117][emoji117][emoji3][emoji3][emoji817][emoji95]
Uzuri wa hotel wanazokula kule nyingi Zina escape route , mfano nangurukuru Basi likisimama unavuka tu bara bara utakutana na bites vinywaji Bei za kawaida
 
Hao jamaa wanajitahidi kwa huduma , kusini mikoa ya mtwara na Lindi bado kunahitaji ukombozi mkubwa sana kwa biashara ya abiria maana ni kama ndo wanaaanza...
Huo ujinga wa kutaka ulipie begi, Wana Sai Baba inyokwenda Liwale. Mibasi mibovu konda jeuri
 
Habari wana JF,

Moja kwa moja nijikite kwenye mada.

Hivi karibuni nilipata safari ya kwenda Mtwara kutokea Dar. Nilifurahishwa na huduma za kampuni ya mabasi ya King Yassin Tours.

Kila kituo tulichosimama abaria tulitangaziwa kupitia kipaza sauti kilichopo ndani ya basi. Tulipewa huduma ya chai, vitafunwa pamoja na vinywaji humo humo ndani ya basi. Wafakazi waje wanaamini abiria na hata tulipofika mwisho wa kituo (Mtwara) abiria tuliombwa radhi endapo tuliona mapungufu yeyote.

Abaria tulipata huduma nzuri kwa nauli sawa na mabasi mengine. Hili ni fundisho kwa kampuni za mabasi mengine. Waache kufanya kazi kwa mazoea. Waige kampuni mpya ya King Yassin Tours.

MUHIMU: Sina maslahi yeyote na kampuni hiyo bali kama abiria nimefurahishwa na huduma zao. Hongera King Yassin Tours mnajua kufurahisha wateja
Hata ABC ya Dar-Dodoma wana huduma kama hiyo wako vizuri kwa kweli,ingawa hiyo ya chai hawana...
 
Back
Top Bottom