Nimepata habari Serikali imeamua kuwanyang'anya na kuvunja nyumba za wananchi wa vijiji vya Kibengu, Wami, Usokami, Mapanda, Ilogombe nk bila kuwapa sehemu mbadala ya kwenda.
Mbunge wa Iringa Vijijini Ndugu Mgimwa ameitisha kikao jana tarehe 19/03/2012 na baadhi wa wanakijiji na kuwaambia Rasilimali ya maeneo hayo yalishauzwa toka Mwaka 1976 hivyo maeneo hayo yatachukuliwa na wenye kumiliki rasilimali.
Wananchi wa maeneo hayo wako hapo toka enzi na enzi leo Serikali inawaambia maeneo yao yameshauzwa toka 1976 bila wao kushirikishwa wala kupatiwa fidia, mbaya imewaambia watafute pa kwenda.
Kwa mfano kijiji cha Kibengu - Mgwao kina nyumba takribani 300 na wakazi wapatao 4,000 wametaarifiwa waondoke kuanzia kesho maana wakati wowote nyumba zao zitavunja.
Je ni kwa namna gani wananchi hawa watasaidiwa?
Naomba kuwakilisha
Wanyalukolo bado wamelala hawapendi kuiga wenzao wa Iringa Mjini waliomchagua Pastor Msiigwa. Nyie na watu aw Morogoro hata wakiwafukuzia Baharini ni sawa tu mtie akili ili 2015 msilogwe mkaichagua CCm. Kuchagua CCm mtahamishwa Kama mifugo na nchi wataiuza kwa wahindi Juzi Jakaya Kikwete ameanzisha kampain ya kuwauzia Akina Somji and Sons Hecta tano tano waendeleze ndoto yake ya kilimo kwanza na Leo kusema waanzishe Benki ya ushirika eti wakulima wapate mikopo yenye RIBA nafuu. Huyu ni juha serikali ya Nyrere ilianzisha CRDB Mkapa akaibinafsisha tatizo la CCM hawajui uchumi. Cha kufanya sio kuanzisha utitiri aw Benki Mara ya akina Mama Mara ya Vikoba Mara ya vijana! This is rubbish just let BOT do it's Regulatory work let them control interest rates. Akina Jakaya na serikali yake sijui walisoma wapi uchumi? Elimu haina regulator hivyo hivyo Kila ambacho mafisadi walichoshikilia no regulation hivi Huko CCM kuna watu au misukule sishangai Masaburi kusema wanafikiria Makalio?