Pyepyepye
JF-Expert Member
- Jan 6, 2017
- 1,940
- 3,825
Leo asubuhi katika pitapita zangu, nimekutana na watoto wadogo wakiwa wamebeba mizigo ya kuni kichwani, nikajikuta nimekumbuka tukio muhimu maishani mwangu ambalo nimeona tushirikiane tu kulitafakari, pengine linaweza kuongeza kitu fulani katika malezi ya watoto wetu.
Miaka 17 imepita sasa, jumapili moja tulienda kuchanja kuni, baada ya kuridhika na viwango vya mizigo yetu, mimi dada yetu na mdogo wangu tukajitwika mizigo ya kuni zetu kichwani tukaanza safari, njia tuliyokuwa tunapita kuelekea nyumbani, ilipita kwa bibi (mdogo wa bibi alotuzalia mama)
Baada ya kufika kwa bibi tukashauriana tuiache ile mizigo pale maana tulikua tumechoka na mizigo ya kuni ni mizito. Kweli tukapita kwa bibi tukatua mizigo yetu tukamwambia tutaifata kesho baada ya kutoka shule, bibi akatugea msosi tukapiga tukaenda zetu home, mambo megine yakaendelea.
Siku iliyofuata jioni mimi na mdogo wangu tukaenda kuichukua mizigo yetu ya kuni, hapo ndo nikagundua ile mizigo ilikua mizito, maana kwa umbali wa kama 2.5km na mzigo kichwani tulipumzika mara kadhaa, mpaka tulipofika nyumbani.
Baada tu ya kufika nyumbani na kutua ule mzigo kichwani mama akaanza kutugombeza kwanini tumechelewa akasema maneno mengi, kilicho niumiza ni kubeba mzigo mzito kichwani na nilipoufikisha nikatukanwa. Niliumia mno.
Tukaenda kuoga mie na mdogo wangu kisha tukatoka kuelekea barabarani tukivuta muda bi mkubwa amalizie kupika tuufinye, coz nyumba yetu ilikua katikati ya mji. Tukiwa hapo, bi mkubwa akaja kutuita, sie tukajua msosi tayari.
Ile tumemfikia akatukumbatia kisha akatuomba msamaha, ndo kusema "nilijua mlikua mnacheza njiani ndo maana niliwatukana na nilipanga kuwapiga, kumbe kweli kuni ni nzito" yaani nilihisi kukabwa kooni nikajikuta nalia kwa uchungu na furaha ikiwa imechanganyika, mama akanibembeleza hapo nikanyamaza akatuomba msamaha. "NAOMBA MNISAMEHE WANANGU" Kauli hii imegoma kufutika kichwani.
Miaka 17 imepita sasa, jumapili moja tulienda kuchanja kuni, baada ya kuridhika na viwango vya mizigo yetu, mimi dada yetu na mdogo wangu tukajitwika mizigo ya kuni zetu kichwani tukaanza safari, njia tuliyokuwa tunapita kuelekea nyumbani, ilipita kwa bibi (mdogo wa bibi alotuzalia mama)
Baada ya kufika kwa bibi tukashauriana tuiache ile mizigo pale maana tulikua tumechoka na mizigo ya kuni ni mizito. Kweli tukapita kwa bibi tukatua mizigo yetu tukamwambia tutaifata kesho baada ya kutoka shule, bibi akatugea msosi tukapiga tukaenda zetu home, mambo megine yakaendelea.
Siku iliyofuata jioni mimi na mdogo wangu tukaenda kuichukua mizigo yetu ya kuni, hapo ndo nikagundua ile mizigo ilikua mizito, maana kwa umbali wa kama 2.5km na mzigo kichwani tulipumzika mara kadhaa, mpaka tulipofika nyumbani.
Baada tu ya kufika nyumbani na kutua ule mzigo kichwani mama akaanza kutugombeza kwanini tumechelewa akasema maneno mengi, kilicho niumiza ni kubeba mzigo mzito kichwani na nilipoufikisha nikatukanwa. Niliumia mno.
Tukaenda kuoga mie na mdogo wangu kisha tukatoka kuelekea barabarani tukivuta muda bi mkubwa amalizie kupika tuufinye, coz nyumba yetu ilikua katikati ya mji. Tukiwa hapo, bi mkubwa akaja kutuita, sie tukajua msosi tayari.
Ile tumemfikia akatukumbatia kisha akatuomba msamaha, ndo kusema "nilijua mlikua mnacheza njiani ndo maana niliwatukana na nilipanga kuwapiga, kumbe kweli kuni ni nzito" yaani nilihisi kukabwa kooni nikajikuta nalia kwa uchungu na furaha ikiwa imechanganyika, mama akanibembeleza hapo nikanyamaza akatuomba msamaha. "NAOMBA MNISAMEHE WANANGU" Kauli hii imegoma kufutika kichwani.