Urais CHADEMA moto 2015: Dk Slaa, Mbowe, Zitto hapatoshi

Wana JF,

Itakuwa vizuri zaidi tukajikita katika kujadili mchakato wa katiba.Tujadili maudhui ya katiba mpya ili tupate katiba bora kabisa ili tufike kwenye demokrasia ya kweli na tujenge Tanzania tuitakayo miaka 50 ijayo kuanzia sasa

Kwa wanachadema,tujadili namna bora ya kutunga sera mbadala na tufikirie zaidi kujiimarisha kama timu ili ifikapo 2015 tuingie kwenye uchaguzi mkuu tukiwa hatuna mgogoro wala makundi.Tukiimarishe chama chetu,tunayo fursa ya kuendelea kusaidiana na viongozi wetu wa ngazi zote na tuweke miundombinu itakayotupatia viongozi bora watakaotupeleka 2015.Wakati wenzetu wanagawanyika basi tutumie fursa hii kujiimarisha ila kwa tahadhari ya hali ya juu ili tusije tukaingia kwenye mtego wa kutegemea udhaifu wao tu

Tuweke mikakati mizito,tuzibe mianya yote na udhaifu uliokuwepo uchaguzi uliopita.Tunayo dhamira moja,naamini chama chetu kitatoa mgombea bora 2015 bado.Kitu cha msingi tuepuke ubinafsi tualenge kwenye maslahi mapana ya chama na taifa letu kwa ujumla.Uchaguzi wowote au uteuzi ndani ya chama chetu ni lazima tuuweke kwenye mizani ya 2015,ni uchaguzi wa Transitional team.

Ni wakati muafaka kwa wanachama na viongozi kupima aina ya kauli tunazotoa vinywani mwetu,sio muda wa kutoa reckless statements.Tuwekeze na tuimarishe kitengo chetu cha research.Ni muda wa uwajibikaji zaidi na kila mmoja awe evaluated kupitia results zinazoonekana

Kuna mgombea/wagombea wa chama tawala wanajitahidi kujitenga na udhaifu wa serikali iliyopo ili kujenga aura ya messiah ajaye.Watanzania tusidanganyike.Wanajitahidi kujifanya wanaguswa na matatizo ya vijana ili kuteka kundi la vijana ambao ndio mtaji mkubwa wa vyama na wagombea urais 2015.Tuitumie taasisi ya BAVICHA katika hili na kitengo cha research.Tusiingie kwenye mtego wa majungu kama wenzetu.Pia katibu mkuu na secretariat wanajituma tuwaongezee nguvu

Tujipange kikamilifu kwani uchaguzi ujao utakuwa mgumu sana,naamini CHADEMA itaweka historia.Tupanue mtandao,tuimarishe safu ya uongozi na kuhakikisha umoja na mshikamano ndani ya chama,tufanye tafiti za kutosha tuandae ilani ambayo itakuwa the best na itakayo sustain transition kwa kuzingatia waathirika wakubwa na walengwa wakundi kubwa la vijana katika aspect zote

Ben,

Mkuu chadema isipochukua dola 2015 nahisi unaweza kuingia msituni.ila nimeona unatumia Masters yako ya International relations vizuri katika propaganda na kutetea chama chako.Hata hivyo usitegemee chadema kushinda 2015.ila shwari tu naona mmejipanga kwa juzi kumteua mnyika kwenye hicho kitengo cha propaganda ndani na nje ya nchi.hii ni changamoto kwa nape na January makamba sasa.punguza siasa za ki-radical maanke kila ukiongelea demokrasia huwa nainua eyebrows kwa jinsi ninavyokufahamu.ee mungu iepushe tanzania na umwagaji damu uchaguzi mkuu ujao
Inaonekana mnaanza kujiandaa kama vile mmejua lowassa atakuwa mgombea ndani ya CCM.Hakuna chama chenye hatimiliki ya vijana
.
 
Chama makini kama CDM hakiwezi kufanya kazi moja tu kama inayofanywa na CCM-Magamba ya kulala na kuamka CCM wanawaza uchaguzi tu na ndio maana wameshindwa kuleta maendeleo katika nchi hii kwa miaka mingi sasa,huyu alieandika gazeti alikuwa anatafuta namna ya kuuza tu.na nadhani mwananchi nao wanaanza kupotea njia
CDM mpaka sasa ni chama makini hakiwezi kuanza kuwaza mambo ya urais ndani ya chama leo.
 
CCM AMBAYO KWA VYOVYOTE LAZIMA ISHINDE UCHAGUZI UJAO HATA IKIWAHI NDANI YA KATIBA MPYA:

Maneno niliyoyapigia mstali yanaonyesha kuwa unaipenda siasa ila haujakomaa ktk siasa za ushindani. Hapana sababu ya kupendekeza mgombea wa urais 2015 eti kwa ajiri ya kutoa ushindani tu bila lengo wa kuingia Ikilu. Na kama lengo ni ushindani tu bila nia ya dhati ya kuikomboa nchi toka mkoloni mweusi CCM basi hatuna sababu ya CHADEMA kuingia kwenye uchaguzi wa 2015. Tusipende kukatishana tamaa kwa vita iliyopo mbele yetu, kwani tulio wengi ni matumaini yetu kuwa 2015 Tanganyika itakombolewa rasmi na kurudisha matumaini yaliyopotea baada ya kifo cha baba wa Taifa ( Nyerere). Ushindi ni lazima ndio moto wa wafuasi wa ukombozi wa nchi hii. Matumaini na mawazo ya watanzania ni kwamba 2015 tuwachague wahuni wengine maana waliko sasa basi kwa usanii wao. KUGOMBEA UONGOZI NI LAZIMA IWEPO NIA YA DHATI YA KUONGOZA WATU NA WALA ISIWE KUSINDIKIZO TU.

Fikra "utopia"
 
Siku hizi maoni ya watu yanafanywa heading kwenye magazeti. Au ndiyo mbinu za kuifanya CDM nayo ionekane ina migogoro kama CUF, NCCR mageuzi na CCM? Uzushi, hakuna mbio za urais CDM muda huu. Utaratibu wa kumpata mgombea ndani ya CDM upo wazi kabisa wala hatuna shaka na hilo. Magezeti yaache kuchochea vitu ambavyo havina msingi.

Mwananchi nalo la UDAKU?
 
Una wazimu wewe aliyekwambia Mbowe ananunulika nia nani?????? Angekua hivyo CHADEMA ingeshauzwa long time, fanya research na kwa taarifa yako "no mbowe no more chadema" Chama kinaendeshwa na Mbowe wengine woooote wanafuata ideas za mbowe. Amekua mbunifu wa mambo mbalimbali ndani ya chama. Uliza uambiwe sio unaropoka tu hapa jamvini

Hayo mambo ndio hatuyataki ubinafsi, soma katiba ya chadema haina Mbowe wala Dr Slaa, hayo mambo bila fulani hakuna chama dogo naomba ufute kauli yako.
 
Dr Slaa ana mvuto sana kwa sasa kwhyo chadema msijaribu kutomuweka kwenye kinyang'anyiro cha urais,Ameiinua sana CDM kutoka 2% hadi 46%(kabla hazijachakachuliwa) kwahyo mie kura yangu ya urais ipo kwa Dr.Slaa otherwise sitopiga kura
 
CCM AMBAYO KWA VYOVYOTE LAZIMA ISHINDE UCHAGUZI UJAO HATA IKIWAHI NDANI YA KATIBA MPYA:

Maneno niliyoyapigia mstali yanaonyesha kuwa unaipenda siasa ila haujakomaa ktk siasa za ushindani. Hapana sababu ya kupendekeza mgombea wa urais 2015 eti kwa ajiri ya kutoa ushindani tu bila lengo wa kuingia Ikilu. Na kama lengo ni ushindani tu bila nia ya dhati ya kuikomboa nchi toka mkoloni mweusi CCM basi hatuna sababu ya CHADEMA kuingia kwenye uchaguzi wa 2015. Tusipende kukatishana tamaa kwa vita iliyopo mbele yetu, kwani tulio wengi ni matumaini yetu kuwa 2015 Tanganyika itakombolewa rasmi na kurudisha matumaini yaliyopotea baada ya kifo cha baba wa Taifa ( Nyerere). Ushindi ni lazima ndio moto wa wafuasi wa ukombozi wa nchi hii. Matumaini na mawazo ya watanzania ni kwamba 2015 tuwachague wahuni wengine maana waliko sasa basi kwa usanii wao. KUGOMBEA UONGOZI NI LAZIMA IWEPO NIA YA DHATI YA KUONGOZA WATU NA WALA ISIWE KUSINDIKIZO TU.

i like it
 
Watanzania ikiwa ni mwaka mmoja tu umepita tangu tutoke kufanya uchaguzi mkuu, na sasa mnatuaminisha tuanze kuwa busy na kujadili tena kiongozi ajae kwa mwaka 2015.
Hii inaonyesha ni jinsi gani hatuna mambo ya msingi ya kufanya au kujadili kama kipindi chote ni kuongelea na kufikiria nani na nani awe kiongozi wetu.?

Muda mbona upo tena wa kutosha kuanzia kwenye vyama vya kisiasa mpaka kwenye tume ya uchaguzi, kipindi kingine kinachobaki ni kwa ajili ya kufanya shughuli za kimaendeleo kwa ajili ya nchi yetu.
Kujadaili masuala ya siasa au ya kitaifa hayakuzuii wewe kufanya shughuli nyingine za maendeleo. Mijadala itaendelea, maendeleo yatafanyika, achana na propaganda za magamba kuwa sasa tukae kimya tusubiri had 2015 ndo tuanze kujadili tena siasa. Kimsing tukianza kujadili mambo haya muda huo tutakuwa tayari nyuma ya muda, lazma tujue ni kiongoz mwenye sifa gani tunataka atuongoze, na kama hizo sifa hana kwa sasa, ni muda wake kujipanga upya well before 2015 kama bado ana ndoto za kuiongoza nchi. Aidha, kumbuka mwisho wa chaguzi moja ndiyo mwanzo wa chaguzi zijazo hasa kwa vyama ambavyo havifanyi kazi kwa msimu.
 
naona sasa mwananchi linatumiwa vibaya, chombo pekee cha habari kisichoegemea upande wowote ni hapa JF, hata wahongwe hawawezi kuchakachua mawazo ya members humu.
 
Chondechonde CHADEMA, msijaribu kuingia kwenye majarbu ya mbio za urais. Huu ni wakati wa kuimarisha chama. Kama ni rais basi ni Dr
 
Ritz,

Suala la mgombea Urais ndani ya chadema linjulikana kwamba linategemea mchakato wa kidemokrasia na muafaka ndani ya chama chetu.Siyo kama ilivyo kwa CCM ambako hadi wanajimu walitumika kumtishia yeyote ambaye angetaka kupambana na JK.Pia usisahau maneno ya katibu mkuu Yusuf Makamba kwamba alikuwa tayari kufungwa kwa ajili ya JK,yaani demokrasia huko ni mwiko

Leo hii mgombea urais wa chadema mwaka 2010 Dr. Wilbroad slaa anaonekana mwenye appeal kwa watanzania kuliko Jk na ni tumaini kubwa kwa watanzania.Pia usisahau kwamba Chadema kimejipanga kuwa na hazina kubwa ya viongozi wa baadae

Dr. Slaa is proof that more can be achieved with his moderate and pragmatic style in Tanzania than with the uncompromisingly hardline stance of much celebrated chaps in CCM. You then , as a focused opposition politician , need a hands-on approach , between election periods, to gain support, visibility and acceptance .

I am just not comfortable with folks thinking they have a divine right to be supported to win when , between elections, those folks do not behave like oppositions who want to win . Anyone who seriously wants to defeat the CCM crew should start their effort now (but without jeopardise harmony and peaceful co-existence within the party) or save us the finger pointing in 4 years time .

I personally believe it is not difficult to defeat the CCM if the opposition has the energy, enthusiasm and ideas to stay the course instead of going to sleep for 4 years and hoping to win magically during election when issues such as the mental divisions of Tanzanians still play a huge part in how people vote

Instead our Politicians in opposition remain indolent before election time yet they want to defeat the Chama Cha Mapinduzi with 3 months of election campaign alone.

NB: Halafu ukishauri chama chako(just in case you are a CCM Cadre) kirudi kwenye mstari kabla ya 2014 kwani hukumu yenu itakuwa kubwa,utakuwa ni uchaguzi utakao-evaluate falsafa ya maisha bora kwa kila mtanzania kama chama ,na pia uchaguzi utakaopima confidence ya wananchi kwa mgombea atakayejiita bora lakini ndani ya chama kibovu kisicho na rekodi ya kuwatendea mema watanzania dhidi ya ilani bora na mgombea bora wa chadema
Duu! Ben,unatisha kama ukoma! yaani huu uchambuzi wako hapa na huo mwingine hapo juu nimeukubali kupita maelezo mkuu wangu! Hakika wewe ni future mzuri sana kwa Chadema....ahsante kwa hoja zenye mashiko na uendelee hivyo hivyo.
 
Hii habari nimeiona kwenye gazeti la Mwananchi. Kwa hakika kuna mkono wa magamba nyuma yake. Ishu ya kugombea urais chadema si hoja ya msingi kwa sasa. CDM wanajadili matatizo ya watanzania na kutoa suluhisho, ccm wanataka madaraka na wako tayari kutoa roho za watu wengine ili kutimiza malengo yao. Kwa bahati mbaya hata wakipewa madaraka hawana uwezo wa kuongoza.
 
Una wazimu wewe aliyekwambia Mbowe ananunulika nia nani?????? Angekua hivyo CHADEMA ingeshauzwa long time, fanya research na kwa taarifa yako "no mbowe no more chadema" Chama kinaendeshwa na Mbowe wengine woooote wanafuata ideas za mbowe. Amekua mbunifu wa mambo mbalimbali ndani ya chama. Uliza uambiwe sio unaropoka tu hapa jamvini
Hii hatari. Yaani chama kikubwa kama hiki kinamtegemea mtu mmoja tu! Kwamba bila Mbowe hakuna CHADEMA! Mkuu huo ndio ukweli au ulikuwa unasherehesha tu baraza? NO MBOWE NO CHADEMA! HII MBAYA MKUU
 
Hivi Zitto atakuwa amefikisha umri wa kikatiba wa kugombea urais, hivi wahariri wetu nao mbona makanjanja, kwa nini unaruhusu huu upupu utoke hewani tena the leading story, jamani hata mwananchi. This is too low for the paper that i gave 50% trust.
 
Wanataka nini wote hawa ?
Urais si mchezo, majimbo tu ni kazi.

Kwanini binadamu anasumbuka hivi ?
 
Dr slaa ni rais wetu wa moyoni Mungu ampe nguvu na hekima ili tuweze kuikomboa Tanzania yetu iliyoibwa na Majambazi CCM.
 
Hii habari imekaa kama ya kuuzia gazeti,sikutegemea kama mwananchi lingeripoti habari kama hii

Kwanza,muda bado,na sidhani kama ndani ya CHADEMA kuna mwelekeo wa kimagamba

waliotajwa moja kashawahi kugombea na mwaka jana akampa nafasi mwenzake,hata kama anapenda kugombea tena nafasi itapatikana bila zengwe ,kupigana vikumbo ni habari ya udaku udaku na kimagamba magamba

Zitto Kabwe alishasema hatagombea,na hata kama ikitokea akabadili msimamo na akawa na sifa binafsi na za kikatiba kugombea hahitaji kupigana vikumbo maana uwezo wake unajulikana

Dr Slaa aligombea mwaka jana,uwezo wake unajulikana kwa watanzania,kama akiamua kutogombea tena ndani ya CHADEMA kuna hazina kubwa ya viongozi ukiachana na hao waliotajwa,swala la kupigana vikumbo halipo
nakuunga 100%

ila hata kama wote wanataka nadhani ni vizuri sana na hata wangekuwepo wengine waje tu hii itaonyesha chama kina watu si kila siku huyohuyo hana mpinzani anakuwa mtume kura ndizo ziamue
 
Back
Top Bottom