Acha Urongo wewe!
Uchaguzi ndani ya CCM Mwenyekiti Taifa anashindanishwa na nani?
Usilinganishe mfumo wa kidemokrasia uliopo ndani ya CCM na uliopo CDM.
CCM ni chama kikongwe ambacho kilianza kama chama cha kidikteta na ilikua ni lazima kila msomi,mfanyakazi,na mkulima kuwa mwanachama,jambo ambalo CDM haiwezi kujengwa kwa namna hiyo kwa sasa.
Na pia ni utaratibu wa chama kwa mtu anayeshinda nafasi ya urais anakua pia mwenyekiti wa chama.Huu ni utaratibu wa kuendeleza mfumo wa Chama dola.
Hata hovyo huu utaratibu unakinufaisha chama kinachokua madarakani dhidi ya vyama vingine.
Kwa hiyo CCM wenyewe wameweka utaratibu wa kupita vikwazo vikubwa sana ili mtu aupate uenyekiti jambo linalomfanya apite bila kupingwa.Kikwazo cha kwanza ni cha kupita kwenye kinyang'anyiro cha kugombe urais ndani ya chama.Kikwazo cha pili ni kuingia kwenye uchguzi mkuu wa taifa kwa kushindana na vyama vingine.
Kwa hiyo unaposema Mwenyekiti wa CCM hashindanishi na mtu kwenye nafasi hiyo unasahau vikwazo na ushindani alioupitia mpaka kufikia nafasi ya kupata uenyekiti.
Jambo lingine ni kwamba wakati huu wa mfumo wa vyama vingi ambapo bado hatujapata chama cha upinzani cha kitaifa ili kushindana na CCM yenye wanachama wenye imani kubwa na mapenzi kwa chama, ni vyema kuepuka migogoro midogo midogo ambayo ingeweza kuepukwa.
Mimi mpaka leo najiuliza hivi viongozi na wapenzi wa chadema haowaoni kwamba mgogoro wa Zito kama busara ingetumika usingekuwepo.Na kuwa mgogoro huo unarudisha sana nyuma ustawi wa chama.
Ukweli ni kwamba hakuna uadui kati ya Zito na Chadema kwa maana ya wanachma bali ni mtu au watu wasiozidi watatu ambao wanajali maslahi binafsi ya kisiasa na madaraka kwa kutamani nafasi ya jimbo lake na Unaibu katibu mkuu.Hawa hawatamani kuona Zito anarudi kundini bila kuangalia adhari za kumtosa Zito.Hawataki kuona watu maarufu wanajitokeza ndni ya chama.Hawa ndio maadui wa kubwa ndani ya chama na ndio watakao ua chama kama wataachwa kuendeleza majungu ndani ya chama
Tukubali