The Zanzibar Echo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2025
- 490
- 836
Urusi imerusha mamia ya ndege zisizo na rubani na makombora magharibi mwa Ukraine usiku kucha katika moja ya mashambulizi makubwa zaidi ya mabomu katika wiki za hivi karibuni, maafisa wa Ukraine wamesema.
Mashambulizi hayo yaliripotiwa huko Zaporizhzhia, Dnipropetrovsk, na Lviv, ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine kujeruhiwa.
Waziri wa Mambo ya Nje Andrii Sybiha alisema shambulizi hilo lilionyesha ni kwa nini juhudi za kidiplomasia za kumaliza vita na ulinzi mkali wa anga ni "muhimu".
Hilo linatokea wakati Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amependekeza Uswizi, Austria au Uturuki kama mahali panapowezekana kwa mazungumzo ya amani na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin.
Mashambulizi hayo yaliripotiwa huko Zaporizhzhia, Dnipropetrovsk, na Lviv, ambapo mtu mmoja aliuawa na wengine kujeruhiwa.
Waziri wa Mambo ya Nje Andrii Sybiha alisema shambulizi hilo lilionyesha ni kwa nini juhudi za kidiplomasia za kumaliza vita na ulinzi mkali wa anga ni "muhimu".
Hilo linatokea wakati Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amependekeza Uswizi, Austria au Uturuki kama mahali panapowezekana kwa mazungumzo ya amani na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin.