Unakumbuka breakup yako ya kwanza?

Unakumbuka breakup yako ya kwanza?

Daah kuna kaka nilimpenda mno na alikuwa anajua bhasi bhana wee! Alikuwa ananitesa hatari eti sababu nampenda,
ila nilijikaza baada ya kuchoka na mateso niliamua kumuacha nikakaa wiki sijawasiliana nae hakuamini akapiga simu kuuliza kweli ' L' wiki nzima unakaa bila kuwasiliana na mpenzi wako!

Nikamjibu sina vocha, (maana nisipo piga mimi hapigi) ,
ikaenda akawana anapiga akijisikia hata baada ya siku 2,3 lakini moyoni mwangu nikasema huyu simtaki tena sikuwahi kumpigia tena.

kuna siku alipiga alilalamika mno nimebadilika sijui nini na nini sikumpa majibu yakueleweka najidai nipo bize, ikaenda ikaenda akipiga simu sipokei akachoka akapotezea.

Japo niliumia sana mapigo ya moyo yalikuwa yanaenda si kawaida
Kwa maumivu yale Aisee! Siruhusu tena mapenzi yanitese kiasi kile.
 
Alikuwa mrembo hatari, akasema tuachane ana mwanaume anaempenda...Niliumia vibaya mno yale maumivu hayafanani na chochote, nilikuwa naongea pekee yangu, chakula sili... Majuzi juzi tu hapa nimekutana nae anabonge la ziwa, ule uweupe umepotelea wap cjui... Nikimuangaliaa nacheka najiona bonge la fala
 
Yule ms*nge aliniacha jumapili ambayo jumatatu yake tulikuwa na test...sababu yake mammmae zake nikachafua CV ya kuzungusha ile paper (nilipata zero)

Nilikuwa siwezi kula
Siwezi kulia japo natamani kulia lakini machozi hayaji
Nilikuwa mchekaji mzuri lakini siku hizi sicheki kabisaaaa

Popote ulipo ama kama unasoma hapa ujue tu nakuchukia kuliko kawaida!!!na kwa taarifa yako ninae baby mpya nampenda sanaaaaaa

#povu

Halafu bado nakupenda
Unamchukia sana na kumpenda muda huo huo ?
 
Nimeacha mara nyingi sana na kwa sababu mbalimbali mpaka nishasahau ,nimeumia mara nyingi sana mpaka ikafika mahali moyo umekufa ganzi ,
Nilishawahi taka kumuowa bint fulani ,baada ya mzee wake kujua ni mimi akasema huyu hana kipato cha kumuowa mwanangu atampa shida tu aiseee,na shit mbali mbali mzee alizitoa ,mpaka bi mkubwa akataka aende kuongea na yule mzee ,nikamwambia ndoa hailazimishwi na mke mungu alonipangia hatotomia nguvu ,basi bi mkubwa akanisikia ,na yule mzee alisema hataki mwanae aolewe anataka amsomeshe baada ya miezi 6 yule mzee alifariki na ndoto ya kumsomesha mwanae ilifia hapo ,na yule bint kwa ugumu wa maisha akaolewa na mtu ambaye yaan alikuwa na maisha magumu hatari ,alafu mimi mungu akaja kuninyooshea mambo aiseee acheni haya maisha yana mengi sana
 
Wewe Baharia ni Muuaji! Alipona kweli?
Nilipogundua anataka kuniacha nikamuwahi akajifanya bado ananipenda kumbe ananilia timing anifanyie suprise ya kuniacha, siku anataka kukamilisha mpango wake nilimtandika makofi hatosahau maishani

Yaani nikipiga upande huu narudia upande wa pili ndo nahesabu kofi moja.
 
Nimeacha mara nyingi sana na kwa sababu mbalimbali mpaka nishasahau ,nimeumia mara nyingi sana mpaka ikafika mahali moyo umekufa ganzi ,
Nilishawahi taka kumuowa bint fulani ,baada ya mzee wake kujua ni mimi akasema huyu hana kipato cha kumuowa mwanangu atampa shida tu aiseee,na shit mbali mbali mzee alizitoa ,mpaka bi mkubwa akataka aende kuongea na yule mzee ,nikamwambia ndoa hailazimishwi na mke mungu alonipangia hatotomia nguvu ,basi bi mkubwa akanisikia ,na yule mzee alisema hataki mwanae aolewe anataka amsomeshe baada ya miezi 6 yule mzee alifariki na ndoto ya kumsomesha mwanae ilifia hapo ,na yule bint kwa ugumu wa maisha akaolewa na mtu ambaye yaan alikuwa na maisha magumu hatari ,alafu mimi mungu akaja kuninyooshea mambo aiseee acheni haya maisha yana mengi sana
Huyo mzee alikuwa Mpumbavu aliezeeka...Japo alishafariki Mungua anisamehe
 
What doesn't kill you! Makes you stronger! Nikipata hiyo break up ntakuja!
 
Mimi niliambiwa 'naona bora tuachane' na mimi ki-nunda nunda nikajibu 'poa tu'
Kumbe nilikua sijatafakari anamaanisha nini vizuri.. sasa baada ya kufika hostel ndio nikatafakari vizuri kitandani nikajua kweli 'it's over' mzee usingizi haupandi natamani kumpigia simu pride inanizuia..
Mwisho uzalendo ukanishinda kama saa 6 usiku nikapiga namba iko busy , whatsapp sioni dp.
Nikajua tayari nilishakula tofari(block)
Ikabidi nibadiri namba lkn akisikia sauti yangu anakata...
Nikipata taabu kwa week 2 peke yangu maana siwezi mwambia mtu yyte sababu najifanyaga nna pride na sijali mambo madogo madogo hata kama naumia...
Kama sikufa zile week mbili basi sitakufa tena kwa mapemzi
 
Back
Top Bottom