Unakumbuka kufanya kituko gani during foolish age?

Unakumbuka kufanya kituko gani during foolish age?

Yes!Yes!....
****natumai mumejibu yap! yap! hifyo ndifyo tunatharimianaga tukiwa kambi huko kwetu njenoro shaina*****.

Sasa, kuna hii kijana kimoja kirikuwa kinaitwo mamishe. kirikuwa kunajifanya kwetu sana ati gwasababu warikuwa na hurubaro (wheelbarrow) mupya na sisi hatukuwa nayo. Kira siku tukieda marisoni nakyo kinakuja na hiyo hurubaro na kinakataa kutupatia tubebana nayo ati mbaka tukiripe siringi. Kira musisana hata Wangari Sendeo arikua tu anataka kuongea na Mamishe gwasabau ya hiyo hurubaro. Hai, tukaona hapa rasima tukuwe wajaja.

Hiyo jioni ya jumamwothi, kurikuwa na ngwataniro(village church meeting) ya kijiji kia gachuiro kwetu. sasa wasee na wamama wooote wa kanitha warikuwa wamejaa kwetu.Huku Njesu agitawara kwetu, nasisi tukiwa marisoni, ndaimono arikuwa anatufatia ma~ideas sa vile mamishe angeisha ndio tuedese hurubaro yake.

Saa tisa hifi nikaeda nikandanganya Mamishe..'Mamise...kwa ire shoo ya ure kuria wa nduka, kumeanguka njirongo (siringi mia tano) na watu wemisidwa kuingia. majamaa sanguni sijawai kuona mutu amefurahi nyamna hiyo.Akaasanisa hurubaro na gutoka mbio kama musale.

Baada ya ndikika sinatosana hifi, ndio huyo mamise agatokesea na kijiko ire kubwa (spade) na huma na kaba (rope) na kuerekea kwenye shoo hiyo ya kuria. Nasisi mara hiyo hiyo tugasukua hurubaro na kuaja kuendesa. Washa mamishe aaje kushimba simo kado ya shoo..washa ashibe..mara moja agafungiria kaba kwa gitingi na akajifunga njohero (waist) na kuaja kusuka. huku agisuka, na sisi na Sendeo turikuwa tunatoa tu jaso ni kubebana na kendesa hurubaro.

Kufucia nyamna hii tukasikia nduru ..uuuiiii..uuuiii..jini majini...shoo yangu inaongea..uuuuiiii mwathani! na watu wamesingira hiyo kioro ya kuria. Tugakibia. Kube ni bibi ya kuria arikuja gukojoa nayeye mamise akiwa sini akamuabia..tafadhali nakuona usinikojolee!...watu wakamutoa na kumuhoji kidogo. Arikuwa na mififi kwa miguu yake hadi kwa magoti..Agasema ati ni musatha ariniambiang'e nye' ny'e nyukwa! Nkt..watu wakanirukia nikaferekwa nyubani wengine wakinipiga na safai kwa miguu (stinging nettle).

Kufika nyubani tukafata watu wakiiba wibo ya muiso waombe. mama akanirukia agasikwo ni wasee akaambiwo ati ni saitani ananisubua na inataka maobi. ngaambiwa nifuje magoti hapo mbere yao na niaje kujiobea. Hata ware watu warinireta wakaambiwo wainue mikono kama wameniangarisia..ikaaja hifi:

MUOBI: Njehova tumekuja mbere yako.

WENGINE + MUSATHA:ii niguo baba.(ndio baba)

MUOBI: tukireta kijana hii musatha tukioba umubadilise

WENGINE + MUSATHA:ii niguo baba.(ndio baba)

MUOBI:amekuwa mukora sana na niyeye anafuza watoto wetu tabia baya baba

********hapo ngaona iko sida..ngaona jibu yangu baka i change*****

WENGINE : Niguo baba ( Ndio baba)

MUSATHA (na nguvu) : ni maheni baba (ni uwongo baba)


************WATU WOOOOOTE WAGASEKA*******

Asandi ni musuri kujitetea
 
yaani mwandishi unapozungumzia kumaliza paper ya mock ndiyo kipindi ulipotoka kutoka foolish age??????????
Any way.....
Mi nnachokumbuka ni pale nikiwa na miaka kama 9 hivi wakati dada yangu alipokuwa anacheza rede na wenzake nilimfunua sketi ya rafiki yake ambaye kiukweli alinizidi sana kiumri basi dada yangu alinitandika ngumi ya jicho kama mtoto wa kiume vile basi ilitengenezeka kesi kubwa ambayo iliunguruma na wala siwezi kusahau kisa hiki........
 
Nashangaa........Fulishi age bila MASTABESHENI NA MATESTI TYUBU.......... HAIPO. Kila mtu ohooo... nilimfuata demu hadi kibaha..........., mara fundi maji..........sorry fundi bomba.......... mara ohooo nimecheka sana........... tajeni mastabesheni mlizofanya enzi zenu za fulishi age............ mi nilipiga kadhaa............
 
Nashangaa........Fulishi age bila MASTABESHENI NA MATESTI TYUBU.......... HAIPO. Kila mtu ohooo... nilimfuata demu hadi kibaha..........., mara fundi maji..........sorry fundi bomba.......... mara ohooo nimecheka sana........... tajeni mastabesheni mlizofanya enzi zenu za fulishi age............ mi nilipiga kadhaa............

HaaaaaHaaaaaHaaaaa!!! Usinikumbushe upuuzi mwingine ambao baada ya kuufanya nilijikuta nimejifungia choo cha shule siku mzima hadi nikakumbuka stori za mijamaa iliyokuwa imenizidi umri kuhusu hako kamchezo! Kumbe unatarajia nini baada ya kuwa full nimeboreka humo toilet?! Ilikuwa ni nusura nipige kelele baada ya mautamu niliyopata baada ya kujaribu hako kamchezo!!! Nusura chimbo langu ligundulike!
 
mimi nikiwa form one jamaa akawa ananiuzii daily halafu ndo alikuwa mtu mzimaa class..nikammind adhabu yake iwe nn..basi siku moja jioni class wengine wanafanya usafi nikavizia class madaftari yake yote nikayachanaaa..nikaamini hamna aliyeniona.

basi baadae jamaa kumaliza usafi anacheki madaftari yake yote yamechanwaa...duh wacha ammind akaripoti kwa mwalimu wa zamu jamaa alikuwa mkali kinoma huyo ticha. akatuitaa wote darasani akasema nitajieni aliyefanya kitendo hichoo..duuh nimeuchunaa tuu nasikiliziaa..basi akasema kwa siri mnaruhusiwaa kumtaja kwangi nami nitamshughulikiaaa ipasavyooo..duh kumbe kuna demu aliniona akaripoti kwa tichaa jina languuu..

nikaitwaa kuhojiwa kama polisi vile nikakataaa katakataa..baadae nikapewaa bonge ya adhabuu..nikakairii kosa na kula fimboo kibaooo na adhabu ya kuandika upyaa notes za jamaaa..ilikuwaaa sio mchezoo notes za masomoo kumii.....

kuanziaa hapoo nilikomaaa kufanyaa mambo ya kifoolish na jamaa akawa mshkajiii..duh mungu amrehemu nasikia majuzi kajinyongaa kitaaa...
 
duu nakumbuka niko 4m one nimeenda likizo kwa Aunt mambo ya puli si niko bafuni nakamua kitu bafu lenyewe la uswazi mlango bati kumbe ninavyochochea huku nyuma sauti inatoka coz nimeegemea mlango wa bati shangazi akapiga kelele wee huko ndani vipi nikamwitikia kwa sauti ya kinyonge kwa kujitetea eti naua mjusi
 
duu nakumbuka niko 4m one nimeenda likizo kwa Aunt mambo ya puli si niko bafuni nakamua kitu bafu lenyewe la uswazi mlango bati kumbe ninavyochochea huku nyuma sauti inatoka coz nimeegemea mlango wa bati shangazi akapiga kelele wee huko ndani vipi nikamwitikia kwa sauti ya kinyonge kwa kujitetea eti naua mjusi
Kama nakuona vile ulivyokuwa unaua mjusi...........Loh!!
 
yaani mwandishi unapozungumzia kumaliza paper ya mock ndiyo kipindi ulipotoka kutoka foolish age??????????
Any way.....
Mi nnachokumbuka ni pale nikiwa na miaka kama 9 hivi wakati dada yangu alipokuwa anacheza rede na wenzake nilimfunua sketi ya rafiki yake ambaye kiukweli alinizidi sana kiumri basi dada yangu alinitandika ngumi ya jicho kama mtoto wa kiume vile basi ilitengenezeka kesi kubwa ambayo iliunguruma na wala siwezi kusahau kisa hiki........

tatizo ulikuwa unatumia msuri(maguvu); wenzako tulikuwa tunaweka kioo kwa chini!
 
Kwa waliosoma Moringe Sokoine,Monduli. kuna Mmasai mmoja aliletwa bwenini kwe2 sasa akawa ananuka sana ikabidi bodi ya utundu ikae... Siku moja akiwa amelala jamaa mmoja sasa Marehemu akamfunga kofuli kwenye sikio na kwenye kitanda cha chuma... Kisha akampigia kelele Motoooo! Loh! Jamaa akaamka sikio limekatika... Duuh tulichapwa sana na Mwalimu Kwayu ... nikikumbuka napatwa na uchungu...
 
Kuna siku moja nilikuwa na hamu sana na nyama ya kuku. Unajua tena enzi hizo kuku kula ilikuwa nadra sana...kama si krisimasi basi noeli au idi au maulidi.

Basi bana mimi na machizi wangu takasuka bonge la raketi. Ilikuwa wakati wa likizo ile ya mwezi wa sita. Mida ya kaa saa nne hivi asubuhi tukaenda maeneo ya nyumba ya jirani. Huyu jirani yetu alikuwa anafuga kuku wa kienyeji. Sasa si unajua kuku wa kienyeji zao kuranda randa mtaani wakitafuta chao na wao.

Tukapanga wenyewe siku hiyo lazima tuibe kuku wa jirani halafu tukampike. Tukaanza kuwakimbiza bana...si unajua tena kuku wa kienyeji huwezi kuwakamata hivi hivi tu bila mbinde ya kukimbizana....basi bana kimbiza kimbiza...kwenye migomba...kwenye michongoma....hatimaye tukamkamata mmoja.

Hahahahaaa tukarudi zetu home...tukachemsha maji ya kumnyonyolea....tukampiga bisu.....tukambanika kwenye oven halafu machizi tukapiga menu. Daaah tulifaidi sana siku hiyo aisee...halafu uzuri wake hakuna mtu aliyestukia.
 
Mkuu The Boss!!

Unakipaji!! Si unajua haikupi taabu yeyote kufanya watu kuwa exited na kucheka kabisa kabisa!!!?

Kipaji chako umekitumia vipi so far kutegenezea Kipato?

Yes do smthing with it !!!
 
kuku wa kienyeji humkimbizi bali unategeshea
kamba nyembamba imara ambayo nchani
imepenyezwa punje ya mahindi kisha unangojea.
akikatiza tu na kuimeza hiyo punje wewe unavuta kamba
hapo kuku hata kelele hapigi unamnasa kiulaini lol
 
duu nakumbuka niko 4m one nimeenda likizo kwa Aunt mambo ya puli si niko bafuni nakamua kitu bafu lenyewe la uswazi mlango bati kumbe ninavyochochea huku nyuma sauti inatoka coz nimeegemea mlango wa bati shangazi akapiga kelele wee huko ndani vipi nikamwitikia kwa sauti ya kinyonge kwa kujitetea eti naua mjusi
Duuuuuuh sina mbavu nimechekaa mpaka machozi maana mjusi mwenyewe alitoka nduki...tehtehteeh.
 
Nakumbuka siku moja nilikuwa na rafiki yangu ambaye naye alikuwa mtundu sana enzi hizo, basi alinishawishi kwenda kuvua samaki kwa mzee mmoja ambaye alikuwa anamiliki bwawa la samaki karibu na nyumbani kwake.

Nikakubaliana naye, tukaanda zana za kuvua samaki, uzi mrefu wa kwenye madirisha(nyavu), sindano ambayo ilikuwa ni pini, fimbo ndefu nyembamba tukaifunga ule uzi kwenye fimbo na pini tukaifungia mwishoni mwa ule uzi,na tukatafuta wadudu wafananao na minyoo huwa mara nyingi wanapatikana sehemu za chini ya matofali yaliooza au kwenye udongo na tukawachomeka kwenye pini hao bwawani.

Sasa pale Bwawani,tuiliingia kwa siri ili tusigundulike kirahisi,tukaangalia mazingira kama yanaruhusu kuvua samaki huku na huko tukaona mazingira poa tukarusha ndoano bwawani na kusikilizia kama samaki watanaswa kwenye pini.

Sasa huyo rafiki alitikisa nyasi zilizoko pale bwawani kwa kutumia miguu yake, ghafla tukashtushwa na mimawe makubwa yanarushwa mfululizo kwa upande wetu kumbe mzee alikuwepo nje ya nyumba yake aliona nyasi kama zinatikisika vile akarusha mawe makubwa meengi tu alidhani nyoka, baadaye tukaona kama mawe hayarushwi tukaendelea kutafuta samaki pale,kumbe yule mzee alitusogelea akidhani nyoka labda amekufa kumbe ni sie,nakumbuka maneno haya aliyatamka "Kumbe ni ninyi watoto!!"

Dah ilikuwa noma kweli aibu lkn alituachia samaki wawili kila mmoja wetu.
 
Kuna siku moja nilikuwa na hamu sana na nyama ya kuku. Unajua tena enzi hizo kuku kula ilikuwa nadra sana...kama si krisimasi basi noeli au idi au maulidi.

Basi bana mimi na machizi wangu takasuka bonge la raketi. Ilikuwa wakati wa likizo ile ya mwezi wa sita. Mida ya kaa saa nne hivi asubuhi tukaenda maeneo ya nyumba ya jirani. Huyu jirani yetu alikuwa anafuga kuku wa kienyeji. Sasa si unajua kuku wa kienyeji zao kuranda randa mtaani wakitafuta chao na wao.

Tukapanga wenyewe siku hiyo lazima tuibe kuku wa jirani halafu tukampike. Tukaanza kuwakimbiza bana...si unajua tena kuku wa kienyeji huwezi kuwakamata hivi hivi tu bila mbinde ya kukimbizana....basi bana kimbiza kimbiza...kwenye migomba...kwenye

michongoma....hatimaye tukamkamata mmoja.

Hahahahaaa tukarudi zetu home...tukachemsha maji ya kumnyonyolea....tukampiga bisu.....tukambanika kwenye oven halafu machizi tukapiga menu. Daaah tulifaidi sana siku hiyo aisee...halafu uzuri wake hakuna mtu aliyestukia.


heheheheh unikumbusha story ya kuku bwana, basi bwana nyumbani tulikuwa tunafuga kuku wa kienyeji,mama alikuwa mkali sana na kuku wake hataki kabisa waliwe ovyo ovyo yeye alikuwa anatoa kuku siku ya xmas na pasaka tu, basi siku hiyo mimi na mdogo wangu tukakubaliana lazima leo tule kuku, kama kawa mama akaenda zake job si tukaingia bandani tukachagua kuku aliyenona yaani jogoo, tukamjicha vizuri,nyonyoa manyoa mwisho tukamkaangaa, kweli nyama ilikuwa tamu sana na mama tumbakizia

alivyotoka tu kazini tukamdaka kabla hajaingia ndani, mama leo kuku amegongwa na baiskel kabla hajafa tukamchinja, mama alisikitika huyo kaulizia kuku yupi tukataja jogoo lile alilolipenda, alisikitika sana kama angejua tumemchinja kwa kusudi tungepigwa marufuku kula usiku week nzima

duu utoto bana
 
Very funny hii thread kwa kweli nimecheka mpaka nimelia jamani. Mna vituko mno.
 
Hahaha umenikumbusha mbali sana, nakumbuka nilikuwa darasa la sita shule moja inaitwa Gedeli kule Nyakato , Mwanza. Darasa nililiklokuwa nasoma kulikuwa na minjemba mikubwa na mimi nilikuwa na kiumbo kidogo, yaani nilikuwa dogo flani hivi. Sasa kulikuwa na mwalimu mmoja sikumbuki jina lakini alikuwa wa somo la kiswahili, alikuwa na kawaida kila aingiapo darasani, wanafunzi wote husimama na kumuamkua, na baada ya hapo hakuna kukaa hadi ujibu swali. Sasa kwenye dawati nililokuwa nakaa mimi nilikuwa nakaa na njemba moja wapo, kutoka pande za Kagera jamaa alikuwa amekariri darasa, sasa sijui niliwaza nini au ndio utoto huo, mimi nilikuwa wa kwanza katika dawati letu kujibu swali na hivyo nilikaa, sasa ile njemba alipojibu swali na ilipokuwa inajiandaa kukaa, mimi nilichukua peni yangu na kutegesha kule kwenye ncha kali chini ya makalio ya jamaa, sa jamaa si ndio akae! aaaaaa yaani ile peni ilizama kati kati ya makalio mawili yaani****! Jamaa alipiga kelele huyo na mimi nikaitoa ile peni haraka, lakini jamaa alinipa kichapo si mchezo na kisha nikaenda tena kuchezea bakora za walimu kama watatu hivi ofisini " staff room" . Yaani hii incident kila nikiikumbuka huwa nashindwa elewa niliwaza nini hadi kufanya vile!
 
Ilikuwa ni baada ya kumaliza paper ya mock (Form Four Mock Examination)miaka kadhaa iliyopita! Baada tu ya kumaliza paper, nikajiona kama mkataba wangu na mambo ya skonga ndo ushaisha! Wiki iliyofuata, nikapiga full ndela-sikuibuka school hata siku moja! Washikaji wakaniletea ujumbe kwamba Brother Masabo (Alikuwa ndie Headmaster-S.t. Anthony’s Sec. School) ananitafuta ile mbaya! Kwamba kila siku alikuwa anaibuka class kuulizia kama nimekuja shule! Taarifa hii nililetewa wakati nakusudia kuibuka skul wiki inayofuata! Hata hivyo, baada ya kuambiwa Bro. Masabo ananisaka, nikaanza kuogopa na kuachana na mpango wa kutaka kwenda skul wiki iliyofuata! Wakati nafikiria hivyo, nikajiuliza nitamweleza nini Bro. Masabo! Baada ya kutafakari sana, nikakumbuka mstari mmoja wa Bob Marley kwenye track iitwayo WAR! Kipande cha mstari huo kinasema “TOTAL DESTRUCTION, THE ONLY SOLUTION!” Nami nikaona suluhisho la kisanga nilichozusha ni kufanya total destruction!!!

Wiki iliyofuata, nikamwomba mshikaji mmoja aitwae Sweetbert aende mwa Mwalimu wa Darasa akatoe ripoti kwamba naumwa! Aliponiuliza endapo teacher angeamini; nikamjibu acha asiamini kv siku ya siku nitaenda kumthibitishia Bosi wake kwamba nilikuwa naumwa! Nikaendelea kumweleza kwamba “Sitamthibitishia kwa vyeti, bali kwa vitendo!”

Kama tulivyokubaliana, wiki iliyofuata mchizi akapanda gari hadi St. Anthony’s na kupeleka taarifa kwamba nipo hoi! Inavyoelekea, Ticha wa darasa hakuamini, lakini sikujali kv nilishapanga kwamba Bosi wake(Bro. Massabo) ataamini tu kwamba nilikuwa taabani.

Nikaongeza wiki zingine tatu(3) za utoro, nikatimiza mwezi mzima bila kwenda shule!Utoto bana! Siku niliyoamua kuibuka skul ni siku ambayo ilikuwa inaanza Pre-National Exams! Mchizi nikachukua masizi meupe nikadondoshea mafuta ya kula kidogo kisha nikajipaka kwenye lips! Mzee kujicheki kwenye kioo, lips zilikuwa nyeupeeee, kama mgonjwa ngoma au typhoid! Nikaona YES, success in first step! Nikaibuka skonga, huku nikiwa mnyonge maradufu!!!! Sikuongea na m2, kwa kuogopa yasije masizi yangu yakafutika!!! Nikaingia Class, na mara paper ya CIVICS ikagawanywa tayari kwa kuanza Pre-National Exams! Nikafanya swali la kwanza hadi la tano, mara nikaanza kutetemeka(KUJITETEMESHA)! Kuanzia swali la sita hadi la tisa, nikabadilisha mwandiko na kuwa kama ni wa mtoto wa darasa la kwanza!Hata hivyo, nilipofika swali la tisa, nikaongeza kasi ya kutetemeka hadi Msimamizi aliponiona! Jamaa ile kuniona tu, akaanza kutaharuki! Manake nilikuwa nimebadilika vibaya mno, mithili ya mtu aliyepandisha mashetani! Jamaa akaagiza nitolewe darasani hadi dispensary ya hapo skul! Pale dispensary waliponiona tu, wakaona ile issue ni mzito kwao! Kwani licha ya kutetemeka kupita kiasi, nilikuwa napiga makelele isivyo kawaida! SIO SIRI, ILITISHA! Sijui niliutoa wapi ule ujasiri!

Pamoja na yote hayo, bado akili yangu ilikuwa kwa Brother Massabo! Ni yeye peke yake ndie niliyetaka kumthibitishia kwamba nilikuwa naumwa taabani! Na kwakuwa issue yangu ilionekana ni mzito sana; ilibidi akaitwe Headmaster Brother Massabo!! Dakika mbili baadae, Bro Massabo akaja huku akionesha dalili zote za kutaharuki!

“NasDaz, nini! Umekumbwa na nini!” Nakumbuka Brother Massabo aliniuliza mara alipofika eneo la tukio! Akili yangu ikasema “nilikuwa nakusibiri wewe hapo Brother Massabo!” Badala ya kujibu, mzee nikaongeza kasi ya kujitetemesha na kupiga kelele hadi mwenyewe nikaanza kujiogopa! Kuona vile, Brother Massabo akaamuru atafutwe mtu anayekufahamu home! Sijui ni kwanini jamaa hakutoa wazo la kupelekwa hospital; inawezekana aliona haukuwa ugonjwa wa kawaida! Tena wana bahati, wakati ule nilikuwa sifahamu lolote kuhusu kupandisha mashetani; manake wangenikoma!

Baada ya Bro. Massabo kuamrisha atafutwe mtu anayekufahamu home, ikabidi nishushe mashetani kidogo ili nipate nafasi ya kumtaja mtu anayekufahamu home! “Habibu....!Habibuu...!Habibu Mabehewa!” Nakumbuka kumtaja mshikaji mmoja ambae wakati huo alikuwa ama Form I au Form II! Habibu akaenda kuitwa, na alipofika na kunikuta na hali niliyokuwa nayo; nae nikaona anaanza kulengwalengwa na machozi!Angekuwa demu, naamini angelia tu!NILITISHA BWANA!!

Ili nisiwafie mikononi, Brother Massabo akatoa gari yake binafsi ili nipelekwe home tukiambatana na Habibu, Dereva na Mwalimu Mtiro! Safari ikaanza, na tulipoenda mbali kidogo Mwalimu Mtiro akataka kuleta ukuda wake wa kiualimu!! Eti badala ya kupelekwa home, nipelekwe hospital!! Jamaa sijui alinishitukia kwamba nafanya sanaa, au ndo alikuwa ananihurumia nisije nikafia home! Kuona hivyo, nikashusha mashetani kidogo ili nipate nafasi ya kutetea uamuzi wa kurudishwa home badala ya kupelekwa hospital!

Nikashinda, hivyo safari ikaendelea! Mbele kidogo, Mwalimu Mtiro akajibu nakaa wapi! Nikawahi kujibu kwamba nakaa Kurasini Kota za Bandari! Nikahisi habibu ni kama alishangaa ni kwanini nimesema nakaa huko! Hakufahamu na ndio maana niliwahi kujibu kv nilijua angejibu yeye angetaja mitaaa ya JKT! Huko kote ni kwetu, but JKT walikuwa wanaishi wazazi wangu ambao wangeshangaa sana kusikia eti naumwa karibu mwezi mmoja sasa(Kuna mida nilishusha mashetani na kuwapiga fix kwamba nilianza kuumwa soon after Mock Exams)! Na huko Bandari ndiko nilikokuwa naishi na uncle wangu lakini wakati huo nilikuwa alone kv uncle alikuwa safarini! Naamini Habibu angetaja JKT kv alijuwa pale bandari nilikuwa naishi peke yangu!

Safari ikaendelea! Mbele kidogo Mr. Mtiro akauliza naishi na nani! Nikamjibu nipo peke yangu. Akauliza endapo nina ndugu ili akafuatwe aje kukaa na mimi kwa wakati huo! Nikajibu ndio, ninao!

Safari ikaendelea, huku nikipiga mahesabu nitamweleza vipi Habibu kuhusu ni ndugu gani anayetakiwa kutaarifiwa juu ya ugonjwa wangu! Nilijua, taarifa hizo zikipelekwa home lazima wangeshangaa kv ni jana yake tu nilikuwa nimetoka kuuchapa wali maharage kwenye meza yao!

Kama zali, Mr. Mtiro akajisahau kwa sekunde chache! Bila kupoteza muda, nikamnong’oneza Habibu “wapeleke kwa Sweetbert!” Mchizi akanielewa, ingawaje ni kama alizidi kukumbwa na mshangao kuhusu ugonjwa wangu! Huyu Sweet, ni mchizi wangu na ni Bro. wa huyu Habibu!!

Nikafikishwa gheto, kisha Habibu akaondoka tena na akina Mr. Mtiro ili afuatwe ndugu yangu! Kama nilivyokuwa nimemtonya, Habibu akawapeleka kwa Sweet ambae nae akaletwa kwa mgonjwa!

Ninachokumbuka ni kwamba, hata Sweet alipokuja home aliiingia chumbani huku akiwa ametaharuki! Sielewi aliambiwa nini kuhusu ugonjwa wangu!
“NasDaz, vipi kwani?” Sweetbert aliniuliza huku akiwa ametaaharuki mara baada ya kuingia chumbani kwangu!
“Vipi, wameshaondoka?” Badala ya kumijibu nilikumbwa na maswahibu gani mimi nilimtupia swali katika namna ya kunong’ona! Hata hivyo, badala ya kujibu nae akaangua kicheko kwani akagundua sikuwa na mapepo wala nini; bali ni sanaa! Muda huo, Mr. Mtiro nae alikuwa keshaondoka baada ya kumfikisha mgonjwa home!


Brother Massabooooooo!!!! Wherever you are, forgive me man! That small play was all about saving myself from your punishment!! Mr. Mtiro, na wewe nichunie ticha wangu, si unajuwa tena mambo ya uanafunzi! Kwanza hata form zenu za kujiunga kuna kipengele kinasema “sometimes, use your common sense!” LOL!

Kesi yangu na Brother Massabo ikaishia hapo! Wala hakuniuliza kwanini baada ya kumaliza Mock sikwenda shule! Angeniuliza nini wakati mwenyewe kashuhudia kwa macho yake kwamba nilikuwa mgonjwa mahututi?! Au kama ni wewe ungekuwa ndie Brother Massabo ungefanya nini?!

Hicho ni kisa kimojawapo tu nilichokifanya enzi zileeeee za uendawazimu, manake sio utoto! Bila shaka, hata wewe una visa kama hivi ulivyovifanya hususani enzi za primary school na sekondari! Tudadavulie bathiiii!!

Ebana Nasdaz Turuka alikuwepo enzi hizo.....Kama ye ndo angepewa hiyo issue angekuganda hadi ajue ukweli...Mtata sana yule mzee!!!
 
Kwakweli vituko viko vingi ila ambacho sitasahau kilitokea niko chekechea..si unajua ile LY ya kuingia la kwanza..kikapigwa kitu cha graduation basi tukaambiwa tupeleke michango manake shule ilikuwa ya hadhi flani mgodini Mwadui(ile nzuri ya miaka hiyo ) basi bwana jamaa nikapewa mchango nipeleke..nikakumbuka kuna mwenzangu kapeleka pungufu sikumbuki ngapi coz nilikua najua rangi tu ya fedha..nikaenda kununua pipi na kula na wenzangu (siwakumbuki wote) chenji nikapeleka shule noti ya kufanana na ile aliyopeleka mwenzangu kumbe dingi yake aliomba kulipa kwa installment na atamalizia in short time...nikapeleka na kujikausha,maticha wakamtafuta mdingi na kumhoji akasema amenipa yote..aisee nikahojiwa na nilipobainika nilikula za mianzi hadi niliona hio graduu haina raha ila siunajua utoto tena ...michezo kibao nikasahau na kutimba kwenye graduu coz mdingi alirekebisha ila home walinimaind na sisahau hadi leo coz huwa wananikumbushia nilivyojifanya mjanja.
 
Back
Top Bottom