nashangaaga sana watu wanatafuta fremu kariakoo,huwa najiuliza kwani mpaka ufanikiwe lazima huishi dar?nakupa maujanjatafuta fremu dodoma then pafanye hapo ulipochukua hiyo fremu kama kariakoo yani chukua bidhaa kwa wingi huko kariakoo kwenu zimwage dodoma,matangazo kibao na kuhakikishia utapiga pesa nzuri tui
Kkoo kuna mzunguko mkubwa sana wa pesa na mwingiliano wa watu mkubwa kutoka ndani ya nchi na nje ya nchi tofauti na mji wa kiserikali wa Dodoma ambao wengi ni watumishi wa serikali hasa baada ya serikali kuhamia rasmi pale, sisemi hakuna biashara lakini mzunguko wa biashara bado ni mdogo sana kulinganisha na Kkoo au miji mikubwa mingine licha ya kwamba kwa sasa serikali kwa kiwango kikubwa inajitahidi sana kuboresha mji huo. Ikiwemo kuwekeza katika miundombinu kama vile barabara, majengo, huduma za maji taka, usafirishaji nk. Kikubwa kwa mfanyabiashara ni kuangalia ulipo mzunguko mkubwa wa pesa japo sio mbaya kwa mtu kuanzisha biashara sehemu na kuanza kukua taratibu hatimae biashara kuwa kubwa.
