Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Tukubali kwamba Rais amekwazika sana na ripoti ya CAG. Nilipomsikiliza akitamka neno stupid nilimkumbuka Rais wa sasa wa Zambia Hichilema alipowaambia Wazambia kwamba, siku anaingia ofisini alikuta majalada yanayomtaka aidhinishe fedha za magari na samani nyingine za ofisi kwa kigezo kwamba magari na samani zilizotumiwa na mtangulizi wake haziwezi kutumika na utawala wake.
Hoja hii aliikataa na ikawapa picha wasaidizi wake kuelewa yeye ni mtu wa aina gani.
Mhe. Rais naamini anatafakari kuona wale aliowateua wakaamua kutingisha kiberiti, anawaondoa ofisini ili TAKUKURU na taasisi nyingine ziweze kuanza uchunguzi.
Ni vigumu kumchunguza mteule wa Rais akiwa bado yupo ofisin, naamini sasa vyombo vya uchunguzi vinasubiria awafungulie baraba lakini je, amfungulie baraba pasaka hii au baada ya Eid?
Asipomfungulia baraba mapema upo uwezekano mabaraba wakadestroy ushahidi na akiwafungulia mapema anaweza kuwakwaza baadhi walio kwenye mfungo.
Zuhura Yunus tunasubiri kalamu yako imwake wino kuelekea kunako umma wa Watanzania kuwaambia hasira za mama zimeisha? Sitegemei ziishe kimya kimya au ziishe baada ya azimio la Bunge, maana akisubiri kelele za wabunge italeta tafsiri kwamba serikali inasubiri kufundishwa na Bunge.
Pasaka njem, funga njema kuelekea Eid.
Hoja hii aliikataa na ikawapa picha wasaidizi wake kuelewa yeye ni mtu wa aina gani.
Mhe. Rais naamini anatafakari kuona wale aliowateua wakaamua kutingisha kiberiti, anawaondoa ofisini ili TAKUKURU na taasisi nyingine ziweze kuanza uchunguzi.
Ni vigumu kumchunguza mteule wa Rais akiwa bado yupo ofisin, naamini sasa vyombo vya uchunguzi vinasubiria awafungulie baraba lakini je, amfungulie baraba pasaka hii au baada ya Eid?
Asipomfungulia baraba mapema upo uwezekano mabaraba wakadestroy ushahidi na akiwafungulia mapema anaweza kuwakwaza baadhi walio kwenye mfungo.
Zuhura Yunus tunasubiri kalamu yako imwake wino kuelekea kunako umma wa Watanzania kuwaambia hasira za mama zimeisha? Sitegemei ziishe kimya kimya au ziishe baada ya azimio la Bunge, maana akisubiri kelele za wabunge italeta tafsiri kwamba serikali inasubiri kufundishwa na Bunge.
Pasaka njem, funga njema kuelekea Eid.