Umehit point. Niliwahi kusema kuwa kijeshi vitu vipo classfied sio kila kitu kipo hadharani,
Ndio mana hata specification za missile/fighter zinatlewaga za chini alaf real zinakua hidden, Anaejua ukweli kuhusu details zote labda ni kikosi kinachofanya operation kwa kutumia vifaa husika, mtangenezAji na maafisa waandamizi labda na raisi/waziri wa ulinzi
Ila kuwan vifaa ni issue nyingine na vita ni issue nyingine,
Kumbuka Marubani wa Iraq walikataa kurusha ndege kupambana na wa USA during operation iraqi freedom, So vifaa havikusaidia kitu
My point:kuna siri nzito sana chini ya kapeti la super powers, Hakuna alietegemea bomu la hiroshima wala nagasaki, So kuna vitu vingi hatujui,
Narudi kumpigia chapuo USA:kumbuka wwII anamchapa mtu na atomic bomb na bila yy ile vita isingeisha aisee, Shikamoo USA, sasa pimia how advanced hiyo technology itakua kwa sasa
Kasome upya historia coz kama uliisoma basi hukuielewa.
Baada ya USSR kuimaliza Ujerumani huko Ulaya. Joseph Stalin aliamuru vikosi vyake vielekee China ili kuwaondoa Japan huko hasa katika eneo la Manchuria na Korean Peninsula.
Expectation ya Marekani ilikuwa kuwa USSR isingefanikiwa kuishinda Japan kwani Uingereza, Ufaransa na Marekani wenyewe walishashindwa katika initial attemp hali iliyosababisha Wachina walemewa sana na Wajapan ambao walikuwa very advanced ki-teknolojia kuliko Wachina. Hali hii ilisababisha WW2 ichelewe kuisha huko Asia mashariki kwani huko Ulaya vita ilikuwa ishaisha.
Stalin alishaahidi kupeleka majeshi huko Uchina na Korea kwa sharti kuwa amalize kwanza vita vya kumng'oaHitler Ulaya. Alitimiza ahadi yake August 1945.
Ilikuwa ni vita iliyowashangaza sana Europeans na Americans kwani matokeo yake yalikuwa kinyume kabisa na matarajio yao.
Mashambulizi ya vikosi vya ardhini vya USSR huko China yalikuwa ya kasi sana na iliwachukua Warusi only 22 days kuwang'oa kabisa Wajapan kutoka China na kiasi cha eneo la Korean Peninsula.
Hali hii ilimshtua sana Marekani. Itambulike kwamba mpango wa USSR ulikuwa ni kuingia visiwa vya Japan na kumlazimisha Mfalme wa Japan ku-surrender. Tafsiri yake ni kwamba endapo USSR ingefanikiwa basi Japan ingekuwa under the influence of Communism instead of Capitalism.
Kwa kuiona hatari hii Marekani aliamua kumuwahi USSR kuingia Japan ila si kwa kutumia Conventional War maana alishashindwa approach hii bali aliamua kutumia newly developed Atomic Bombs. Kwa njia hii Marekani akaiwahi USSR kuingia Japan na hatimaye Japan ikawa under American influence hadi leo.
USSR hakuwa na ujanja kwani back then USSR alikuwa bado hajagundua Atomic Bombs. So, majeshi ya USSR hayakuingia Japan.
Baada ya Marekani kufanikiwa kuizuia USSR isiingie Japan. Ulibaki mtihani mwingine wa kuizuia USSR isiichukue Korean Peninsula yote coz walikuwa wameshachukua kama nusu ya hiyo Peninsula. Marekani ikatuma vikosi haraka Korea kusini na kwa kushirikiana na majeshi ya ukombozi ya Korea wakawa wanaelekea kuwakabili Warusi. Ndipo USSR ilipositisha ku-advance southward. Pale majeshi haya yalipokabiliana ndipo ulipochorwa mstari wa kwa kwanza wa demilitarized zone unazitenganisha North and South Korea.
Fukuto hilo lilibaki frozen kwa muda hadi mwaka 1950 vilipoibuka vita ya Korea. But this time USSR hakuingia vitani direct but alimtumia China kama Proxy kwa kumpa silaha na mafunzo. Marekani yeye aliingia vitani moja kwa moja akiwa upande wa Korea Kusini while China alikuwa upande wa North Korea. Majeshi ya China yalifanikiwa kuizuia Marekani asichukue Korean Peninsula yote na ile line of demilitarized zone ikabaki almost vilevile though initially wakati wa vita ilihama sana in favour of Americans.