Upuuzi wa Masoud Kipanya

Kivumah

JF-Expert Member
Jan 7, 2008
2,428
1,050
http://3.bp.blogspot.com/-4_12nGrXGA4/TsNmc1XqDoI/AAAAAAAASGA/oLFD4GU0OPc/s1600/kipanya.TIF
kipanya.jpg

...Ni Documentary hii imetengenezwa na Masoud Kipanya, imeingia sokoni jana 15/11/2011, tuitafute tuone kilichomo.
By the way Maisha Plus sijui iliishia wapii!!!

 
Mkuu nilimuona akiitambulisha TBC1 ni kali kinoma mi naitafuta kwa udi na uvumba pia alisema ukiuziwa zaidi ya 3,000 kashitaki. Kuhusu maisha plus ni kila baada ya miaka 2 so mwakani kitu hewani.
my take: kile kichwa ni noma kinaona mbali na kufahamu mengi na makubwa sikuwahi kufikiria.
 
wakuu! tunatakiwa tuone kilichomo ndani ndo tutoe maoni! yeyote anayejua kinapatikana wap atujulishe hapa...
 
Yeh, he is a guy emboded with exceptional intellectual ability and creativity. Is extra genius!!



kp+Aug+12.jpg


[h=3]PRESS RELEASE YA KUZINDUA DOCUMENTARY YA ''UPUUZI WA MASOUD KIPANYA''[/h]

UPUUZI WA MASOUD KIPANYA its a 47 minutes documentary ambayo Masoud himself recorded since mwaka juzi katika mazingira ya kijiji kilichotumika kurekodia MAISHA PLUS.....guese you know wat i mean.....


kp.jpg

In his own words,KP says ''Mfumo nilioutumia ni kuongelea mambo mengi mchanganyiko na ili kuondoa uchovu wa kunitazama nikiongea, nimechanganya footages za videos, illustrations na animation (katuni) kuchagiza yale ninayokuwa nayazungumzia.
kipanya1bc.jpg

Ujumbe wa dvd hii ni nadharia ya vipande 26 vya keki. nikatengeneza MFANO wa uwepo wa idadi hiyo ya vipande vya keki ambavyo mara baada ya kuwekwa mbele ya watu (watanzania), kundi hilo la watu likataka kutoana roho ili kila mmmoja apate kipande cha keki hiyo, bahati nzuri wakatokea werevu (viongozi) ambao waling'amua kuwa kumbe idadi ya vipande vya keki (26) ni sawa kabisa na idadi ya watu waliokuwepo ambao walikuwa wanakaribia kutoana roho.
kipanya2bc.jpg

Werevu hawa wakawaambia watu hawa kuwa hatuna haja ya kung'oana meno wakati idadi yetu ni sawa kabisa na vipande vilivyopo, ukatengenezwa uataratibu wa kupanga foleni ili kila mmoja apite mbele achukue KIPANDE chake. baada ya kukubaliana hilo, bado werevu wakaona ni vema foleni hii iangalie walio dhaifu ili wawe mbele wawahi kupata keki kuchelea kuanguka kwa njaa.
kp3.jpg

Wakati vipande hivi vya keki vilipoanza kugawiwa, hawa viongozi, (watatu) wakaamua nao kwa kuwa ni sehem ya watu 26 kuchukua VIPANDE VYAO MAPEMA, bahati mbaya baadhi yao kutokana na kuwa karibu na meza ya keki na kutokana na ULAFI, wakaamua kuchukua zaidi ya kipande kimoja cha keki hali iliyopelekea watu wa mwishoni katika foleni ile kukosa vipande vyao.Dvd hii pia imeingia ndani kwa mafumbo kiasi kuangalia sababu inayopelekea watu kutaka kujipendelea zaidi kiasi cha kupelekea kudhulumu wengine, ikajaribu pia kuangalia dawa inayoweza kutumiwa kuepuka hali hii ya uchu na tamaa inayosababishwa na hofu ya kujiuliza nitapata lini na woga wa kuhofia kupoteza kidogo alicho nacho mkononi.


Kwanini umeitwa upuuzi? Masoud Answers ''kwa sababu ya tabia na hulka za binaadam kupenda kupuuza kila kitu, ni hili nalo limetengenezwa ili ulitazame kisha ulipuuze....''
Concept: Ni documentary yenye sauti na picha za video pamoja na katuni mnato na katuni mtembeo (still cartoons and animation)

Main Characters: Masoud Kipanya himself

Imeingia sokoni jana jumanne tarehe 15-11-2011 na inasambazwa na UMOJA AUDIO VISUAL.
Bei: Shilingi buku 3,000 tu.

Running time: Dakika 47

Sponsors: Hakuna mdhamini.

Future plans: Ni matayarisho ya upuuzi mwingine "WENYE NGUVU NA WAPAGAZI"

Nashukuru kwa ushirikiano wenu na mungu awabariki sana

Regards,
MASOUD KIPANYA.


 
Ukiwa mbunifu hulali njaa hapa mjini, haya Kipanya tutakuunga mkono japo copy 2 tutanunua....
 
Nae si member humu atuambie wamatumbi wa ugaibuni watapataje hii DVD
 
Nae si member humu atuambie wamatumbi wa ugaibuni watapataje hii DVD

NI kweli mkuu maan ainaonekana tumesahauliwa!! Maana hizi ladha za kibongo ni adimu!! Haya ma-drama ya wazungu yamechosha sasa!!
 
Na ndiyo maana clouds walishindwana naye, hicho kichwa wakuu. Wakaamua kubaki na magumegume ya magamba hadi leo, wanaelekea kuzimu. wehu sana clouds
 
jamaa amelenga soko ktk wakati muafaka, hadhira sahihi. safi masoud kipanya
 
Back
Top Bottom