Ndugu zangu wana janvi, ploleni na majukumu
Mimi si mwana siasa, ila ni kati ya sehemu kubwa ya kundi kubwa la watanzania linalohitaji mabidiliko, Kwanza kabisa niwapongeze wana siasa wa vyama vya upinzani na wa chama twawala, lakini pia wanaharakati na waandishi wa habari kupitia vyombo vyao vya habari, na hasa Jamii Forum, na wengine wote ambao wameshiriki kikamilifu bega kwa bega, kichwa kwa kichwa,jicho kwa jicho, kuhakisha wanaleta babadiliko na kuwatoa watanzania matongotongo kujua hatima ya nchi yetu.
Ndugu zangu tunapo zungumzia mabadiliko ni kitambo sasa watanzania wamehitaji mabadiliko dhidi ya kinacho itwa utawala dhalimu wa Ccm, ushahidi tosha ni wakati ule mwaka 195 wakati wa Ndugu yetu Agustine lyatonga Mrema hakika watu wale walihitaji mabadiliko. Nawatu wa aina hii wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku, mwaka hadi mwaka.
Kwa namna ya pekee nimpongeza ndugu yetu Mbowe kwani kuongoza chama kufikia hatua ya kuaminiwa namna hii ndugu zangu wa Tanzania tuamini si kazi ndogo wala kuibeza, ikiwa baadhi yetu tunashindwa wakati mwingine hata kujiongoza wenyewe na kuonekana hatufai mbele ya uso wa jamii iliyo tuzunguka , sembuse kikundi cha watu taasisi hata lichama likubwa namna hii? Hapana nasema huyu bwana anastahiki kuheshimiwa ikiwa ni pamoja na kupongezwa na si kubezwa. Ameweka historia ya aina yake kesho na kesho kutwa tutamkumbuka. Binafsi namtakia afya njema . Japo ni kazi ambayo ameifanya kwa ushirikiano mkubwa sana na wenzake, lakini tunasema gari likianguka analaumiwa dereva na si waliomo.
Ndugu zangu uongozi si jambo dogo hata kidogo, sasa chama kimekua naami dhamila ya Mbowe ni njema kabisa mbele ya uso wa watanzania, kweli analo jukumu la kukamilisha kazi kubwa aliyo ianza kitambo, lakini wasiwasi wangu chama kinakua na changamoto zinazidi kuwa nyingi, hapa ndo nahiitaji wachambuzi wa masuala ya siasa watuambie, je! Tathimini ikoje tangu ameanza, na mahali alipofikia.
Je! Ana washauri? Inawezekana jibu ni ndiyo lakini je ni mtii wa kupokea ushauri? Nahitaji watafiti wa siasa zetu wasema wazi kuhusu mzigo mkubwa huu alio beba mwenzetu kama uwezo wake bado unatosha kuufikisha, kwani Chadema imebeba matumaini ya watanzania, watanzania wanaamini bado kitambo kidogo,kuuondosha utawala uliopo madarakani.
Jitokezeni watafiti wa mabo ya siasa mbele ya uso wa watanzania walio jawa matumaini, wekeni maslah ya taifa mbele pasipo ushabiki wa vyama itikadi,dini ukanda. wekeni mioyo yenu wazi tuaambieni watanzania kama bado Mbowe anao uwezo wa kukiongoza chama, na kama ameelemewa mwambieni pasipo kumungunya maneno kama mnaona amechoka asaidiwe, kwani kazi anayo fanya ni yetu sote kwanini aumie pekeyake wakati tunajenga nyumba moja.
nawasilisha