Unazikumbuka enzi za Barua!

Da umenikumbusha mbali mkuu,enzi zile nilikuwa na demu korogwe girls,karatasi lazima iwe ya rangi rangi,mwandiko wa kuremba,michoro ya kufa mtu alafu lazima apulizie perfume.vitu kama hivi ndo huwa vinanifurahisha kwenye mapenzi mpaka leo ninazo hizo barua

weye ulikuwa mitaa wa wapi?,Tanga school,Galanos au Magamba?

 
Nakumbuka Kuna binti fulani kidato cha 5 alijinyoonga baada ya kutumiwa barua ndan yake wameandika kwa toilet paper then mchizi akajichambia. Binti alikua amegombana na mpenz wake wakaachana. Tarime sec hyo!
 
Nakumbuka Kuna binti fulani kidato cha 5 alijinyoonga baada ya kutumiwa barua ndan yake wameandika kwa toilet paper then mchizi akajichambia. Binti alikua amegombana na mpenz wake wakaachana. Tarime sec hyo!

duh duh duh! hao mabinti na mapenzi ya kikurya yako so military
 
No hakua mkurya, alikua mtoto toka Arusha, hata huyo Bf wake alikuwa arusha nadhani ilboru! Mapenzi noma mkuu, enzi hzo nipo kidato cha 3. Kitambo sana!
 
Dah nakumbuka enzi hizo nikiwa sec!unaandika barua unaifunga kwenye bahasha halafu kwenye upande wa kufungulia bahasha unaandika guess who wrote!kazi kweli kwa anaepokea!ilikua safi saaaana!
 
haha, that girl lizzy make my day.....i ddnt ge the chances either to write those colourfull later.but will try to write one as lizzy impess me.:tonguez:
 
Hahaaaaa, umenifanya nichangie fasta hii thread maana juzi nilikua nawafundisha wanafunzi wangu mahali fulani nikawaambia kuwa hawajui kuandika essay kwasababu wao siku hizi wanategemea sms ambazo zimefupishwa kiasi kwamba huwezi jua hata maana yake. Enzi hizo nipo pale Magamba Boys now ( SeKUCo- Sebastian Kolowa University College-Lushoto) ndio nilikua nafanya dili za kuwaandikia washkaji barua halafu wananilipa....serious nilikua bingwa wa kuandika hizo barua hasa kwa lugha ya kigeni maana zilikua zinaenda Mazinde Juu ( St.Mary's) au Kifungilo Girls' ambako ndio by then kulikua na watoto wakali kinoma na ngeli inapanda sana, sasa ukiaka uwapate lazima uandike barua kwa kiingereza.


Nilikua naenda kununua karatasi maalum za kuandikia barua za mapenzi halafu nawauzia jamaa, kisha kama nitaandika Mimi hio barua inabidi uongeze dau! Ndio maisha yangu yalivyokuwa, huwezi kwenda kununua kadi bila kupata ushauri wangu.....next time nitawaeleza kisa nilichokifanya kwa mshkaji aliekua anataka nikamnunulie Card amtumie Demu wake pale Mazinde Juu.

Barua zilisaidia sana kuweza kuandika essay zenye maana na kanuni za uandishi zilizingatiwa......Umenikumbusha mbali saaaaana


mwalimu mimi nilikwambi hadi leo natumia hizo barua..(MIT)
 
jaman mmh! Mlopata ku2miana barua mwanitamanisha kweli, nilishajaribu mara ghafla ndo kukawa na ujio wa cm.ts was real gud i hope.
 
Dah leo nimekumbuka mengi, tulikuwa tukituma barua kupeleka vijijini halafu ndani unaweka pesa. Kwenye bahasha unaweka X watu wanajua ni ya msiba hawafungui tena unampa mtu yeyote tu! akikatisha kijijini kwenu anaitupa dirishani. Sijui ndo kusema siku zile uaminifu ulikuwa mkubwa?
 
Sikubaliani na wewe kwa jinsi ulivyoanisha kwamba kwa text huwezi kubuni/jaza hisia kama ilivyo kwa barua.Binafsi hua naandika text/email ndefu mpaka nashangaa na sio copy n paste mind you.We sema siku hizi watu ubunifu haupo kiwango...hata ingekua lwa barua bado tu wangeandika mistari kadhaa au mingi isiyotoka moyoni(yakuambiwa).Kwahiyo tatizo hapa sio njia ya mawasiliano bali ni watu wanavyowasiliana!!!

Pengine hujanielewa Lizzy, sio wote lakini kama unafuatilia vizuri hii mitandao ya siimu unakuta unatumiwa meseji Tuma neno mapenzi kwenda 1423333 sijui ngapi ngapi utaletewa meseji nzuri za mapenzi.Huduma hii utakatwa 500 kwa mwezi. Hizo ndizo wanazozipenda siku hizi. Kama wewe unabuni zako basi umepata kaharufu ka enzi za barua.
 
Nilishawahiandikiwa barua lakini niikumbukayo mpaka leo ni ile niliyoipokea nikiwa chuoni...........mwandishi alitumia peni za rangi zote nne, nyeusi, kijani, nyekundu, purple na blue..............hayo maneno aliyapanga yakapangika ...............It impressed me kwa kweli sema tu nilikuwa bado kinda na naive kimapenzi sikuwezajiuliza wala baini what it meant kwa Mkaka mzima wa mwaka wa tatu kumuandikia binti wa mwaka wa kwanza barua kama ile........... niliichukulia juu juu tu kuwa alikuwa domo zege ........but kaka wa watu hakuwaga hivyo. Nway everything happens for a reason..........
 
Barua ni nzuri jamani siku moja mupemzi aliandika kabarua then akakapresi kwenye note book wat a feelin it was so gud!
 
hapa naona mnasema tu, ebu mmoja atuandikie barua anayoikumbuka, iwe ameituma au ametumiwa ili angalau tukumbukie, mm kama nimesahau! ebu tumwagieni jamani

Kwako Dena Amsi, Utakapokujua hali yangu mimi na wana JF ni bukheri wa Afya. Hofu ni kwako ulie mbali ya upeo wa macho yetu. Kama barafu umeyeyuka hapa JF, tumejaribu kukutafuta kila kona hatujakuona rafiki.
Nia au madhumuni ya kuandika barua hii ni kutaka kukufahamisha kuwa tunakumiss hapa JF, umepotelea wapi mpenzi au umehamia Face book. Kama tumekukosea tunaomba utusamehe. Au mzee amekuwa mkali siku hizi hataki uonekane hapa JF? Kama kompyuta yako ina Virus tunao wataalam hapa watakusaidia. Mara tu upatapo barua hii tunaomba utumie njia yoyote kutufahamisha wapi uliko. Kama upo kwenye fungate mbona umeondoka bila kutuaga, Jamani dena rudi basi mpenzi wetu.
Namtuma njiwa akuletee barua hii iliyojaa upendo juu yako
Wako akupendae
GAZETI
wasalam!
 
Ni fursa ya kipekee kwa waliopotea jf kuandikiwa barua so guys write to those whom u think they ar nt that much present here jf! as they started before
 
jf wachokozi, yaani natamani nirudi nyuma enzi za primary, nilikuwa na rafiki yangu wa kiume namnunulia kitumbua kimoja ndo anipelekee barua, ila hadi sasa nilizificha huko hom za binti niliyemtongoza drs la 4 na kuniacha tukiwa advance! aaah ona sasa nalengwa na machozi! sirudi tena hapa.
 
Dah! lizzy umeniacha hoooi! nkupe box yangu uniandikie barua kama hii, umeniacha nataabika kwa utamu wa barua. mama cjui ulimwandikia nani! yaani kama ungeniandikia mm ningetangaza ndoa mama. ebu jaribu kuniandikia tuone itakuwaje. nimeipenda na umetumia akili za ukweli mama.
 
Dah! lizzy umeniacha hoooi! nkupe box yangu uniandikie barua kama hii, umeniacha nataabika kwa utamu wa barua. mama cjui ulimwandikia nani! yaani kama ungeniandikia mm ningetangaza ndoa mama. ebu jaribu kuniandikia tuone itakuwaje. nimeipenda na umetumia akili za ukweli mama.

Hahhaha Kamugisha nipe sanduku hilo nipate ndoa fasta!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom