Nilidhani wataazimia tamko la majina ya wanufaika wa escrow kupitia Stanbic yawekwe hadharani na wahusika wachukiliwe hatua za haraka.
KAMATI KUU ya CCM iliyokutana leo tarehe 28/8/2015, kuanzia saa nne asubuhi mpaka saa kumi na moja alasiri, imeazimia yafuatayo;
1. Kamati Kuu iliyopita iliiagiza kamati ya maadili kuwaita na kuwahoji wanachama na viongozi watatu waliotajwa kuhusika na kashfa ya Escrow
2. Viongozi hao ni; @ Mheshimiwa Anna Kajumulo Tibaijuka. @ Mheshimiwa William Mganga Ngeleja. @ Mheshimiwa Andrew Chenge.
3. Baada ya Kamati ya Maadili kuwahoji, Kamati Kuu imeazimia kuwasimamisha kuhudhuria vikao vyote vya Chama ambavyo wao ni wajumbe.
4. Ikiwemo Kikao cha Kamati Kuu kwa Mama Anna Tibaijuka na Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kwa Mheshimiwa Chenge na Mhe. Ngeleja.
5. Wakati ambapo kamati ndogo ya maadili ikiendelea na uchunguzi wa kuhusika kwao katika kashfa hiyo.
6. Pia, Kamati Kuu imejadili suala la Adhabu iliyotolewa kwa wanachama wake sita ambao walibainika kuvunja Kanuni na sheria za Chama.
7. Kamati Ndogo ya Maadili imeagizwa kuendelea kuchunguza mienendo ya wanachama hao walioadhibiwa kwa kuanza Kampeni kabla ya wakati.