Blue G
JF-Expert Member
- Jun 20, 2012
- 5,339
- 3,673
It's like this SnowBall binadamu tumeumbwa tukiwa na uwezo wa kujenga picha akilini na kuumba kitu akilini eiza kutokana na sauti,picha au masimulizi,kwa hiyo wapo ambao huweza kusikia sauti na kujenga picha akilini kuwa huenda huyu mtu akawa wa namna fulani na tabia fulani,na wengine huweza kusimuliwa habari kumhusu mtu fulani na kuweza kupata picha kuwa huenda mtu huyo ni wa namna fulani.Na kupitia hiyo picha aliyoijenga akilini mwake hujikuta akiwa na hisia za upendo kumwelekea mtu wake aliyemuunda kichwani mwake.
Kwa hiyo kwa ufupi kwa upande wangu mimi inawezekana sana tu kumpenda mtu pasi kumwona.
Kwa mfano mi ni mpenzi wa riwaya za A.E MUSIBA ambapo mhusika mkuu anyetumiwa na mwandishi huyo ni Willy Gamba,kutokanana masimulizi yake kumhusu willy nilipokuwa nasoma hadithi zake tayari nilikuwa namjua WIlly wangu yukoje kichwani mwangu niliijua sauti yake na tabia yake ambayo nilikuwa nimeiunda kichwani mwangu na hilo lilinifanya nikawa mpenzi mkubwa sana wa mtu dhahania wa kwenye riwaya WILLY GAMBA,nilimpenda sana kiasi kwamba hata nilipokuwa nawasimulia wenzangu niliwasimulia kwa msisimko kama vile nilishawahi kumwoan huyo mtu.Na mpaka leo hii ninaye Willy wangu kichwani na sikuzote nitaendela kumpenda na ndio maana hadithi za A.E MUSIBA hazinichoshi.
Mtu pia aweza kukupenda kwa kuona avatar yako ndiyo,na hii ni bada ya hatua ya kwanza ya kuvutiwa na avatar yako na kisha kwa kutumia hiyohiyo avatar yako mtu akajenga picha kicwani kuwa kutokana na hii avatr huenda huyu mtu atakuwa wa namna hii na atakuwa ana tabia fulani na hivyo kujikuta anajenga hisia za upendo kukuelekea.
Kwa hiyo kwa ufupi kwa upande wangu mimi inawezekana sana tu kumpenda mtu pasi kumwona.
Kwa mfano mi ni mpenzi wa riwaya za A.E MUSIBA ambapo mhusika mkuu anyetumiwa na mwandishi huyo ni Willy Gamba,kutokanana masimulizi yake kumhusu willy nilipokuwa nasoma hadithi zake tayari nilikuwa namjua WIlly wangu yukoje kichwani mwangu niliijua sauti yake na tabia yake ambayo nilikuwa nimeiunda kichwani mwangu na hilo lilinifanya nikawa mpenzi mkubwa sana wa mtu dhahania wa kwenye riwaya WILLY GAMBA,nilimpenda sana kiasi kwamba hata nilipokuwa nawasimulia wenzangu niliwasimulia kwa msisimko kama vile nilishawahi kumwoan huyo mtu.Na mpaka leo hii ninaye Willy wangu kichwani na sikuzote nitaendela kumpenda na ndio maana hadithi za A.E MUSIBA hazinichoshi.
Mtu pia aweza kukupenda kwa kuona avatar yako ndiyo,na hii ni bada ya hatua ya kwanza ya kuvutiwa na avatar yako na kisha kwa kutumia hiyohiyo avatar yako mtu akajenga picha kicwani kuwa kutokana na hii avatr huenda huyu mtu atakuwa wa namna hii na atakuwa ana tabia fulani na hivyo kujikuta anajenga hisia za upendo kukuelekea.
Last edited by a moderator: