thadei kimambo
JF-Expert Member
- Jan 31, 2013
- 220
- 126
Vuta picha umelala mida ya alfajiri hivi, usingizi ule wa kukesha jana yake, halafu kuna mtu anakuja kukugongea mlango kwa fujo sana kwenye mida ya saa moja moja hivi.
Ile unaamka kwa hasira kwenda kumfungulia unajikwaa kidole cha mwisho cha mguu katika kona ya kitanda - ile ndiii!, ukaruka kwa maumivu ukapamia ndoo ya maji yakamwagika sakafuni.
Mara unateleza katika yale maji unaangukia meza unaangusha TV, deki na wewe chini mara waya wa umeme unakupiga short mgongoni unafika mlangoni na maumivu ya kidole na uchovu + hasira+hasara na short juu unakutana na jamaa anakwambia nasajili line za simu halafu anakutolea meno kwa tabasamu, eti pozi la biashara.
Sipati picha utamfanyaje?
Ile unaamka kwa hasira kwenda kumfungulia unajikwaa kidole cha mwisho cha mguu katika kona ya kitanda - ile ndiii!, ukaruka kwa maumivu ukapamia ndoo ya maji yakamwagika sakafuni.
Mara unateleza katika yale maji unaangukia meza unaangusha TV, deki na wewe chini mara waya wa umeme unakupiga short mgongoni unafika mlangoni na maumivu ya kidole na uchovu + hasira+hasara na short juu unakutana na jamaa anakwambia nasajili line za simu halafu anakutolea meno kwa tabasamu, eti pozi la biashara.
Sipati picha utamfanyaje?