Maabara ya Kituo cha Afya Kigamboni inatumia vifaa vya kupimia Malaria visivyoaminika.Vifaa hivyo vinadaiwa kutolewa kwa msaada na Marekani.Watu na Watoto wanaopimwa Malaria kwa kutumia vifaa hivyo huonekana hawana malaria,lakini wakienda sehemu nyingine huonekana na malaria.Wakati mwengine mgonjwa huzidiwa kwa kupimwa na vifaa hivyo na kuonekana hawana malaria.Vifaa hivyo vinaonekana vinaweza kutumiwa na zaidi ya mgonjwa mmoja,je ni salama kwa afya?na vifaa vyenyewe vimethibitishwa ubora?Ni vizuri Wizara ya Afya ikafutilia na kuhakiki ubora wa vifaa hivyo.Wana JF mwenye zaidi kuhusu hili aturushie.