Usafi katika masterbedroom

Usafi katika masterbedroom

siku hizi wanaume kuwapata ni kazi

Uko sahihi! Kama ni wanaume wa hit & run ni wengi, lakini mwanamume atakayekuamini kukukabidhi mwili wake jumla! uwe mke na mama wa watoto wake! akuamini kumtunza yeye pamoja na watoto wake! akuamini kuwa wewe ndiwe MTU sahihi mtakayesaidiana kuzifikia ndoto zake za maisha! akuamini kuwa utamvumilia katika hali zote! akuamini kuwa utamtii! Mwanamume wa jinsi hiyo siyo siri ni adimu sana!
Usione kina Dada wazuri miaka inayoyoma from 20's to 30's, from 30's to 40's then wanaishia kuwa single parents!
Kama haujui thamani ya mwanamume utakuja kulazimika kuijua baadaye!! Pamoja na madhaifu yake yote bado ni Mara mia ukawa na huyo dhaifu kuliko kuikabili miaka mingi mbele yako ukiwa single!!!
Ila kuweka uwiano mwanamke kwa maana halisi ya mwanamke ni adimu pia!
 
Pyeeeeeeeeee

Kama usafi wa mkeo hauridhishi wewe si una mikono? Pale anapoishia endelea.

Hivi maana ya kuwa wawili ni nini???
 
Hujui kuna wanaume kazi yao kukunja mikono?????? Na kuagiza tu

(Kwa uzi huu inaelekea mleta uzi ndio aina ya hawa wanaume......)


kule bedroom hakuna mtu maalum wa kusafisha jamani kati ya mke au mume, mimi kuna siku nikiamka weekend napiga usafi wa maana including kushusha neti,mapazia na kuyaloweka wife akija anamalizia tu, kusogeza kitanda makabati mabegi kukung'uta vumbi na kupanda,wife kama alikuwa kazini akija anakuta suprise, hawa wanawake tusiwaonee hivi jamani, wanaume tumekuwa kama vilema siku hizi ikifika weekend ni bia na totoz tu,ndoa ni upendo so kama kweli unampenda mkeo utamsaidia tu,
 
Mimi na mke wangu tumekuwa na mtazamo tofauti sana kuhusu usafi wa chumbani kwetu. Naona usafi wa chumba unaofanywa na mke wangu hauridhishi na hivyo nilimshauri mmoja wa wasichana wetu wa kazi afanye pia usafi wa chumbani.

Kwa bahati mbaya sana yeye hakubaliani kabisa na wazo hilo,anasema heshima yake kwa wasichana wa kazi itapungua. Nikumuuliza heshima yake itapungua kwa vipi anadai hataki binti wa kazi aone nguo zetu za ndani kitu ambacho mimi naona ni sababu ndogo sana.

Sasa nimeshindwa kusubiri nimeona nije hapa jukwaani nisikize ushauri wenu,malezi yangu kwa baba na mama yangu yalikuwa binti wa kazi anafanya usafi pia chumbani kwa mama na baba.

Nawasilisha!


:decision:wewe bwana huna akili kabisa!, nadhani mkeo ana akili sana ila wewe umekuwa boga kichwani kwako. Yaani ningepata mtu kama mkeo yaani ningepeta sana kwa pale town. Hahahaaa!, ila we jamaa angu kichwa lako kama boga tu naona limejaa maji tu. Au unatafuta njia ya kumuingiza housegirl kwenye faragha yako?
 
Uko sahihi! Kama ni wanaume wa hit & run ni wengi, lakini mwanamume atakayekuamini kukukabidhi mwili wake jumla! uwe mke na mama wa watoto wake! akuamini kumtunza yeye pamoja na watoto wake! akuamini kuwa wewe ndiwe MTU sahihi mtakayesaidiana kuzifikia ndoto zake za maisha! akuamini kuwa utamvumilia katika hali zote! akuamini kuwa utamtii! Mwanamume wa jinsi hiyo siyo siri ni adimu sana!
Usione kina Dada wazuri miaka inayoyoma from 20's to 30's, from 30's to 40's then wanaishia kuwa single parents!
Kama haujui thamani ya mwanamume utakuja kulazimika kuijua baadaye!! Pamoja na madhaifu yake yote bado ni Mara mia ukawa na huyo dhaifu kuliko kuikabili miaka mingi mbele yako ukiwa single!!!
Ila kuweka uwiano mwanamke kwa maana halisi ya mwanamke ni adimu pia!
kazi tunayo kwa kweli
 
Mbona dawa yake ndogo? Unampa promotion housegirl ili afanye usafi kila mahali. Hii inaenda sambamba na kumpa demotion motherhouse.

Hili nalo ni gumu kwako Mkuu leipzig?

Atleast nimekuelewa wewe...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom