US wameiteka meli ya mafuta ya Urusi

US wameiteka meli ya mafuta ya Urusi

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
10,884
Reaction score
18,824
Habari kubwa ya leo duniani imekuwa ni jeshi la US kuiteka Meli ya mafuta iliyotoka Venezuela na kudhaniwa ikielekea Russia. Meli hiyo ilikuwa na bendera ya Russia imedakwa huko Bahari ya Kaskazini. Russia walijaribu kutuma Nyambizi na manowari kwenda kuilinda lakini hawakufanikiwa.

US wanadai meli hiyo inahusika na kubeba mafuta yaliyowekewa vikwazo, japo inadaiwa kuwa wakati wa kukamatwa kwake haikuwa na mafuta. Russia atakubali bila kulipa kisasi?
images (5).jpeg
 
Meli kupeperusha bendera ya taifa fulani haimaanishi kuwa inamilikwa na taifa hilo

Hakuna reliable source inayosema kuwa Russia walituma submarine kuilinda meli hiyo.

Meli yenyewe ilipewa kibali cha kutumia bendera ya Russia Desemba 24 mwaka jana kabla ya hapo ilikuwa inatumia bendera ya Guam

Vyanzo vinavyotegemeka vinasema ni 'stateless ship'

Ni miongoni mwa meli zilizokuwa zinatumiwa kusafirisha mafuta kutoka Venezuela kimagendo

Kabla ya kupost muwe hata mnafanya kautafiti kwanza
 
Mkongwe, hili suala limeshtua Dunia nzima, sio Tanzania tu.

Hili suala ndio hot topic kwasasa, Dunia nzima wanaicheka Russia, labda kama unamaanisha dunia nzima hawajui lugha ya Kiingereza, sawa!
Kwanza umeelewa hizo heading?
 
Meli kupeperusha bendera ya taifa fulani haimaanishi kuwa inamilikwa na taifa hilo

Hakuna reliable source inayosema kuwa Russia walituma submarine kuilinda meli hiyo.

Meli yenyewe ilipewa kibali cha kutumia bendera ya Russia Desemba 24 mwaka jana kabla ya hapo ilikuwa inatumia bendera ya Guam

Vyanzo vinavyotegemeka vinasema ni 'stateless ship'

Ni miongoni mwa meli zilizokuwa zinatumiwa kusafirisha mafuta kutoka Venezuela kimagendo

Kabla ya kupost muwe hata mnafanya kautafiti kwanza
Ni Guyana siyo Guam. Guam ni teritory ya Marekani. Itakuwa uchizi na kujihujumu kusajili meli yq hivyo Guam.

Meli haiwezi kuwa stateless, ndiyo maana zinapeperusha bendera. Na hakuna aliyesema ikipeperusha bendera ndiyo inamilikiwa huko, kilichopo ni kuwa majority ya hizi shadow fleet ni za Warusi.

Hii ni developing story hakuna atakayesema ni chanzo cha kuaminika.
 
Ni Guyana siyo Guam. Guam ni teritory ya Marekani. Itakuwa uchizi na kujihujumu kusajili meli yq hivyo Guam.

Meli haiwezi kuwa stateless, ndiyo maana zinapeperusha bendera. Na hakuna aliyesema ikipeperusha bendera ndiyo inamilikiwa huko, kilichopo ni kuwa majority ya hizi shadow fleet ni za Warusi.

Hii ni developing story hakuna atakayesema ni chanzo cha kuaminika.
Sawa, thanks I stand to be corrected

Kasome habari Sky News inasemwa kuwa ni stateless ship

Wapi imesemwa kuwa hiyo meli ni ya Warusi? Twende kwa fact
 
Sawa, thanks I stand to be corrected

Kasome habari Sky News inasemwa kuwa ni stateless ship

Wapi imesemwa kuwa hiyo meli ni ya Warusi? Twende kwa fact
Haijasemwa wazi ni ya Urusi au kampuni ya Urusi. Ni kukamatwa North Atlantic inadaiwa ilikuwa inaelekea bandari ya Murmansk Russia. Na kuwa inapeperusha bendera ya Russia.
 
Back
Top Bottom