Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,812
- 40,418
Hilo la abiria kuimbwa radhi mwisho wa safari kama wameona mapungufu inaweza kuwa basi ya kwanza Tanzania kufanya hivyo, hongera zao maana hata Air Tanzania hawafanyi hivyo.Habari wana JF,
Moja kwa moja nijikite kwenye mada.
Hivi karibuni nilipata safari ya kwenda Mtwara kutokea Dar. Nilifurahishwa na huduma za kampuni ya mabasi ya King Yassin Tours.
Kila kituo tulichosimama abaria tulitangaziwa kupitia kipaza sauti kilichopo ndani ya basi. Tulipewa huduma ya chai, vitafunwa pamoja na vinywaji humo humo ndani ya basi. Wafakazi waje wanaamini abiria na hata tulipofika mwisho wa kituo (Mtwara) abiria tuliombwa radhi endapo tuliona mapungufu yeyote.
Abaria tulipata huduma nzuri kwa nauli sawa na mabasi mengine. Hili ni fundisho kwa kampuni za mabasi mengine. Waache kufanya kazi kwa mazoea. Waige kampuni mpya ya King Yassin Tours.
MUHIMU: Sina maslahi yeyote na kampuni hiyo bali kama abiria nimefurahishwa na huduma zao. Hongera King Yassin Tours mnajua kufurahisha wateja