Unapenda watoto?

Wanavutia sana lakini nikiwaza namna maisha yalivyo na mateso naogopa sana kuleta watoto duniani waje kuzunguka duara la michosho tulilozunguka sisi
Yaan kama unahisi kabisa hutakua nafasi ya kuwahudumia au kuwajali acha tu usiwalete

Lakin watoto mbali na kua wanaleta furaha na utulivu

Kuleta watoto duniani ni kama project dunia ili iwepo ni lazima watu wengine waje maana tuliopo lazima tutaondoka
 
Cchildren are lovely to be around, napenda sana watoto. They're pure and innocent. Mdogo wangu wa kike, anaweza kuniamrisha nifanye jambo la kijinga na nikafanya. Because I find myself taken by her beautyy
 
Hata kama wewe ni bilionea, bado haiondoi uhalisia kwamba ukipata watoto hawatoteseka... Anaweza kutekwa akateswa vibaya sana kisha akauawa au akaachiwa kilema.
Kuna ajali, magonjwa na sonona zisizo na sababu huku dunia nayo ikiwa ni mwamba unaoelea hewani pasipo na usalama wa uhakika.... Hivyo ukishagundua hili bora ule zako bata ukija kudanja usiache uzao nyuma/ufe na mbegu zako😄
 
Wanasema kuwa ukiwa na mtoto wa miaka 2 - 5 hivi, halafu akapotea kwenye uwepo wako na huko aliko akiwa kimya, ujue anafanya uchunguzi wenye uharibifu😀. Labda amepasua simu, anaharibu kitasa nk
Dah watoto bhana 😁😁
Na badai akikutwa anaweka kasura ka innocent 😅
 
Safi kabisa mwanakwetu ila umewaza nini leo rafiki yangu ?
 
Kwanini una mawazo negative kiasi hicho?
Wazazi wako wangewaza hivyo hizo raha wewe ungezipondea wapi?

Wewe sema hivi sivutiwi tu na mambo ya kuzaa ila hizo sababu ulizotoa ni nyepesi sana

Wewe mwenyewe unaweza kua na mali zako wahuni wakakudaka wakakuminya na wakachukua kila kitu
 
Infropreneur njoo umsikie huyu dada anachokisema
 
Ukweli mtupu! Kuna muda nawaza ingekua inawezekana kumsindikiza mtoto kila anapoenda ili kumlinda na walimwengu ila ndo hivyo haiwezekani.
Na jinsi anavyozidinkuwa mkubwa ndo wasiwasi unazidi maana huwezi tena kumlinda. Unakuwa unawaza masaa yote sijui anafanya nini huko, je yupo salama yaani shida tupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…