Upi mtazamo wako juu ya kipindi maarufu cha Jahazi kufungiwa?

Jamaa kauliza mitazamo ya watu. Watu wakitoa mitazamo anaipinga.
 
Kuna vipindi havihitaji kuwa seriously na kukaza uso ili kukiendesha.
Ni soga tu Kama kijiweni na kipindi kinaenda swaafi kabisa.

La muhimu kusiwe na maneno mengi yenye ukakasi Kama aliyokuwa anayatoa Marehemu Kibonde..yule alikuwa mropokaji haswa

Radio nyingi na hata vituo vya TV hapa nchini vipindi ni hovyo tu, wanaita ni radio za burudani lakini hata burudani ina uwasilishaji wake basi!
 
Kipindi Changu Safi Cha wakubwa ni MAZUNGUMUZO YA FAMILIA pale redio one siku ya jumapili. Hakina matangazo na unajifunza na kuburudika. Hawa wwngine acha wafungiwe tu.
 
Yote? Kivipi??
Kama hivyo
Screenshot_20200827-164203.jpeg
 
Hii kasumba ya kuokoteza watu waropokaji wasio na weledi na kuwapa vipindi haina afya kwa tasnia ya habari, eti wanaojiita ‘wachekeshaji’ ndo wamekuwa watangazaji!!
Hakuna watangazaji hapa, hakuna wahariri na hakuna waongozaji. Ni vikundi vya wahuni vinavyokutana kupiga soga kwenye vipaza sauti. Periodt

Kila kipindi wanakuja kufreestyle tu. Ukiwauliza wanataka kuachieve Nini mwisho wa kipindi chao.. hakuna anayejua.

What are the news bits, ili tuwapime mwisho wa kipindi? Kama walifanikiwa... hakuna ajuaye.. Ni patashika nguo kuchanika na sio uwadhaniao. Wanapopita ukiwauliza... Hakuna ajuaye..

Na ukiitisha kila redio Leo hii...waje na work plan ..utashangaa ..vichwani empty empty tupu. Yaani wanaongozwa na hype..

Wakishangiliwa wanashikiria humo humo. Kwa wanahabari huo ni uzwazwa lazima uwe controller of the narrative..sio unazurula tu Kama kucheza kiliwanzenza.

Mwana habari wewe Ni mwalimu wa Umma. Sasa unaachaje wanafunzi(Umma) wakuendeshe kisa unasifiwa.. unakuwa punguani. Unaropoka kila ujinga bila kujua hadhira yako ni mchanganyiko kwa muda ulioko hewani.

Kwenye daladala watoto wanatoka mashuleni wapo wazee, walimu wao na kila Aina ya watu...mtu Mzima upo redioni umekazana na pungeto..

Hawa watu wanahitaji bodi. Wakitoka shule wakakae Kwanza kwenye kukusanya taarifa na kuhariri mpaka waive ndio wapewe nafasi ya kukaa nyuma ya vipaza sauti. Na huko wakizingua leseni inafutwa na akae miaka minne akijifunza ndio arudi tena kwa kusoma ripoti za mikoani.

Upuuzii hatutaki.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Leo nimesikia wamefungiwa wiki mojahiyo radio kwa kutangaza habari za wagombea ubunge kupita bila kupingwa bila ya kuwa na uthibitisho.
 
Siku ya jana, tumeshuhudia na kusikia hukumu iliyotolewa na Mamlaka ya mawasiliano Tanzania juu ya kipindi maarufu cha Jahazi kinachoruka kupitia Clouds Fm.

Hukumu hiyo imekuja baada ya watangazaji wa kipindi hicho akiwemo G. Habash, Dj Fetty na wenzao kukiuka miiko na maadili ya utangazaji.

Watangazaji hao kupitia kipindi hicho kilichokuwakikiruka kila siku za wiki kuanzia majira ya saa 10 alasiri walisikika wakihamasisha jamii kufanya tendo la kujichua yaani "Punyeto". Jambo ambalo ni kinyume na maadili ya jamii yetu na kuwafunza tabia mbovu vijana na watu mbalimbali.

Baada ya kipindi watangazaji pamoja na msimamizi wa kipindi, Abdul Chembea, msimamizi wa maudhui wa Clouds, Seba Maganga pamoja na Sheba Kusaga waliitwa na kuhojiwa. Wote walikiri makosa hayo na uongozi wa Clouds uliwachukulia hatua za kinidhamu watangazaji wawili, mmoja akisimamishwa kazi mwezi mmoja na Dj Fetty akisimamishwa kazi wiki mbili.

Pamoja na hayo, Mamlaka ya mawasiliano Tanzania wanasema kuwa, vitendo hivyo vimekuwa vikijirudia rudia kwa watangazaji wa kipindi wa kipindi hicho ambapo, mwezi June mwaka huu waliitwa kutokana na kukiuka miiko na maadili ya utangazaji wakiwa katika kipindi hicho na walikiri kosa na kupigwa faini ya million 5.

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, imekifungia kipindi hicho na kuwaambia CMG wasizalishe kipindi kingine tena chenye maudhui yanayofanana na kipindi hicho katika muda husika. Pia, wamepewa rai ya kuwapa mafunzo watangazaji na wasimamizi wa vipindi juu ya miiko na maadili ya utangazaji. Kadhalika, kuzihariri taarifa na maudhui ya siku husika kabla ya kwenda hewani.

Watu mbalimbali wapenzi na wafwatiliaji wa kipindi hicho wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii. Wengine wakisema kuwa walikuwa wanafanya 'comedy'. Wengine wakisema hivyo ndivyo kipindi kinachangamka kwani hakuna mtu anaeyazingatia.

Upi mtazamo wako?
CLOUDS FM/TV NI WATOVU WAKUBWA WA NIDHAMU
ADHABU IONGEZWE pia watu wao hawana taaluma yeyote ya uandishi
 
Back
Top Bottom