Uonevu mashuleni ni janga la kitaifa

Miss Cherry

Member
Oct 2, 2020
36
249
Awali ya yote ningependa kuwatakia wana JF heri ya Mwaka mpya na Mwenyezimungu atufanyie wepesi katika shughuli zetu za kila siku, na bila kupoteza muda ningependa kwenda moja moja kwenye lengo la uzi huu.

Bullying in school is a total mess, watoto wetu wanaathirika kisaikolojia kwa ajili ya uonevu unaondelea mashuleni, kibaya zaidi tunaweza kuchukulia kawaida lakini hii kitu ni mbaya na inaweza kumnyima mtoto amani maisha yake yote.

Nakumbuka kipindi nasoma shule ya msingi nilikua na mwili mdogo maana nilikua nasumbua sana kwenye suala la msosi, nilikua sipendi kula kiasi kwamba wazazi wangu walijitahidi kunipa dawa za kuongeza hamu ya kula lakini haikusaidia.

Sasa kuna marafiki zangu walikuwa wananiita “Chaupepo” yaan nilikua naumia lakini sikua na cha kufanya kwa sababu kweli nilikua chembamba mpaka basi, kuna kipindi nikawa sitaki kwenda shule nalia kabisa na kuomba kuhamishwa lakini wazazi wangu waliona hoja yangu ni dhaifu hivyo ilinibidi kuendelea na shule japo sikua na furaha kabisa.

Turudi kwenye current situation, Kama tujuavyo kipindi hiki cha likizo watoto wa ndugu zetu wanakua majumbani kwa maana shule zimefungwa. Basi bwana kipindi hiki cha sikukuu nikaenda kigamboni kuungana na familia ambapo nimepata fursa ya kukaa na kupiga story na watoto wa kaka yangu ambao walikua shule za bweni.

Mimi huwa nina kawaida ya kujenga urafiki na watoto na wananikubali sana na wapo radhi kuniambia chochote wanachokutana Nacho pindi wawapo mashuleni. Kuna huyu Dogo anaumri wa miaka 11 basi kuna kipindi aliteleza koridoni wakati akielekea bafuni na aliumia kiukweli hadi kupelekea kushonwa nyuzi kadhaa kwenye paji lake la uso. Jeraha lilikua kubwa kwaiyo amebaki na kovu linaloonekana sana usoni.

Sasa wakati tunapiga stori za kuhusu maisha ya shule akaniambia “aunt mimi sitaki tena kurudi kwenye ile shule naomba kuhamishiwa shule nyingine kama anayosoma Husein” (kayumba) nilistuka sana nikahisi kuna kitu kibaya cha kikatili anafanyiwa na wenzie ikabidi nimuweke kirafiki zaidi ili aweze kufunguka.

Nilimchukua nikaenda naye chumbani nikamwambia haya mtoto wangu naomba niambie kila kitu kinachokusumbua na usinifiche, siunajua nakupenda ee? Akajibu yes aunt. Akaanza kuongea kwa uchungu mpaka nikaona machozi yanamlengalenga.

“Teacher kaniambia nina makovu kama kibaka, wenzangu baadhi wananiambia mm ni kibaka sitaki tena kwenda shule, ongea na baba nikasome shule nyingine aunt plz I beg you” aisee roho iliniuma sana, yaan dah!

Nikawa najiuliza hivi walimu wengine wanaakili kweli? Unawezaje kumkashifu mtoto kiasi hicho na unajua kabisa alipata ajali tena akiwa katika mikono yenu? Unawezaje kumwambia mtoto mambo ya kipuuzi tena mbele ya wanafunzi wenzie? Ni ukosefu wa weledi au ni utaahira wa aina gani huu?

Nilichogundua ni kwamba tayari huyu mtoto ameshakua affected na hizi bullying, nikaanza kuongea naye kumuweka sawa na kumsihi kwamba yeye ni handsome sana na hao wenzie wanamuonea wivu tu na kwa mantiki hiyo basi awapuuze maana hawajui walitendalo.

To make it short, suala hili ni tatizo sana na tusipokua makini tutakua na kizazi cha ajabu kwa maana mtoto akishazoea kuonewa kuna uwezekano akakua na roho ya chuki na visasi, kuna umri ambao mtoto ni ngumu kusahau vitu, sasa hii inaweza pia kuharibu psychology ya mtoto completely.

Je ulishawahi kupitia majanga kama haya wakati ulivyokua shuleni au hata mtaani, kukashifiwa, kubezwa au hata kudhihakiwa kutokana na muonekano wako eidha rangi, kimo au vinginevyo? Uliwezaje kuepukana au kupambana na hii hali? Karibuni kwa michango zaidi wakuu.

Natanguliza shukrani
 
Wakati wa kusoma kwangu hasa secondary , niliwahi kupitia hali hiyo ya unyanyasaji , kukashifiwa kisa nilikuwa na chunusi sana

Hali iliyopelekea kuacha shule nikiwa kidato cha tatu ... Shule nilikuwa naipenda ila tatizo ni huko shuleni ukifka mada unakuwa ni wewe,

Nilishindwa kwa kweli" na hivi sikuwa na mtu wa karbu kama mtoa mada wa kunipa moyo ndo na ikawa hivyo ...

Kitu hicho kilinijengea chuki sana kwa class mates wenzangu hadi leo".

Mfano " kuna jamaa mmoja alikuwa anapenda sana kunitania haiwezi kupita siku bila kunitukana yaan nilikuwa najiskia vibaya kiasi kwamba nikawa natoroka shule kwa ajili yake badala ya kutoka sa 8 nikawa natoka sa 4 kwa kumkwepa matusi yake sasa nmeskia juzi kafariki nmefurahi mno "

Najua sio sawa kufurahia matatizo ya mwenzio lakini ndio hali niliyonayo kwa sasa na hao ndugu zangu waliokuwa wananidhihaki mpaka nikaacha shule....

Nikushukuru shangazi kwa kuweza kumpa matumaini mapya huyo mtoto endelea kumjenga kisaikolojia mpaka aone ni kawaida kwenye maisha haya ya duniani...
 
Kwanza kabisa huwa nashangaa sana.

Unampelekaje mtoto aende kusoma boarding??

Shule za day siku hizi zipo nyingi tu mbona.

Zamani watu hata umri ulikuwa mkubwa, mtu anaingia form 1 boarding ana miaka 15 kidogo anajielewa,

sasa siku hizi na huu utandawazi unapelekaje watoto wana miaka 11 huko boarding aisee, Wazazi muwe mnajiongeza basi, hizo boarding ni biashara tu kama ilivyo school bus, Mimi mwanangu shule anayosoma ina biarding waliniambia eti asome boarding ili afaulu vizuri, Nilikataa kata kata huo upuuzi,

Matokeo ya mwanangu huwa anakuwepo 10 bora na nimeridhika, Silaha kuu ni tuition, Kuna mwalimu namletea nyumbani awe anamfundisha kwa saa 1 mchezo umeisha, mwanangu bado ni mdogo anahitaji kukuzwa na wazazi wake, huyu ninae hapa hapa kwangu mpaka anamaliza form 4, Mambo ya boarding yashapitwa na wakati, akiingia sekondari ntamkazania ajifunza kujibu mtihani wa kidato cha nne ntamnunulia vitabu vya maswali na majibu ya mitihani na nitaendelea kumlipia tuition mchezo umeisha, boarding huko hakunaga tuition aisee, bora asome day tu, mimi kama baba yake ninaijua elimu ya Tanzania inahitaji upite mtihani wa taifa kwahiyo namuandaaga apite mitihani, mambo mengine ya boarding naweza kuyalipia ila siwezi kwasababu najua ni biashara tu.

Kuhusu kuonewa huko boarding usipokuwa ngangali utaonewa sana tu, peleka mtoto huko kama unajua kabisa nae ni ngangali, kama unajua mtoto wako ni lege lege, sio mjanja, n.k. usipeleke huko mtoto hata kama ana akili darasani, huko mabwenini kuna mbwa mwitu wenye tabia za ajabu, wakishajua fulani ni mnyonge watamsumbua sana tu.Mtoto atakuja kuf*rw* hivi hivi kwasababu ya makosa anayofanya mzazi wake kufata mkumbo kupeleka watoto boarding.

Wazazi nawaasa wawe wanapeleka watoto wao boarding kuanzia form 5 huko , siku hizi shule zipo nyingi tu za day, hata hizo za boarding zina day, kama unajidanganya kwamba mtoto akisoma boarding ndio atakuwa salama unajidanganya sana, huko boarding mtoto anaenda miezi minne hamuonani akitumbukia shimoni anatumbukia kweli kweli, akisoma day ni rahisi kujua na kumrekebisha.
 
Wakati wa kusoma kwangu hasa secondary , niliwahi kupitia hali hiyo ya unyanyasaji , kukashifiwa kisa nilikuwa na chunusi sana

Hali iliyopelekea kuacha shule nikiwa kidato cha tatu ... Shule nilikuwa naipenda ila tatizo ni huko shuleni ukifka mada unakuwa ni wewe,

Nilishindwa kwa kweli" na hivi sikuwa na mtu wa karbu kama mtoa mada wa kunipa moyo ndo na ikawa hivyo ...

Kitu hicho kilinijengea chuki sana kwa class mates wenzangu hadi leo".

Mfano " kuna jamaa mmoja alikuwa anapenda sana kunitania haiwezi kupita siku bila kunitukana yaan nilikuwa najiskia vibaya kiasi kwamba nikawa natoroka shule kwa ajili yake badala ya kutoka sa 8 nikawa natoka sa 4 kwa kumkwepa matusi yake sasa nmeskia juzi kafariki nmefurahi mno "

Najua sio sawa kufurahia matatizo ya mwenzio lakini ndio hali niliyonayo kwa sasa na hao ndugu zangu waliokuwa wananidhihaki mpaka nikaacha shule....

Nikushukuru shangazi kwa kuweza kumpa matumaini mapya huyo mtoto endelea kumjenga kisaikolojia mpaka aone ni kawaida kwenye maisha haya ya duniani...

Dah! Pole sana Mkuu jitahidi uwasamehe tu ili na ww upate amani ya moyo. Haya mambo ya a athari kubwa sana katika maisha, imagine mpaka unafurahia adui yako kufariki this is way too much, unahitaji kuachia ili uwe huru Mkuu.
 
Dah! Pole sana Mkuu jitahidi uwasamehe tu ili na ww upate amani ya moyo. Haya mambo ya a athari kubwa sana katika maisha, imagine mpaka unafurahia adui yako kufariki this is way too much, unahitaji kuachia ili uwe huru Mkuu.
Amin M/mungu atajaalia na nitawasamehe wote...
 
Kwanza kabisa huwa nashangaa sana.

Unampelekaje mtoto aende kusoma boarding??

Shule siku hizi zipo nyingi tu mbona.

Zamani watu hata umri ulikuwa mkubwa, mtu anaingia form 1 boarding ana miaka 15 kidogo anajielewa.

sasa siku hizi na huu utandawazi unapelekaje watotp wana miaka 11 huko boarding aisee.

Mtoto atakuja kuf*rw* hivi hivi kwasababu ya makosa anayofanya mzazi wake kufata mkumbo kupeleka watoto boarding

Mkuu kila mmoja ana sababu zake za kumpeleka mtoto boarding, wengine inabidi iwe hivyo kutokana na sababu zilizonje ya uwezo wao, suala la watoto kuingiliwa lipo kila mahali, tena huko majumbani ndio balaa zaidi maana hufanyiwa na ndugu wa karibu kabisa, tuwaombee tu watoto wetu wawe salama.
 
Sema tu zamani wale wavulana walikuwa wanatuwekea kioo kuchungulia eti umevaa upi, sasa ndo ukute hujavaa utashangaa
 
Nikiwa darasa la nne Kuna mwalimu wa kike aliwahi kunifukuza kwenye somo lake la sanaa na sayansi kimu, kwasababu nilikataa adhabu yake iliyopitiliza,

Nilipaswa kuinua mawe juu huku nimepiga magoti kwa dakika 60, hakika nilishindwa na kumuomba msamaha lakini alinikatalia, akaunganisha fimbo mbili kwa pamoja anipige kichwani, ikanibidi kukimbia kurudi nyumbani.

kosa langu kupelekea adhabu hiyo nilishindwa kupeleka sanaa ya kamba ya kufungia mifugo yake (alikuwa mfugaji)

Nilirudi shule baada ya wiki kupita, nyumbani nilijifanya naumwa sana hivyo wakaniruhusu kupumzika, hapo shuleni nikamueleza mwalimu wa nidhamu akawa amenisaidia kurudi darasani.

Changamoto iliyofatia yule mwalimu akawa ananitukana darasani matusi hadi ya nguoni, mara nafanana na mbwa nk.

Yule mwl namchukia yeye na kizazi chake.
Wazazi tuwe karibu na watoto kwasababu wananyanyasika na hii huwapelekea kuchukia shule na kuporomoka kitaaluma
 
Aunty mnapelekaje katoto ka miaka 11 boarding?
Ndo maana watoto wa siku hizi hawana adabu maana hawapati msingi wa malezi kutoka kwa wazazi wao.
Peleka mtoto boarding atleast akiwa ordinary level huko walau ukiwa umekafinyanga tayari.
 
Mkuu kila mmoja ana sababu zake za kumpeleka mtoto boarding, wengine inabidi iwe hivyo kutokana na sababu zilizonje ya uwezo wao, suala la watoto kuingiliwa lipo kila mahali, tena huko majumbani ndio balaa zaidi maana hufanyiwa na ndugu wa karibu kabisa, tuwaombee tu watoto wetu wawe salama.
Kama hujasoma boarding kaa kimya tu mkuu uelezewe.... Boarding watoto wanaingiliwa sana sana sana. nina rafiki zangu waalim wa hizo shule nimethibitisha hili, kesi za homo sexuals zipo nyingi ila ni kimya kimya, tena huko kwenye shule za boys ndio usiseme

huku majumbani umekuza tu mambo, yani hadi ndugu kamwingilia mtoto wa kiume labda kapewa masharti na mganga ama ni psycho path, ndio ipo lakini ni nadra sana, ndugu kufanya hivi ni sawa na kumtongoza shemeji yake kwa sms, kitu hicho anachokifanya kinaweza kugundulika kirahisi tu, mtoto unamzidi akili kirahisi tu anasema yote, si rahisi kama unavyofikiria.

Huko boarding wazazi wengi hupeleka watoto kwa mazoea ama mkumbo tu. Mimi ninaijua system ya elimu ya Tanzania ni kufaulu mitihani ya taifa, hayo mambo ya boarding hayana umuhimu, ni vile tu yamekuwa biashara kubwa,
 
Nikiwa darasa la nne Kuna mwalimu wa kike aliwahi kunifukuza kwenye somo lake la sanaa na sayansi kimu, kwasababu nilikataa adhabu yake iliyopitiliza,

Nilipaswa kuinua mawe juu huku nimepiga magoti kwa dakika 60, hakika nilishindwa na kumuomba msamaha lakini alinikatalia, akaunganisha fimbo mbili kwa pamoja anipige kichwani, ikanibidi kukimbia kurudi nyumbani.

kosa langu kupelekea adhabu hiyo nilishindwa kupeleka sanaa ya kamba ya kufungia mifugo yake (alikuwa mfugaji)

Nilirudi shule baada ya wiki kupita, nyumbani nilijifanya naumwa sana hivyo wakaniruhusu kupumzika, hapo shuleni nikamueleza mwalimu wa nidhamu akawa amenisaidia kurudi darasani.

Changamoto iliyofatia yule mwalimu akawa ananitukana darasani matusi hadi ya nguoni, mara nafanana na mbwa nk.

Yule mwl namchukia yeye na kizazi chake.
Wazazi tuwe karibu na watoto kwasababu wananyanyasika na hii huwapelekea kuchukia shule na kuporomoka kitaaluma

So sad
 
Shule zetu bullying ni tatizo kubwa. Na teachers hawama awareness, na wala hawa jali. In my opinion, hizi shule wana jali hela tu, period.
Mtoto ana tatizo la primary nocturnal enuresis, anaitwa kikojozi. Waalimu wala hawana habari.
Bullying ina drastic psychological impact kwa mtoto ambaye yuko affected.
In my opinion, there is a dire need to train our teachers to realise the psychological impact of bullying and not to just concentrate on academics.
Mtoto anaweza akawa na some sort of learning disability and the teachers have absolutely no idea about it.
 
Mkuu upo sawa
Mimi mwanangu kimbo nilitaka mpeleka huko boarding .
Siku aliyoiba kofia ya mwalimu nami nikaivaa siku ya kikao cha wazazi,

Lakini sasa kupitia hapa nimeghairi
 
Wakati wa kusoma kwangu hasa secondary , niliwahi kupitia hali hiyo ya unyanyasaji , kukashifiwa kisa nilikuwa na chunusi sana

Hali iliyopelekea kuacha shule nikiwa kidato cha tatu ... Shule nilikuwa naipenda ila tatizo ni huko shuleni ukifka mada unakuwa ni wewe,

Nilishindwa kwa kweli" na hivi sikuwa na mtu wa karbu kama mtoa mada wa kunipa moyo ndo na ikawa hivyo ...

Kitu hicho kilinijengea chuki sana kwa class mates wenzangu hadi leo".

Mfano " kuna jamaa mmoja alikuwa anapenda sana kunitania haiwezi kupita siku bila kunitukana yaan nilikuwa najiskia vibaya kiasi kwamba nikawa natoroka shule kwa ajili yake badala ya kutoka sa 8 nikawa natoka sa 4 kwa kumkwepa matusi yake sasa nmeskia juzi kafariki nmefurahi mno "

Najua sio sawa kufurahia matatizo ya mwenzio lakini ndio hali niliyonayo kwa sasa na hao ndugu zangu waliokuwa wananidhihaki mpaka nikaacha shule....

Nikushukuru shangazi kwa kuweza kumpa matumaini mapya huyo mtoto endelea kumjenga kisaikolojia mpaka aone ni kawaida kwenye maisha haya ya duniani...
kwaio ulikua mzee wa kuanika ulezi usoni
 
Back
Top Bottom