Upendo Nkone amuomba msahama Martha Mwaipaja

Upendo Nkone amuomba msahama Martha Mwaipaja

Mawele

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2023
Posts
424
Reaction score
1,281
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Upendo Nkone, amemuomba radhi Mwimbaji mwenzake Martha Mwaipaja kufuatia kauli aliyoitoa kwenye moja ya mahojiano, akidai kuwa aliwahi kutishiwa Maisha kupitia simu.

Sakata hilo limeibuka leo katika mitandao ya kijamii, baada ya Martha Mwaipaja kuchapisha video akimtaka Upendo Nkone kueleza kwa ushahidi wa kisheria ni lini na wapi aliwahi kumtishia Maisha, pamoja na madai ya kuwasiliana naye kwa simu. Kauli hiyo ya Martha imeonekana kumlazimisha Upendo Nkone kujitokeza hadharani na kuomba msamaha.

Akizungumza, Upendo Nkone amesema kuwa yeye ni Mkristo na anaamini katika msamaha, hivyo ameona ni vyema kuomba radhi kwa kauli aliyoitoa kwenye mahojiano aliyofanya na Lilian Mwasha.

Akizungumza na AyoTV, Nkone amesema “Kazi ya Shetani ni kugombanisha na kuchonganisha Watu. Inawezekana sikupaswa kulisema suala hili hadharani, nilipaswa kubaki nalo kimya. Lakini nilipohojiwa, nikajieleza, na sasa naona imeleta madhara.

Nipo hapa kumuomba msamaha Mwimbaji mwenzangu Martha Mwaipaja. Naomba anisamehe popote nilipomuumiza au kufanya jambo ambalo hakulipenda. Halikuwa lengo langu. Mungu hapendi mvutano, anapenda amani. Nilizungumza kama simulizi ya jambo lililopita, lakini kwa sasa nashusha moyo na kumuomba anisamehe.” Amesema Nkone.
 
759646c1-5ab6-4df3-b436-bf1f4ec76e2b.jpeg
 
Wanazozania nini hawa wapendwa? Kwa nini huyu mdogo atake mwenzake mama mtu mzima athibitishe? Si angekaa kimya tu na kuja na wimbo wa kumfumbafumba kuliko kumsanua mwenzake kwa watu wa mataifa? Huko ni kukosa hekima na busara ya kiungu
 
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Upendo Nkone, amemuomba radhi Mwimbaji mwenzake Martha Mwaipaja kufuatia kauli aliyoitoa kwenye moja ya mahojiano, akidai kuwa aliwahi kutishiwa Maisha kupitia simu.

Sakata hilo limeibuka leo katika mitandao ya kijamii, baada ya Martha Mwaipaja kuchapisha video akimtaka Upendo Nkone kueleza kwa ushahidi wa kisheria ni lini na wapi aliwahi kumtishia Maisha, pamoja na madai ya kuwasiliana naye kwa simu. Kauli hiyo ya Martha imeonekana kumlazimisha Upendo Nkone kujitokeza hadharani na kuomba msamaha.

Akizungumza, Upendo Nkone amesema kuwa yeye ni Mkristo na anaamini katika msamaha, hivyo ameona ni vyema kuomba radhi kwa kauli aliyoitoa kwenye mahojiano aliyofanya na Lilian Mwasha.

Akizungumza na AyoTV, Nkone amesema “Kazi ya Shetani ni kugombanisha na kuchonganisha Watu. Inawezekana sikupaswa kulisema suala hili hadharani, nilipaswa kubaki nalo kimya. Lakini nilipohojiwa, nikajieleza, na sasa naona imeleta madhara.

Nipo hapa kumuomba msamaha Mwimbaji mwenzangu Martha Mwaipaja. Naomba anisamehe popote nilipomuumiza au kufanya jambo ambalo hakulipenda. Halikuwa lengo langu. Mungu hapendi mvutano, anapenda amani. Nilizungumza kama simulizi ya jambo lililopita, lakini kwa sasa nashusha moyo na kumuomba anisamehe.” Amesema Nkone.
kiki
 
Back
Top Bottom