kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,213
Ndugu wana JF
Nimekuwa nikimsikiliza waziri mkuu Pinda kwenye hotuba zake na anapotoa hoja mbali mbali, nilichogundua ni kwamba waziri mkuu wetu mara nyingi huwa nachagua maneno ambayo yatamfanya abaki neutral kwenye hoja husika, asiiudhi serikali na asiwaudhi wananchi, anataka kufurahisha pande zote, hili haliwezekani kwa siasa za nchi yetu kwa sasa kwa madudu yanayoendelea, na hili ndilo limemfanya Pinda ambaye alikuwa kipenzi cha watu baanda ya kuchaguliwa, kupoteza kabisa ile sifa yake kwa sababu ameonekana ni mnafiki na si mtendaji.
Ni mtu ambaye siku zote anahakikisha analinda kibarua chake hata ikibidi kwa kutoa machozi mbele ya camera.
Mfano mmoja wa unafiki wa Pinda ni kauli yake kuhusu malipo ya Dowans, nakumbuka yeye alisema, suala la Dowans ni gumu, na wanasubri hukumu isajiliwe mahakama kuu ya Tanzania ili wajue kama ni halali basi Dowans walipwe. Tangu wakati huo hajaongea kitu tena hata baada ya kauli za kutaka Dowans ilipwe kabla ya kesi kusajiliwa mahakamani kuu. Ukimuuliza leo Pinda atakwambia yeye hakusema ilipwe, atasema "nilichokisema tusubiri hukumu isajiliwe mahakama kuu tuangalie uhalali wake" na labda atakuja na blabla nyingine nyingi ili tu aonekana mzuri kwa wananchi kwamba hajatamka solidly kwamba Dowans walipwe lakini pia aonekane hapingani na serikali kwa sababu hajasema Dowans wasilipwe. Huyu ni mnafiki mkubwa. Huwa simwelewi.
Vile Vile mheshimiwa Pinda aliwahi kukataa gari mpya aliyonunuliwa lakini akakubali apewe mtu mwingine, yaani yeye aonekane hapendi anasa za magari ya kifahari lakini anaacha wengine wayatumie, huu nao ni unafiki ili aonekane mzuri kwa wananchi lakini asiwaudhi wenzake. Yeye kama waziri mkuu hapaswi kuwa peke yake anakataa magari bali apige marufuku ununuzi wake.
Mh Pinda kuna gazeti moja la kila wiki aliandikwa kuwa anamiliki hisa kwenye kampuni ya usafirishaji abiria ya Sumry based in Sumbawanga, sijasikia akikanusha hivyo inawezekana ni kweli ana hisa, lakini alipotaja mali zake hakusema kuhusu hisa hiza kwa hiyo alitupiga changa la macho?
Mh Pinda soma alama za nyakati, watu siku hizi akikuangalia anajua mpaka unachowaza, kutafuta huruma za wananchi kwa kujiita mtoto wa mkulima au kulia mbele ya camera hakuwasidii watanzania.
Hili la Arusha nalo hatujakusikia zaidi ya kusoma kwenye magazeti kwamba sijui umwemweka kiti moto Mwema, tunataka ufumbuzi wa jambo hili mapema, kitu ambacho waziri mkuu mtendaji angeshafanya. Angalia usijekukaa muda wote na ukaondoka hapo bila cha kukumbukwa, utachekwa kwa kuwa hata Lowasa na skendo zake zote pamoja na kuhalalisha uwepo wa kampuni ya kutuibia ya Richmond lakini kwa kipindi kifupi alichokuwa waziri mkuu alihamasisha ujenzi wa shule na zinaonekana, so far wewe mizengo umetufanyia nini unachojivunia?
Mwenye maoni kuhusu Mh Pinda anakaribishwa. Naomba kuwakilisha.
Nimekuwa nikimsikiliza waziri mkuu Pinda kwenye hotuba zake na anapotoa hoja mbali mbali, nilichogundua ni kwamba waziri mkuu wetu mara nyingi huwa nachagua maneno ambayo yatamfanya abaki neutral kwenye hoja husika, asiiudhi serikali na asiwaudhi wananchi, anataka kufurahisha pande zote, hili haliwezekani kwa siasa za nchi yetu kwa sasa kwa madudu yanayoendelea, na hili ndilo limemfanya Pinda ambaye alikuwa kipenzi cha watu baanda ya kuchaguliwa, kupoteza kabisa ile sifa yake kwa sababu ameonekana ni mnafiki na si mtendaji.
Ni mtu ambaye siku zote anahakikisha analinda kibarua chake hata ikibidi kwa kutoa machozi mbele ya camera.
Mfano mmoja wa unafiki wa Pinda ni kauli yake kuhusu malipo ya Dowans, nakumbuka yeye alisema, suala la Dowans ni gumu, na wanasubri hukumu isajiliwe mahakama kuu ya Tanzania ili wajue kama ni halali basi Dowans walipwe. Tangu wakati huo hajaongea kitu tena hata baada ya kauli za kutaka Dowans ilipwe kabla ya kesi kusajiliwa mahakamani kuu. Ukimuuliza leo Pinda atakwambia yeye hakusema ilipwe, atasema "nilichokisema tusubiri hukumu isajiliwe mahakama kuu tuangalie uhalali wake" na labda atakuja na blabla nyingine nyingi ili tu aonekana mzuri kwa wananchi kwamba hajatamka solidly kwamba Dowans walipwe lakini pia aonekane hapingani na serikali kwa sababu hajasema Dowans wasilipwe. Huyu ni mnafiki mkubwa. Huwa simwelewi.
Vile Vile mheshimiwa Pinda aliwahi kukataa gari mpya aliyonunuliwa lakini akakubali apewe mtu mwingine, yaani yeye aonekane hapendi anasa za magari ya kifahari lakini anaacha wengine wayatumie, huu nao ni unafiki ili aonekane mzuri kwa wananchi lakini asiwaudhi wenzake. Yeye kama waziri mkuu hapaswi kuwa peke yake anakataa magari bali apige marufuku ununuzi wake.
Mh Pinda kuna gazeti moja la kila wiki aliandikwa kuwa anamiliki hisa kwenye kampuni ya usafirishaji abiria ya Sumry based in Sumbawanga, sijasikia akikanusha hivyo inawezekana ni kweli ana hisa, lakini alipotaja mali zake hakusema kuhusu hisa hiza kwa hiyo alitupiga changa la macho?
Mh Pinda soma alama za nyakati, watu siku hizi akikuangalia anajua mpaka unachowaza, kutafuta huruma za wananchi kwa kujiita mtoto wa mkulima au kulia mbele ya camera hakuwasidii watanzania.
Hili la Arusha nalo hatujakusikia zaidi ya kusoma kwenye magazeti kwamba sijui umwemweka kiti moto Mwema, tunataka ufumbuzi wa jambo hili mapema, kitu ambacho waziri mkuu mtendaji angeshafanya. Angalia usijekukaa muda wote na ukaondoka hapo bila cha kukumbukwa, utachekwa kwa kuwa hata Lowasa na skendo zake zote pamoja na kuhalalisha uwepo wa kampuni ya kutuibia ya Richmond lakini kwa kipindi kifupi alichokuwa waziri mkuu alihamasisha ujenzi wa shule na zinaonekana, so far wewe mizengo umetufanyia nini unachojivunia?
Mwenye maoni kuhusu Mh Pinda anakaribishwa. Naomba kuwakilisha.