comfix
Member
- Feb 15, 2014
- 59
- 11
Wakati mwingine kuna matukio ambayo naamini huwa ni nadra kutokea.
Sikia hii: Siku moja nilisafiri kutoka Dar kwenda Mza kwa basi. Katika kiti cha mbele yangu alikaa dada mmoja mrembo, baada ya kufika Chalinze aliniomba nimwitie wale wachuuzi wa bidhaa ndogondogo kwani mimi nilikaa dirishani, baadae safari iliendelea na baada ya kufika Morogoro tulikwenda kupata chai ambapo tulisabahiana na kujuzana ni wapi tunaelekea, alisema anakwenda Nzega then Sikonge kikazi na angerudi baada ya kazi yake kukamilika.
Baada ya wiki mbili mimi nilirudi Dar nikiwa safarini tulipofika Nzega nilimwona yule dada akijongea kulikaribia lile basi nililokuwemo kisha akapanda, amini usiamini alikuwa amepewa seat # kwenye kiti nilichokuwepo mimi.
Tulisafiri km marafiki tukishirikiana kwa kila jambo, alishuka Morogoro na aliniahidi kuwa baada ya shughuli zake atakuja Dar kunitembelea, baada ya siku nne alinipigia simu nikampokee stand.
Nilimkaribisha na kuwa nae kwa siku mbili tulienjoy sana, kisha aliondoka kuelekea Arusha, tuliendelea kuwasiliana kwa simu na email pia, lakini ghafla nikawa simpati kwenye simu hata nikimtumia email hareply.
Sielewi ni nini kilimtokea ukizingatia nilikuwa nimekwisha mweka moyoni na akilini pia. Nasikitika kumpoteza Rachel.
Sikia hii: Siku moja nilisafiri kutoka Dar kwenda Mza kwa basi. Katika kiti cha mbele yangu alikaa dada mmoja mrembo, baada ya kufika Chalinze aliniomba nimwitie wale wachuuzi wa bidhaa ndogondogo kwani mimi nilikaa dirishani, baadae safari iliendelea na baada ya kufika Morogoro tulikwenda kupata chai ambapo tulisabahiana na kujuzana ni wapi tunaelekea, alisema anakwenda Nzega then Sikonge kikazi na angerudi baada ya kazi yake kukamilika.
Baada ya wiki mbili mimi nilirudi Dar nikiwa safarini tulipofika Nzega nilimwona yule dada akijongea kulikaribia lile basi nililokuwemo kisha akapanda, amini usiamini alikuwa amepewa seat # kwenye kiti nilichokuwepo mimi.
Tulisafiri km marafiki tukishirikiana kwa kila jambo, alishuka Morogoro na aliniahidi kuwa baada ya shughuli zake atakuja Dar kunitembelea, baada ya siku nne alinipigia simu nikampokee stand.
Nilimkaribisha na kuwa nae kwa siku mbili tulienjoy sana, kisha aliondoka kuelekea Arusha, tuliendelea kuwasiliana kwa simu na email pia, lakini ghafla nikawa simpati kwenye simu hata nikimtumia email hareply.
Sielewi ni nini kilimtokea ukizingatia nilikuwa nimekwisha mweka moyoni na akilini pia. Nasikitika kumpoteza Rachel.