Hello wanajamvi,
Tuko hapa tena tukiongelea uchaguzi.
Kama ambavyo tutakua tunajadili uchaguzi 2025.
Nothing is going to change, CCM itaendelea kuongoza tena na tena
I just think we need us makamanda to have a big debate on how to fight this Enemy... (which is a focus of this thread)
Kwangu mimi most ni upinzani kupenetrate rural areas, Miji mikubwa kama Arusha, Dar, Mwanza tayari kuna MUAMKO ndio maana Hata uchaguzi wanajitokeza watu kwa wingi... hata kampeni zake hazihitaji nguvu sana. I think more effort ipelekwe vijijini, sikumbuki niliona wapi kwamba 80% ya watanzania wanaishi vijijini.. so it make sense UPINZANI KUWEKEZA NGUVU ZAKE HUKO .... (How? Makamanda tusaidiane hapa)
Mimi jibu langu hasa ni kuweka mkakati in the next five years CHADEMA ikuze vyanzo vyake vya mapato (makamanda hapa tusaidiane HOW). CHADEMA pia ifungue CHARITY yake, kwa mfano tunaona MKAPA, JAKAYA KIKWETE FOUNDATION, ila sijaona kiongozi yeyote wa upinzani mwenye charity yake, LISSU una exposure ni mtu unajulikana kimataifa ukifungua CHARITY utakua suppprted ndani na nje ya nchi, fungua lengo ni kuimprove rural areas residents na Watanzania wote kwa mapana, identify kila kijiji kinahitaji nini, then unatoa SOLUTIONS.
Kama ni maji, vyoo vya shule, ama kujenga hospitali shule trust me within FIVE YEARS, UTAKUA UMEKUWA KARIBU NA WANANCHI NA PIA UTAKUA NA PROJECTS zitakazokusaidia kuomba kura, sio sasa hivi Magufuli anasema nimejenga hiki kile, halafu wewe unakua ni mtu wa kupromise tu nitafanya hiki kile. Ukiwa na projects ulizozipatia solutions , wewe pia utakua na projects za kuonyesha kwenye uchaguzi ujao.
Makamanda toeni mawazo yenu, karibuni