Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,760
Mwenyekiyi wa Chadema anakaribia Makao Makuu ya Polisi muda mfupi atakuwa anaingia hapo. Police wameanza kukamata watu waliojitokeza kumsindikiza Mwenyekiti. Huku waandamanaji wanapambana na askari wa FFU vikali. Mji mzima ni balaa.
Dodoma Maandamano ya kupinga Bunge la Katiba
Jeshi la polisi jijini Dar es Salaam limetumia mbwa na virungu kuwatanyama mamia ya wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Manendeleo Chadema ambao walifurika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa lengo la kumsindikiza Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ambaye aliitwa kwa mahojiano.
Chanzo: ITV
Dodoma Maandamano ya kupinga Bunge la Katiba
Nipo hapa makao makuu ya polisi jijini Dar es Salam,nimekuja kumsindikiza mwenyekiti wangu Freema Mbowe akahojiwe na hawa polisi,watu ni wengi sana hapa,polisi wametanda kila eneo,pia sura za makachero naziona pia,
kamanda Mnyika kamaliza kuongea na wandishi wa habari na makamanda wengine,anasema mpaka sasa Mwekiti Mbowe hajahojiwa na polisi ,amewakatalia na kuwagomea polisi kuandikisha maelezo kwa shitaka la kutoa maneno ya uchochezi,kuna mabishano makubwa ya kisheria,Mbowe amekubali kuandika kwamba amegoma kutoa maelezo mpaka pale utata wa kisheria utakapoisha.
cha kusikitisha polisi wamewapiga vibaya na kuwaumiza waandishi wa habari wa Daily News na Josephat Isango wa TanzaniaDaima,waandishi hao walijikuta wakipokea kipigo kikali kutoka kwa polisi licha ya kuonesha vitambulisho vyao vya kazi,bt polisi waliendelea kuwapiga mpaka pale mkuu wao alipotokea na kuwazuia,polisi hao waliwapga watu kadhaa walihisi ni wanachama wa CHADEMA.
![]()
Mwenyekiti mwenza wa UKAWA na Mwenyekiti wa chama cha UDP Mch. Mtikila, alifika kwenye viunga vya Makao Makuu ya polisi akiwa ndani ya pikipiki ya mataili matatu maarufu kama Bajaji,huku akipunga mkono wa vidole vi3 kuashiria UKAWA, lakini polisi walimzuia kuingia ndani ya jengo na Mtikila kuwaambia "laiti mngejua kwamba tunachokipigania UKAWA ni kuwakomboa nyie na Watanganyika kwa ujumla msingenizuia"
Attachments
Last edited by a moderator: