Nimemhurumia sana jamaa yangu.Ni jamaa ambaye tumekua naye, tumesoma naye ni mpole sana na mcha Mungu sana. Kanisani kwao ni mtu mkubwa tu sijui anacheo gani, lakini ni mtu mkubwa tu.
Huyu mshikaji alioa mwaka jana mwanamke mrembo sana lakini alionekana kama mtukutumtukutu. Mshikaji kamuombea mpaka mwanamke kawa mtu mzuri tu na kanisani naye kapewa cheo fulani hivi ni Kanisa kubwa tu hapa Dar es salam.
Sasa mwanamke amekuwa akitumia sana upole wa mwanaume kumdrive kama anavyopenda. Anaweza kumnunia tu hata wiki nzima, huku mshikaji anachanginyikiwa sana na kukonda mno, hapendi kabisa wagombane na mke wake.Yaani jamaa anavyopelekwa mpaka unamuonea huruma.
Jana nimemwambia dawa ya hawa wanawake watafutie papi, akileta nyoro kale maini. Mbona atanyooka mwenyewe tu bila hata kuchapwa.Hapa mshikaji nimemtafutia msichana na vile mshikaji anapesa demu kakubali, na huyu msichana ni wa ushwahilini mshikaji atakipata cha moto mpaka atasahau mateso.
Wanaume wapole msifikiri ni sifa ni uzombi.