Miaka karibu ishirini iliyopita kipindi nilipobalehe siku moja nikiwa bafuni naoga nilisikia sauti ya dada mmoja wa jirani akiongea na wenzake na kucheka ktk hali isiyo ya kawaida nikamtamani na kuanza kuvuta hisia nikifanya naye mapenzi na kwa mara ya kwanza nikaanza kupinga punyeto, ukawa ni mwanzo wa safari ambayo imenifikisha sehemu nisiyotamani kabisa kuwepo.
Kama kuna wengine hili kwao halina madhara basi kwa upande wangu limekuwa tatizo kubwa sababu tangia hapo ukawa ni mchezo wa almost kila siku, nikimwona mdada yuko nusu uchi hata kwenye tv mm tamaa inawaka najimaliza kwa punyeto. Wadada wa bongo movie wengi sana nimeshawapigia punyeto yaani nikiona tu mapaja au chupi tu kwangu ni tatizo moyo unaenda speed lazima nipige punyeto.
Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na vijarida vinaandika story za picha za mapenzi nilikuwa navinunua usiku navitumia kuvuta hisia huku napiga punyeto. Kwa sasa almost kila siku niko xvideos napakua video za porn za kila aina nikiwa naangalia namaliza hapo hapo, najisikia hatia nafuta video zote ila kesho yake nazipakua nyingine mchezo unaendelea, nimeshatuma sana elfu tano tano kwa wadada ili wanitumie picha zao na video zao za uchi au sometime kufanya sex video call.
Nimetamani sana kuacha, nimeomba na kuombewa lkn bado, nimejiwekea resolutions mara nyingi ya kuwa sasa naacha, nitajitahidi kujizuia kwa muda kama wiki mbili au tatu baada ya hapo narudi tena kwa nguvu mpya yaani ni kama nakuwa nakusanya nguvu tu ya kurudia upya na hasa kwa kuwa mara nyingi mawazo ya kuacha porn&punyeto huja baada ya kufanya punyeto kwa siku mfululizo so nahisi mwili huwa umechoka/kukaukiwa hivyo akili inakuwa imekaa sawa, ila zikishaongezeka tu mwili unaanza kusukuma kutafuta porn video na kupiga punyeto.
Kuna kipindi smartphone iliharibika nikawa natumia kitochi hapo ndio nilikaa kama miezi 3 kwa sababu sikuwa na means ya kuangalia porn, ila siku nilipopata tu smartphone nilikaa kama wiki mchezo ukaanza upya. Nikiwasha data huwa najisemea leo siingii xvideos so nitaperuzi vitu vingine ila mawazo yatanisukuma tu kwenda xvideos tatizo nikiaanza kuzipakua hadi kuja kumaliza na mwishowe kupiga punyeto mwili na akili vimechoka.
Binafsi hiki kifungo na hizi tabia zimenichosha sana na yako mambo ktk maisha yangu nayaona sasa naamini yako linked na hizi tabia, mimi ni mvivu hasa wa kutenda mambo, nimekuwa mwoga mwoga hivi, muda naotumia kuangalia na kupakua porn kama ningekuwa nautumia ktk mambo ya maana naamini ningekuwa ningepiga hatua zaidi ya niliyopo sasa.
Jana nimeangalia porn mpaka nikakosa kitu cha kuangalia maana vyote nimeshaviangalia mpaka intrest imeisha na hili nalo likanipa hofu sana hadi nikajiuliza kama nimejisikia hivi, nini kitafuata? Ninaamini hii ni ishara nyingine kuwa inabidi nitoke kwenye hili shimo nililoingia.
Nimeishi maisha yenye sura mbili kwa miaka yote hii na sasa natamani niishi maisha ya aina moja yaliyo safi, kuna watu wananiheshimu sana na kuniona mtu wa maana na muhimu sana hata kunishirikisha mambo yao mazito mazito ili niwashauri, huwa najisemea tu kuwa hawajui kuwa mm ni mchafu zaidi yao, ni dhaifu zaidi yao na si msafi kama wanionavyo nje na hili linanisumbua sana natamani niishi maisha safi nje na ndani.
Wale mliowahi kupambana mkashinda ktk changamoto kama hizi naomba ushauri, maana nimedhamiria kabisa kuwa siku ya jana tarehe 05/09/2019 ndio iwe siku ya mwisho ya kupiga punyeto na kujihusisha na pornography na ninaamini "one day at a time" nitafanikiwa.
Natanguliza shukrani kwa ushauri na support nitakayopata hapa.