CPU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 3,863
- 686
Pumba kila mtu huwaga anazitoa. Na huwezi ukazuia watu kutoa pumba kwa sababu hoja kama ni pumba au la inategemeana na mtazamo wa mtu.
Kuna wengine tu, kwa mfano wale wasiompenda Nyani Ngabu, wanaweza kabisa kuona hata hiki nilichoandika hapa ni pumba na wengine wakaona nilichoandika ni kuntu. Pumba za maoni hazina vipimo wala chujio linalokubalika na wote.
Cha msingi ni kuwa mvumilivu na muelewa wa maoni yaliyo tofauti na ya kwako. Kuna wengine 'jiwe' mwenzio analiona 'mkate'. Sasa katika hali kama hiyo ni uelewa tu ndiyo unaohitajika ili kusonga mbele pasipo na kukwazana.
Miafrika Ndivyo Tulivyo.