Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,305
- 9,734
Ndugu zangu Watanzania,
Uongozi wa Rais samia umeleta matumaini katika maisha ya watanzania,umekuwa nuru kwa wanyonge,umekuwa faraja kwa waliokata Tamaa,umekuwa Neema kwa wengi na umekuwa baraka kwa Wote na kuleta furaha katika mioyo ya watanzania. Kwa sasa watanzania wengi sana wana matumaini ya kufanikiwa kimaisha na kila mtu anamatumaini ya kutimiza ndoto zake. kutokana na mazingira wezeshi yaliyo tengenezwa na Rais samia na serikali yake.
Ikumbukwe ya kuwa hakuna jambo linakatisha Tamaa kwa mwanadamu kama kukosa matumaini katika maisha,hata mgonjwa akikosa matumaini hawezi akachukua muda mrefu kuishi hapa Duniani. matumaini huamsha morali katika moyo wa mtu ,huleta nguvu ,huchochea mtu kujituma na kutokukata Tamaa katika jambo fulani hata kama anapitia magumu na vikwazo viliaje ,lakini ni lazima atang'ang'ana kusonga mbele na kupambana kwa kuwa anauona na ana matumaini ya kupata ushindi mbele yake.
Kila mtanzania kwa sehemu yake ana amani kwa kuwa anaona akikaribia kufika kilele cha mafanikio yake,hii ni kutokana na serikali ya Rais samia kuwa muwezeshaji wa watanzania kila mmoja kwa Eneo lake,hii ndio maana unaona serikali ikiwekeza katika ujenzi wa miundombinu ili wakulima wasafirishe mazao yao kwenda sokoni bila shida, hii ndio maana unaona serikali ya Rais samia ikitoa Elimu bure ili kujenga matumaini hata kwa watoto maskini yakuja kupata Elimu mpaka pale wanapohitaji kufika, hii ndio maana serikali ya Rais samia inaboresha huduma za afya katika hospitali za serikali ili watu waone kuwa wanaweza kupata matibabu na huduma nzuri katika hospitali zao na kupona maradhi hata pasipo kwenda hospitali za binafsi ambazo wengi wanashindwa kutokana na gharama kuwa kubwa kwa baadhi ya hospitali.
Hii ndio maana serikali inaboresha maslahi ya watumishi wa umma ili wafanye kazi kwa bidii na kujituma na kuwa na uhakika wa kupata stahiki zao na malipo yao kwa wakati pamoja na viinua mgongo vyao. Hii ndio sababu ya kuona kila mtanzania anachapa kazi na kuwa na matumaini ya kufaidika na jasho lake,hii ndio maana unaona Taifa likiwa limetamalaki kwa amani na utulivu pasipo manung'uniko kutoka kwa watu ,kwa kuwa hakuna aliyefungwa kamba katika shughuli anayoifanya,kila mtu ana nafasi ya kupata fedha na kupata utajiri. Aliye chini ana nafasi ya kupanda juu pasipo kushushwa na serikali ,lakini pia aliye juu anayo nafasi ya kukua zaidi kulingana na juhudi zake mwenyewe.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Uongozi wa Rais samia umeleta matumaini katika maisha ya watanzania,umekuwa nuru kwa wanyonge,umekuwa faraja kwa waliokata Tamaa,umekuwa Neema kwa wengi na umekuwa baraka kwa Wote na kuleta furaha katika mioyo ya watanzania. Kwa sasa watanzania wengi sana wana matumaini ya kufanikiwa kimaisha na kila mtu anamatumaini ya kutimiza ndoto zake. kutokana na mazingira wezeshi yaliyo tengenezwa na Rais samia na serikali yake.
Ikumbukwe ya kuwa hakuna jambo linakatisha Tamaa kwa mwanadamu kama kukosa matumaini katika maisha,hata mgonjwa akikosa matumaini hawezi akachukua muda mrefu kuishi hapa Duniani. matumaini huamsha morali katika moyo wa mtu ,huleta nguvu ,huchochea mtu kujituma na kutokukata Tamaa katika jambo fulani hata kama anapitia magumu na vikwazo viliaje ,lakini ni lazima atang'ang'ana kusonga mbele na kupambana kwa kuwa anauona na ana matumaini ya kupata ushindi mbele yake.
Kila mtanzania kwa sehemu yake ana amani kwa kuwa anaona akikaribia kufika kilele cha mafanikio yake,hii ni kutokana na serikali ya Rais samia kuwa muwezeshaji wa watanzania kila mmoja kwa Eneo lake,hii ndio maana unaona serikali ikiwekeza katika ujenzi wa miundombinu ili wakulima wasafirishe mazao yao kwenda sokoni bila shida, hii ndio maana unaona serikali ya Rais samia ikitoa Elimu bure ili kujenga matumaini hata kwa watoto maskini yakuja kupata Elimu mpaka pale wanapohitaji kufika, hii ndio maana serikali ya Rais samia inaboresha huduma za afya katika hospitali za serikali ili watu waone kuwa wanaweza kupata matibabu na huduma nzuri katika hospitali zao na kupona maradhi hata pasipo kwenda hospitali za binafsi ambazo wengi wanashindwa kutokana na gharama kuwa kubwa kwa baadhi ya hospitali.
Hii ndio maana serikali inaboresha maslahi ya watumishi wa umma ili wafanye kazi kwa bidii na kujituma na kuwa na uhakika wa kupata stahiki zao na malipo yao kwa wakati pamoja na viinua mgongo vyao. Hii ndio sababu ya kuona kila mtanzania anachapa kazi na kuwa na matumaini ya kufaidika na jasho lake,hii ndio maana unaona Taifa likiwa limetamalaki kwa amani na utulivu pasipo manung'uniko kutoka kwa watu ,kwa kuwa hakuna aliyefungwa kamba katika shughuli anayoifanya,kila mtu ana nafasi ya kupata fedha na kupata utajiri. Aliye chini ana nafasi ya kupanda juu pasipo kushushwa na serikali ,lakini pia aliye juu anayo nafasi ya kukua zaidi kulingana na juhudi zake mwenyewe.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.