Unaisubiri paradiso ishushwe? Unachelewa, tengeneza paradiso nyumbani

Uhakika Bro

JF-Expert Member
Mar 29, 2022
2,398
3,071
Hivi paradiso italetwa? Au tutaileteleza wenyewe hapa duniani?

Screenshot_20231024-083303_WhatsApp.jpg


Watu wenye kusali hutusisitizia kila mara kwamba paradiso ni mahala pazuri saana 😍

Ni mahali ambapo kuna miti na maua mazuri ya kupendeza πŸ’πŸŒΊπŸŒΈπŸŽ„πŸ€πŸŽ‹πŸͺ»πŸŒΉ

Kuna wanyama wazuri wasioumana wala kuumauma watu ovyo πŸ‡πŸŽπŸ¦’πŸ†πŸ¦“πŸΆπŸ¦†πŸ¦šπŸ¦œ

Yaani ni bustani moja nzuri sana watu wanajilia tu matunda πŸŽπŸ‡πŸ‰πŸ“πŸ’πŸ…πŸ«πŸπŸπŸŠ na mito inaturirisha maji kila wakati.

Sasaa nimeanza kufikiria kwamba hivii kama tukiweka mikakati, hatuwezi kweli kujaribu kuikaribia hiyo hali?

Tunabadili tu tabia ndogondogo mfano;
1.Badala ya ukuta tunaweka fensi ya miba ile ya maua
2. Badala ya paving unaweka ukoka hasa zile sehemu ambazo sio njia
3. Badala ya kujaza jumba kiwanja chote. Unaweka tu nyumba ya kiasi sehemu inayobaki unaweka miti na matunda na maua.

Ukiitazama picha utagundua kuwa kuna maendeleo makubwa sana hapo, na bado pana hali nzuri tu ya kijijini. Tena kama ni picha ya kweli utakuta hapo wanaishi matajiri tu. Sema kitu kimoja hapo sijui wamewekeana sheria hakuna kumiliki gari yaani wao ni mwendo wa baiskeli tu!πŸ€”. Duh nao wamepitiliza asee. Ila fresh tu au we unaonaje?

Ukiweka mazingira ya nyumbani kwako hivyo utashangaa ndege na vipepeo wanajaa tu.

Na tukitaka kila familia iweze ku'afford' (kumudu bhana🀣) kuweka mazingira katika hali kama hiyo hapo inabidi kitu kinaitwa maji kiwe ni BWERERE kabisa. Yaaani nchi isambaze na kutiririsha maji kila kona ya nchi na vijiji. Vyanzo vya maji vipo tushindwe miundombinu tu na nia labda.

Eeh hali safi ya hewa ukirudi nyumbani unapumzika kweli.Kwani jamani ndugu zangu, kujenga majumba na mabarabaraπŸ—οΈπŸŒƒπŸŒ‡πŸ€πŸ­πŸ˜οΈπŸŒ kila sehemu ndio maendeleo? Kwa nini tusije na tafsiri ya kiafrika ya maendeleo na sie?

Unafikiri ni kwa nini UNICEF wanachukulia maeneo kama Ngorongoro kuwa ni Urithi wa dunia. Si kutokana na uasili wake?

Sikia na hii;
Tena kutokana na udadisi na kufikiria. Ninadhani katika mazingira hayo, watoto wanaokulia humo wanakuwa na akili sana. Kwa nini? E eeh kwa sababu wakiwa hapo akili inakuwa imetulia saafi kabisa hivyo wanajihisi amani na wanakuwa wadadisi. Na udadisi ndio akili ujue. Masala ni Kulangwa.
 
Sasaa nimeanza kufikiria kwamba hivii kama tukiweka mikakati, hatuwezi kweli kujaribu kuikaribia hiyo hali?

Tunabadili tu tabia ndogondogo mfano;
1.Badala ya ukuta tunaweka fensi ya miba ile ya maua
2. Badala ya paving unaweka ukoka hasa zile sehemu ambazo sio njia
3. Badala ya kujaza jumba kiwanja chote. Unaweka tu nyumba ya kiasi sehemu inayobaki unaweka miti na matunda na maua.
  1. Naafikiana nawe, fensi ya miba inachuja hewa, inapendezesha mandhali ya makazi na kuvutia viumbe hai kama ndege ili kuwianisha ekolojia
  2. Nyasi ni pambo zuri na hasa kama ukizipata zile zinazo repel nyoka kwaajili ya usalama
  3. Hapa mamlaka za ugawaji wa ardhi zinatakiwa kuongeza ukubwa wa viwanja na kuondokana na low density plots
Kwa ujumla hii mada ina mashiko sana ila changamoto zilizopo kwa maeneo mengi ni upatikanaji wa maji ya kumwagilia mimea
 
Ntaleta feed back miaka miwili ijayo, kuna eneo nilipata Ekari 10 najaribu kupabadilisha nimeanza kupanda miti mingi sana matunda ni nimepanda uzio wa michongoma kwanza, Patavutia sana we subiri
 
Ntaleta feed back miaka miwili ijayo, kuna eneo nilipata Ekari 10 najaribu kupabadilisha nimeanza kupanda miti mingi sana matunda ni nimepanda uzio wa michongoma kwanza, Patavutia sana we subiri
Una akili sana.

Hivyo ndivyo unamiliki na kuufaidi utajiri sasaa
 
  1. naafikiana nawe, fensi ya miba inachuja hewa, inapendezesha mandhali ya makazi na kuvutia viumbe hai kama ndege ili kuwianisha ekolojia
  2. Nyasi ni pambo zuri na hasa kama ukizipata zile zinazo repel nyoka kwaajili ya usalama
  3. Hapa mamlaka za ugawaji wa ardhi zinatakiwa kuongeza ukubwa wa viwanja na kuondokana na low density plots
Kwa ujumla hii mada ina mashiko sana ila changamoto zilizopo kwa maeneo mengi ni upatikanaji wa maji ya kumwagilia mimea
Exactly.

Ahsante

Na tuanze kufanyia kazi mmojammoja kidogokidogo
 
Maisha yamebadilika sana aisee
UCHUMI TATZO KUBWAAAA SANAAAA
HUWA NATAMANI SANA MAISHAN YA HIVI ila kiuhalisia mtu mmoja anapaswa kuishi kwenye eneo kubwa sana unapanda kila aina ya mti wa matunda na maua mbalimbali
 
Back
Top Bottom