Mchakato wa kura za Maoni Jimbo la kongwa hatimaye Leo Umefika mwisho baada ya Aliyeongoza kura za Maoni awali Hayati Job Ndugai kufariki Dunia .
Isaya Mngulumi anaongoza"ushindi wa awali wa kura za Maoni Jimbo la kongwa!
Anayefuatia kwa kura ni Dr Samora Mshang'a kwa kuwa mshindi wa pili wa kura za awali katika Jimbo la kongwa!
Wagombea walikuwa 13 ambapo mgombea mmoja ambaye ndo mshindi hakuweza kufanya kampeni kutokana na kufiwa na kaka yake.
Jimbo la kongwa Lina kata 22.
Tarafa 3 Yani mlali Ina kata 10 ,Kongwa Ina kata 5
Zoisa Ina kata 7
Ukitizama wagombea wawili namba 1 na 2
Kwa kura walizopigiwa na wajumbe wa CCM wa mkutano mkuu wa Jimbo la kongwa
Kila mmoja ameshinda kwenye tarafa yake !
Mshindi wa kwanza amepata kata 12 kata 9 ni za Tarafa anayotoka yeye na kata mbili ni tarafa ya Zoisa na kata Moja tarafa ya Kongwa .
-Mshindi namba 2 yeye anatoka kata ya Sejeri tarafa ya Kongwa yenye kata 5 .Ameshinda kata 4 ,huku Tarafa ya Zoisa ameshinda kata 3 na tarafa ya mlali kashinda kata Moja .
Ukitizama hapo utagundua kura zilikuwa zinapigwa kwa ukanda!,
Kwa matokeo ya Jumla ya kura zote mshindi wa kwanza anaongozaa na kwa matokeo ya tarafa mshindi wa kwanza anaongoza tarafa Moja tu ya mlali .
Kwa matokeo ya kata Wingi mshindi wa kwanza anaongoza
Kwa matokeo ya Ushindi wa Tarafa Dr Samora anaongoza tarafa ,2 yani tarafa ya Kongwa na Zoisa .