Upo wapi Anneth Benidicta?

Upo wapi Anneth Benidicta?

Hi!

2014 ulinipenda pasipo chochote, sikuwa na kitu lakini hukujali, ulinipenda na umasikini wangu, licha ya kuwa ulikuwa mrembo Sana,
Nimekumbuka sauti yako nyororo na macho yaliyolegea.

Ulinichagua katika ya wanaume wengi walionizidi sifa za kihadhi, kifedha na hata kielimu.

Popote Ulipo Anastazia Benedicta jua Michael bado anakupenda,

Ulikuwa unaishi Kwa Aunt yako pale Kwenye Kota za mapolisi Moshi mjini, Nyumba yenu ilikuwa mkabala na uwanja wa mashujaa wa pale Moshi mjini.

Nimekumbuka mara ya mwisho tulivyokutana mida ya saa mbili chini ya lile sanamu la mwanajeshi pale uwanja wa mashujaa. Mpaka leo nakumbuka Marashi yako mpaka hivi leo.

Ile zawadi uliyonipa nimeitunza mpaka Leo Kama ukumbusho.

Anneth popote Ulipo nakuomba ujitokeze. Kama kuna mtu humu anamjua Aneth aliyekuwa anaishi na Aunt yake pale Kota za polisi uwanja wa mashujaa naomba amtaarifu Mick ninamtafuta Sana.

Aneth nakupenda Sana. Hata kama umeolewa, sitajali, ninachotaka nikuone roho yangu ipumzike jamani
Mkuu chukua tu tahadhari mapema, kama alikuwa anaishi kota za polisi, kuna uwezekano mkubwa aliolewa na njagu. Omba tu asiwe ni mke wa afande Kingai!

Mwaka 2014 simu za mikononi na barua pepe zilikuwepo, ina maana ulishindwa kuwa mawasiliano ya aina hiyo zaidi ya kuonana naye ana kwa ana tu!
 
Hi!

2014 ulinipenda pasipo chochote, sikuwa na kitu lakini hukujali, ulinipenda na umasikini wangu, licha ya kuwa ulikuwa mrembo Sana,
Nimekumbuka sauti yako nyororo na macho yaliyolegea.

Ulinichagua katika ya wanaume wengi walionizidi sifa za kihadhi, kifedha na hata kielimu.

Popote Ulipo Anastazia Benedicta jua Michael bado anakupenda,

Ulikuwa unaishi Kwa Aunt yako pale Kwenye Kota za mapolisi Moshi mjini, Nyumba yenu ilikuwa mkabala na uwanja wa mashujaa wa pale Moshi mjini.

Nimekumbuka mara ya mwisho tulivyokutana mida ya saa mbili chini ya lile sanamu la mwanajeshi pale uwanja wa mashujaa. Mpaka leo nakumbuka Marashi yako mpaka hivi leo.

Ile zawadi uliyonipa nimeitunza mpaka Leo Kama ukumbusho.

Anneth popote Ulipo nakuomba ujitokeze. Kama kuna mtu humu anamjua Aneth aliyekuwa anaishi na Aunt yake pale Kota za polisi uwanja wa mashujaa naomba amtaarifu Mick ninamtafuta Sana.

Aneth nakupenda Sana. Hata kama umeolewa, sitajali, ninachotaka nikuone roho yangu ipumzike jamani
Yaani unamuulizia mke wangu?
Njoo umsalimie tuko hapa Mwanga

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Hii ndio tunaita Karma, what you put in is what you get out.... Shikamoo mapenzi hisia zinazochoma zisizoisha utamu
 
Back
Top Bottom