Unayosababu (reasoning) - kipimo cha IQ yako

Unayosababu (reasoning) - kipimo cha IQ yako

Tutor B

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2011
Posts
9,025
Reaction score
6,617
Kila siku utasikia watu wengi wakiongelea kuwa IQ ya watanzania ni ndogo - iko kwenye asilimia 70. Ufafanuzi uko hivi: ni kutokana na matendo ya walio wengi kutotenda kwa sababu sahihi.

ONA HAWA WATU:

1. Siwezi kujenga slop, najipanga nijenge nyumba ya maana (ana miaka zaidi ya 15 anapanga chumba kimoja na sebure)

2. Mwanangu hawezi soma shule za kata (analalamika eti shule wamepandisha gharama na vyuma vimekaza)

3. Siingii kwenye nyumba haijaisha (anaendelea kupanda na anadaiwa kodi miezi 6 nyuma)

4. Siwezi kulima mchicha mjini hapa (ananunua mchicha kila siku)

5. Siwezi kununua gari la hivyo (anapanda bajaji kila siku)

6. Siwezi kulala na mifugo (kuku) ndani ya nyumba (ana bill ya mayai ya mtoto kila mwezi.

ONGEZA NA NYINGINE …

Hicho ndo kipimo cha IQ za watanzania … hawana sababu za msingi kwa yale wanayoyatolea maamuzi. Kama na wewe ni wa hivyo … BADILIKA.
 
Umeshahamia kwenye ile nyumba yako ya chumba na sebule rafiki?
Nakutania tu, tuko pamoja.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Nyuzi kama hizo huwa hazisomwi na zikisoma hazchangiwi.
Inamaana kubwa sana hii kitu nimejifunza hapa
Watu hawapendi kuambiwa ukweli - hapa kuna wengine wamelog out kabisa baada ya kuona huo uzi mkuu.
Mi naongeza nyingine ...
Siwezi kumuoa mhudumu wa bar ... (alafu anafanya naye mapenzi tena bila kinga!)
 
Umenifanya nicheke peke yangu mkuu ...
Kujitolea kufanya kazi walau apae hata nauli na lunch - hataki anasema siwezi kufanya kazi bila mshahara - ANASHINDA KIJIWENI .. HAPO KIJIWENI UNALIPWA NA NANI? TENA HUYO ANA DEGREE KABISA!
 
Watu hawapendi kuambiwa ukweli - hapa kuna wengine wamelog out kabisa baada ya kuona huo uzi mkuu.
Mi naongeza nyingine ...
Siwezi kumuoa mhudumu wa bar ... (alafu anafanya naye mapenzi tena bila kinga!)
Hahahaaa [emoji28] [emoji28] [emoji28] , siwezi oa mwanamke mweupe nataka black, wakati huo huo kaoa black anayepaka mkorogo
 
Hahahaaa [emoji28] [emoji28] [emoji28] , siwezi oa mwanamke mweupe nataka black, wakati huo huo kaoa black anayepaka mkorogo
Ulweso! wabongo wanajidanganya wenyewe! Uzi huu sijui niupeleke kwenye MMU labda!
Nimeipenda hii ...
 
Ulweso! wabongo wanajidanganya wenyewe! Uzi huu sijui niupeleke kwenye MMU labda!
Nimeipenda hii ...
Ukweli unauma hawata kuja unafiki mwingi sana eti hawauoni, wanapita pita kama mlosaji nani katupia asome basi [emoji28] [emoji28]
 
Siwezi jenga nyumba uswahilini mimi!Bora nipange tu nyumba yenye geti...analipa kodi million 3 kwa mwaka kiwanja hana huyo.
 
Kwa hiyo kila kitu ambacho unatumia kwa chakula unachokiponda unatakiwa ulime ndio IQ inakua kubwa?
 
Back
Top Bottom