BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Unamkumbuka huyu mtoto? Mwaka 2015 aliokotwa Abuja Nigeria akiwa na utapiamlo mkali. Wazazi wake walimtupa wakihisi wamezaa jini.
Raia mmoja wa Norway Anja Ringgren Lovén alimuokota, akamuogesha na kumpeleka hospitali. Akapata matibabu kisha akarudi kuishi nae. Akamlisha vyakula vyenye virutubisho ili kuondokana na utapiamlo mkali aliokua nao.
Mwaka 2017 katika ukurasa wake wa Facebok Anja aliandika maneno haya (nimefanya tafsiri isiyo rasmi);
"Siku ile nilipomuona huyu Malalika aliyetelekezwa niliumia sana. Nilipombeba ktk viganja vyangu nilijua kabisa HATAPONA. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilipoteza matumaini ya uhai kwa mtu niliyeamua kumsaidia.
Alisimama kwa shida, alipumua kwa shida, alikula kwa shida. Hata alipolia sauti ilitoka kwa shida. Kila kitu kwake kilikua shida. Kwahiyo nilijua atakufa. Lakini sikutaka afe kama mnyama. Sikutaka afe bila utu. Sikutaka afe bila jina.
Nikaamua kumpa jina. Nikamuita HOPE. Neno Hope kwangu ni la pekee. Miaka mingi iliyopita nilichora "tatoo" yenye neno HOPE mikononi. Sijaifuta hadi leo. HOPE kwangu inamaanisha.
H- Help
O- One
P- Person
E- Everyday
Kwa muujiza wa Mungu Hope alipona. Picha ya kwanza kushoto ni wakati ameokotwa. Inayofuata ni 2017 akiwa ameanza shule. Picha ya 3 kushoto ni mwaka 2018, Anja alipost kuonesha maendeleo ya Hope tangu alipookotwa hadi wakati huo. Na picha ya mwisho kulia ni December 2020 Hope akiwa nyumbani kwa Anja anapolelewa.
Kuna mengi ya kujifunza kwenye kisa hiki. Unajisikiaje ukitupia chakula mbwa wakati watoto wa jirani yako wanashindia uji wa chumvi? Unajisikiaje kila weekend unafuja hela kwenye kumbi za starehe wakati kuna ndugu yako anakufa kwa kukosa elfu 10 ya matibabu?
Mungu anapokubariki sio kwamba wewe ni bora kuliko wengine. Anakubariki ili ubariki wengine. Tunapotafakari kisa cha Anja na Hope tuendelee kukamilisha ujenzi wa nyumba ya Penina. Wewe unayesoma ujumbe huu ndiye Anja wa kuikoa familia ya Penina itoke kwenye zizi wanaloishi kama wanyama, na wawe na makazi bora.
Raia mmoja wa Norway Anja Ringgren Lovén alimuokota, akamuogesha na kumpeleka hospitali. Akapata matibabu kisha akarudi kuishi nae. Akamlisha vyakula vyenye virutubisho ili kuondokana na utapiamlo mkali aliokua nao.
Mwaka 2017 katika ukurasa wake wa Facebok Anja aliandika maneno haya (nimefanya tafsiri isiyo rasmi);
"Siku ile nilipomuona huyu Malalika aliyetelekezwa niliumia sana. Nilipombeba ktk viganja vyangu nilijua kabisa HATAPONA. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilipoteza matumaini ya uhai kwa mtu niliyeamua kumsaidia.
Alisimama kwa shida, alipumua kwa shida, alikula kwa shida. Hata alipolia sauti ilitoka kwa shida. Kila kitu kwake kilikua shida. Kwahiyo nilijua atakufa. Lakini sikutaka afe kama mnyama. Sikutaka afe bila utu. Sikutaka afe bila jina.
Nikaamua kumpa jina. Nikamuita HOPE. Neno Hope kwangu ni la pekee. Miaka mingi iliyopita nilichora "tatoo" yenye neno HOPE mikononi. Sijaifuta hadi leo. HOPE kwangu inamaanisha.
H- Help
O- One
P- Person
E- Everyday
Kwa muujiza wa Mungu Hope alipona. Picha ya kwanza kushoto ni wakati ameokotwa. Inayofuata ni 2017 akiwa ameanza shule. Picha ya 3 kushoto ni mwaka 2018, Anja alipost kuonesha maendeleo ya Hope tangu alipookotwa hadi wakati huo. Na picha ya mwisho kulia ni December 2020 Hope akiwa nyumbani kwa Anja anapolelewa.
Kuna mengi ya kujifunza kwenye kisa hiki. Unajisikiaje ukitupia chakula mbwa wakati watoto wa jirani yako wanashindia uji wa chumvi? Unajisikiaje kila weekend unafuja hela kwenye kumbi za starehe wakati kuna ndugu yako anakufa kwa kukosa elfu 10 ya matibabu?
Mungu anapokubariki sio kwamba wewe ni bora kuliko wengine. Anakubariki ili ubariki wengine. Tunapotafakari kisa cha Anja na Hope tuendelee kukamilisha ujenzi wa nyumba ya Penina. Wewe unayesoma ujumbe huu ndiye Anja wa kuikoa familia ya Penina itoke kwenye zizi wanaloishi kama wanyama, na wawe na makazi bora.