makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Mimi ni mmojawapo wa Watanzania waliokerwa sana na mauaji ya Arusha mjini ya raia 2 Watanzania na Mkenya 1.Tarehe 10/2/2011 wakti WM Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa papo aliamusha hisia kali kuhusiana na mauaji hayo alipokuwa anajibu swali la Mhe.Mbowe(MB)Hai na kiongozi wa upinzani Bungeni.Ndipo Godbless Lema(MB)Arusha mjini kwa kutoridhika na majibu ya Pinda aliomba mwongozo wa Spika kuhusiana na majibu ya WM afanyeje kwa uongo aliousema Pinda Bungeni. Kama kawaida ya Spika Makinda aliwaka na kumtaka Lema alete maelezo ya ushahidi wa kuonyesha kuwa WM amelidanganya Bunge.
Sasa basi mimi napenda kumshauri Mhe. Godbless Lema kuleta uthibitisho wa uhakika ambao utakuwa na mambo ya msingi yafuatayo:
1.Kwamba SI KWELI kuwa polisi wa walianza kupiga risasi za moto mita 50 kabla ya waandamanaji kukifikia kituo cha polisi chenye silaha. Uthibitisho: (1)Waliopigwa risasi na kuuawa hawakuwa mita 50 maana miili ya marehemu na majeruhi haikuuchukuliwa eneo la mita 50 toka kituo cha polisi. (2)Je, mkenya aliyeuawa naye alikuwa anaenda kuvamia kituo cha polisi ili achukue silaha kupeleka wapi?Je,polisi wanaweza kuthibitisha kuwa naye alikuwa ni mwanachama wa CDM? SI KWELI. Huu ni UONGO namba 1.
2. Kwamba SI KWELI kuwa polisi walitaka kuzuia maandamano kwa kisisingizio cha Intelijensia. Maana baada ya mauaji ya tarehe 5/1/2011 maandamano yaliyofanyika siku ya mazishi ya marehemu 2 HAKUKUWA NA ULINZI WA JESHI LA POLISI NA HAKUNA FUJO WALA UVUNJIFU WA AMANI kama walivyodai polisi kwenye maandamano ya tarehe 5/1/2011. Badala yake wana CDM wenyewe ndiyo waliamua kusimamia shughuli zote za mazishiHapa lazima ikumbukwe kwamba siku ya mazishi watu ndiyo wangelikuwa na uchungu/hasira na wangeweza kufanya fujo zaidi. Lakini they proved the Police force totally wrong. No intelligency issue no nothing. Huu ni UONGO namba 2.
3. Kwamba polisi walianza kuwapiga waandamanji kwa risasi za moto,mabomu ya machozi na maji ya washawasha katika eneo la Stand kilomita 2 toka kituo cha Polisi kinachodaiwa kutaka kuvamiwa na waandamanji. Huu ni UONGO namba 3. Urhibitisho: Lema lazima alete PICHA ZA VIDEO kuonyesha maeneo ambayo polisi walianza kurusha risasi za moto.
4. Lema aandae PICHA ZA VIDEO kuonyesha kwamba Polisi walianza kuyashambulia magari ya Wabunge wa CDM kwa kuvunja VIOO v wakitumia virungu huku wakiwanyang'anya simu na vitu vingine vya thamani. Mchumba wa Dk.Slaa ni mmoja wa wahanga waliopigwa sana na kutokwa damu nyingi. Huyu naye hakuwa umbali wa mita 50 toka Police post. UONGO namba 4.
5. Kwamba MIKANDA YA VIDEO YA Polisi iliyo onyeshwa kwenye vituo vya Televisheni ya TBC1 na ITV ilikuwa imechakachuliwa UONGO kwa maana ilikuwa imefutwa kwa maana kuwa EDITED and DELETED some of the sensitive areas,kama marehemu wakipigwa risasi au wakibwebwa kupelekwa hospital or mortuary! Hakuna hizo picha. Uongo namba 5.
6. Kwamba baada ya MAUAJI, Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Vuai Nahodha aliahidi kuvikutanisha vyama vyote viwili CDM na CCM ili wakae meza moja kumaliza mgogoro huu uliopelekea mauaji LAKINI WAZIRI NAHODHA HAKUFANYA HIVO na WALA PINDA HAKUZUNGUMZIA TAMKO HILO LA NAHODHA. Uongo na 6.
7. Picha zote za VIDEO zenye kuonyesha MATUKIO HALISI YA MAUJI ZICHEZWE KWENYE VIDEO PLAYER MBELE YA BUNGE LOTE ili kuweza KUJIRIDHISHA nani MKWELI na nani MWONGO kati ya Mbunge Lema na PM Mizengo Pinda.
8. Naomba wabunge wote na Wanasheria wote wa CHADEMA wakiwemo kina Tundu Lissu na Mabere Marando ili kuweka mkakati wa USHAHIDI WA KUAMINIKA ILI KUWEZA KULITHIBITISHIA BUNGE KUWA CHADEMA WAKO MAKINI NA WANACHOKISEMA.
God bless you Godbless Lema.
Sasa basi mimi napenda kumshauri Mhe. Godbless Lema kuleta uthibitisho wa uhakika ambao utakuwa na mambo ya msingi yafuatayo:
1.Kwamba SI KWELI kuwa polisi wa walianza kupiga risasi za moto mita 50 kabla ya waandamanaji kukifikia kituo cha polisi chenye silaha. Uthibitisho: (1)Waliopigwa risasi na kuuawa hawakuwa mita 50 maana miili ya marehemu na majeruhi haikuuchukuliwa eneo la mita 50 toka kituo cha polisi. (2)Je, mkenya aliyeuawa naye alikuwa anaenda kuvamia kituo cha polisi ili achukue silaha kupeleka wapi?Je,polisi wanaweza kuthibitisha kuwa naye alikuwa ni mwanachama wa CDM? SI KWELI. Huu ni UONGO namba 1.
2. Kwamba SI KWELI kuwa polisi walitaka kuzuia maandamano kwa kisisingizio cha Intelijensia. Maana baada ya mauaji ya tarehe 5/1/2011 maandamano yaliyofanyika siku ya mazishi ya marehemu 2 HAKUKUWA NA ULINZI WA JESHI LA POLISI NA HAKUNA FUJO WALA UVUNJIFU WA AMANI kama walivyodai polisi kwenye maandamano ya tarehe 5/1/2011. Badala yake wana CDM wenyewe ndiyo waliamua kusimamia shughuli zote za mazishiHapa lazima ikumbukwe kwamba siku ya mazishi watu ndiyo wangelikuwa na uchungu/hasira na wangeweza kufanya fujo zaidi. Lakini they proved the Police force totally wrong. No intelligency issue no nothing. Huu ni UONGO namba 2.
3. Kwamba polisi walianza kuwapiga waandamanji kwa risasi za moto,mabomu ya machozi na maji ya washawasha katika eneo la Stand kilomita 2 toka kituo cha Polisi kinachodaiwa kutaka kuvamiwa na waandamanji. Huu ni UONGO namba 3. Urhibitisho: Lema lazima alete PICHA ZA VIDEO kuonyesha maeneo ambayo polisi walianza kurusha risasi za moto.
4. Lema aandae PICHA ZA VIDEO kuonyesha kwamba Polisi walianza kuyashambulia magari ya Wabunge wa CDM kwa kuvunja VIOO v wakitumia virungu huku wakiwanyang'anya simu na vitu vingine vya thamani. Mchumba wa Dk.Slaa ni mmoja wa wahanga waliopigwa sana na kutokwa damu nyingi. Huyu naye hakuwa umbali wa mita 50 toka Police post. UONGO namba 4.
5. Kwamba MIKANDA YA VIDEO YA Polisi iliyo onyeshwa kwenye vituo vya Televisheni ya TBC1 na ITV ilikuwa imechakachuliwa UONGO kwa maana ilikuwa imefutwa kwa maana kuwa EDITED and DELETED some of the sensitive areas,kama marehemu wakipigwa risasi au wakibwebwa kupelekwa hospital or mortuary! Hakuna hizo picha. Uongo namba 5.
6. Kwamba baada ya MAUAJI, Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Vuai Nahodha aliahidi kuvikutanisha vyama vyote viwili CDM na CCM ili wakae meza moja kumaliza mgogoro huu uliopelekea mauaji LAKINI WAZIRI NAHODHA HAKUFANYA HIVO na WALA PINDA HAKUZUNGUMZIA TAMKO HILO LA NAHODHA. Uongo na 6.
7. Picha zote za VIDEO zenye kuonyesha MATUKIO HALISI YA MAUJI ZICHEZWE KWENYE VIDEO PLAYER MBELE YA BUNGE LOTE ili kuweza KUJIRIDHISHA nani MKWELI na nani MWONGO kati ya Mbunge Lema na PM Mizengo Pinda.
8. Naomba wabunge wote na Wanasheria wote wa CHADEMA wakiwemo kina Tundu Lissu na Mabere Marando ili kuweka mkakati wa USHAHIDI WA KUAMINIKA ILI KUWEZA KULITHIBITISHIA BUNGE KUWA CHADEMA WAKO MAKINI NA WANACHOKISEMA.
God bless you Godbless Lema.