Kilianza kwanza kwa wale wanaotumia TTCL, wakaja wazee moderm watu waotumia dish wakamalizia kama wiki mara chali, ule mtandao ungekuwepo mpaka sasa sijui ingekuaje maana watu walikuwa wanapiga desa alafu wanapiga kimya maana baada ya kufungwa unakuta watu wanazungumzia matukio yote (lakini siku hizi na MB za bure na internet unapata hata kama una simu ya 30,000 mpaka watoto wanaangalia mambo). Baada ya mkulu kutolewa vile watu wakaanza kusikitika sasa kwa kile kilichofanywa na mtandao ule wakati kuna watu kibao walitolewa hakuna aliekuwa anapaza sauti na ndipo nilipokuja kufahamu kumbe kitu kikihusisha mamlaka ya juu maamuzi ya haraka hufanyika yaani kulikuwa na uwezekano wa kuufunga siku nyingi.