Kuoneana sasa inakuwa mpaka kwenye mfumo wa maisha.
Shuleni huwezi kutofautisha uonevi kati ya wanafunzi Kwa wanafunzi, nawaalimu Kwa wanafunzi wao.
Vyuoni ndio mpaka mambo ya ngono yanaingizwa, wakufunzi wanawaonea wanafunzi.
Mtaani, nako hali kadhalika, hupati kazi, huduma muhimu Kwa sababu mwenye wajibu huo anakunyanyasa na hakuna pa kukimbilia.
Wanasiasa wananyanyasa wananchi, haijalishi Kwa ngazi gani, mpaka rais, anadiriki kutopeleka huduma za muhimu ambazo nivhski ya kila mlipa kodi kisa hakuungwa mkono kwenye uchaguzi.
Jeshini, bila ya kuyatofautisha, kuoneana baina yao, jeshi moja na jingine, na majeshi Kwa ujumla wao dhidi ya wananchi.
Wafanyakazi popote ni kuoneana tu, wafanyabiashara, baina yao wenyewe na pia na wateja.
Wananchi mitaani, baina yao , na pia majambazi na wananchi.
Kina umuhimu wa Katiba, si tu iwe mpya, bali itakayosimamiwa ili mtu yeyote bila ya kujali umri, alindwe, asikilizwe na kuhakikishiwa haki za utu wake.