sabuwanka
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 690
- 751
Wapendwa wangu wana jukawaa salaam.
Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la mahusiano ya kimapenzi na ndoa kuvunjika hasa kwetu vijana, kugombana, kutofautiana, kupishana maneno ni jambo la kawaida kwasababu tunaingia katika mahusiano tukiwa na tabia tofauti tofauti na tena tumelelewa na kukulia katika mazingira tofauti.
Napenda nishauri kuwa inapotekea migogoro KUWA TAYARI KUJISHUSHA! Unyenyekevu wa mume kwa mwanamke unaokoa mahusiano, na unyenyekevu wa mke kwa mume huyeyusha hasira , kwa ustawi wa ndoa na mahusiano tuwe tayari kunyenyekeana, kuomba radhi , na kuzizungumzia tofauti zetu kwa upendo.
Ngumi, vibao, fimbo, havijengi wala kuimarisha mahusiano isipokuwa zinafanya kila asiyeridhika kuwa mguu upande!
Mwisho kanuni hiyo inatumika katika migogoro mingi isipokuwa ile ya uchepukaji hasa mwanamke kuchepuka
Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni
Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la mahusiano ya kimapenzi na ndoa kuvunjika hasa kwetu vijana, kugombana, kutofautiana, kupishana maneno ni jambo la kawaida kwasababu tunaingia katika mahusiano tukiwa na tabia tofauti tofauti na tena tumelelewa na kukulia katika mazingira tofauti.
Napenda nishauri kuwa inapotekea migogoro KUWA TAYARI KUJISHUSHA! Unyenyekevu wa mume kwa mwanamke unaokoa mahusiano, na unyenyekevu wa mke kwa mume huyeyusha hasira , kwa ustawi wa ndoa na mahusiano tuwe tayari kunyenyekeana, kuomba radhi , na kuzizungumzia tofauti zetu kwa upendo.
Ngumi, vibao, fimbo, havijengi wala kuimarisha mahusiano isipokuwa zinafanya kila asiyeridhika kuwa mguu upande!
Mwisho kanuni hiyo inatumika katika migogoro mingi isipokuwa ile ya uchepukaji hasa mwanamke kuchepuka
Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni