Usafi katika masterbedroom

Usafi katika masterbedroom

leipzig

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
2,766
Reaction score
1,716
Mimi na mke wangu tumekuwa na mtazamo tofauti sana kuhusu usafi wa chumbani kwetu. Naona usafi wa chumba unaofanywa na mke wangu hauridhishi na hivyo nilimshauri mmoja wa wasichana wetu wa kazi afanye pia usafi wa chumbani.

Kwa bahati mbaya sana yeye hakubaliani kabisa na wazo hilo, anasema heshima yake kwa wasichana wa kazi itapungua. Nikumuuliza heshima yake itapungua kwa vipi anadai hataki binti wa kazi aone nguo zetu za ndani kitu ambacho mimi naona ni sababu ndogo sana.

Sasa nimeshindwa kusubiri nimeona nije hapa jukwaani nisikize ushauri wenu, malezi yangu kwa baba na mama yangu yalikuwa binti wa kazi anafanya usafi pia chumbani kwa mama na baba.

Nawasilisha!
 
Duh........

Mkeo yupo sahihi sana, housegirl ana mipaka yake kwa mwanamke anayejitambua na anayejiheshimu pia anayeheshimu watu wengine pamoja na mume wake.

Chumbani kwa mume na mke niaminivyo mimi na malezi niliyopewa mimi, haruhusiwi mwingine kuingia hata mtoto akishafika umri wa kulala peke yake haingii hovyo ndani kwa wazazi sasa iweje house girl?

kwanini kama usafi haukuridhishi umsaidie mkeo kusafisha badala ya kumwambia housegirl. Huoni kwamba utamdhalilisha mkeo kuwa si msafi? huhisi mtamnyanyasa housegirl kwa kitendo cha kuwafanyia usafi mnapolala nyie?

Kama shida ni usafi haukuridhishi tenga muda fanya usafi wa nguvu hadi mkeo aone aibu na usimwambie chochote. Au kama tatizo ni muda ndio maana hafanyi usafi wa kuridhisha hata baada ya kurudi kazini kama anafanya kazi anaweza kufanya usafi, mwisho saidianeni kufanya usafi sio tu usafi hauridhishi na wewe hufanyi juhudi yoyote ya kumsaidia
 
Tenga muda mwambie mkeo kwa furaha kuwa unataka kumsaidia usafi mkafanye wote yye atajifunza kupitia ww ila c kwa house gal
 
Unatamaaa wewe utatakaje msichana wa kazi akufanyie usaf chumbani wakatmkeo yupo
 
Hivi wakati mtu anaandika post huwa anafikiria au anataka kutuchosha tu hapa.

Unashindwa nini kumsaidia mkeo mfanye wote usafi ili wewe uridhike.

Ina maana unatuambia mkeo ni mchafu na humwamini akifanya usafi?

umeniuzi kwa kweli nisamehe kwa maneno makali ila jiongeze kidogo.

asante.
 
mkuu huo uhodari wa "housegirl" katika usafi utapelekea kuvunjika kwa ndoa yako na kwa kuwa huridhishwi na usafi aufanyao mkeo itakuwa vyema kama utamuelekeza kwa vitendo na si vinginevyo.
 
Saidiana na mkeo umuonyeshe hayo maeneo unayoona hayatakati kwa viwango vyako, ili afuate mkondo wako wa usafi. Just because ulikua ukiona 'dada' anafanya usafi chumbani kwa wazazi, sio lazima iaplai na kwako...
 
Mambo ya chumbani mwachie mkeo siyo kila kitu lazima ukiingilie. Ulivyompa wazo siyo vibaya ila kama hataki acha afanye vile anavyoona yeye ni sahihi. Ila kama unamengine hapo sawa.
 
mwiko!!..chumbani ni kwa mume na mke tu, sio mtu yoyote mwingine, yani ikilazimika saana ndio siku hizi unaona na watoto wanaingia ambayo pia sio sawa, ila sijui housegirl, ndugu etc hapana, mwachie mkeo asafishe, kama vipi msaidie
 
Wakati mwingine wanaume huwa tulalamika kuhusu usafi wa chumbani na ilhali wakati mwingine chumba mnacholala ni kidogo na isitoshe cha kupanga. Hata ungeambiwa wewe ufanye usafi usingeweza kwa sababu ya ufinyu wa nafasi. Kama chumba ni kikubwa na kila kitu kinakaa vizuri kwa mpangilio tungesema ni mvivu ila kama ni kidogo jitahidi ujenge kaka chumba cha master kiwe kikubwa.
 
Mwanaume lazima ujue kumtofautisha Mke/ubavu wako/Msaidizi wako na Housegirl.
 
Mbona dawa yake ndogo? Unampa promotion housegirl ili afanye usafi kila mahali. Hii inaenda sambamba na kumpa demotion motherhouse.

Hili nalo ni gumu kwako Mkuu leipzig?
 
Last edited by a moderator:
House girl wako amekuvutia tayari? Maana unataka kumpa access au administrative priviledges... Usijaribu kufanya hivyo ukaja tena humu jf kuomba ushauri ulilala na house girl
 
Haipendezi housegirl kufanya usafi kwenye chumba cha wanandoa
 
at list kama ungesema unafanya wewe ,, dada wa kazi si sawa kumuingiza chumbani kuwafanyia usafi.... kama unaona mkeo hafannyi usafi unavyotaka wewe sidhani kama unamatatizo ya kiuno au mgongo unaweza msaidia
 
kule bedroom hakuna mtu maalum wa kusafisha jamani kati ya mke au mume, mimi kuna siku nikiamka weekend napiga usafi wa maana including kushusha neti,mapazia na kuyaloweka wife akija anamalizia tu, kusogeza kitanda makabati mabegi kukung'uta vumbi na kupanda,wife kama alikuwa kazini akija anakuta suprise, hawa wanawake tusiwaonee hivi jamani, wanaume tumekuwa kama vilema siku hizi ikifika weekend ni bia na totoz tu,ndoa ni upendo so kama kweli unampenda mkeo utamsaidia tu,

Mimi na mke wangu tumekuwa na mtazamo tofauti sana kuhusu usafi wa chumbani kwetu. Naona usafi wa chumba unaofanywa na mke wangu hauridhishi na hivyo nilimshauri mmoja wa wasichana wetu wa kazi afanye pia usafi wa chumbani.

Kwa bahati mbaya sana yeye hakubaliani kabisa na wazo hilo,anasema heshima yake kwa wasichana wa kazi itapungua. Nikumuuliza heshima yake itapungua kwa vipi anadai hataki binti wa kazi aone nguo zetu za ndani kitu ambacho mimi naona ni sababu ndogo sana.

Sasa nimeshindwa kusubiri nimeona nije hapa jukwaani nisikize ushauri wenu,malezi yangu kwa baba na mama yangu yalikuwa binti wa kazi anafanya usafi pia chumbani kwa mama na baba.

Nawasilisha!
 
Hivi hawa wanaume wapumbavu kiasi hiki wataisha lini!? Maswala ya nyumbani kwako tena chumbani kwako unayatoa hadharani! Kinamna hii wanawake wafanyeje sasa?
 
Hivi hawa wanaume wapumbavu kiasi hiki wataisha lini!? Maswala ya nyumbani kwako tena chumbani kwako unayatoa hadharani! Kinamna hii wanawake wafanyeje sasa?
siku hizi wanaume kuwapata ni kazi
 
Back
Top Bottom