Unadhani kwanini Watanzania wengi wanamkubali Rais Samia?

Unadhani kwanini Watanzania wengi wanamkubali Rais Samia?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
45,512
Reaction score
37,234
Ni kwasababu ya makusudi, haja na nia yake thabiti, ya wazi na njema ya kutaka kuibadili tanzania kiuchumi, kijamii na kusiasa?

Au ni kwasababu ya umadhubuti wa sera, mipango, mikakati, jitihada, bidii na umahiri wake katika kutekeleza kwa weledi sana na kwa ufasisi mkubwa mno miradi mtambuka ya maendeleo inayogusa mojakwamoja maisha ya watanzania kama vile maji, afya, elimu, kilimo, viwanda, uvuvi, miundombinu, usafirishaji N.K?

Au ni kwasababu ya amani liliyopo, ulinzi, usalama, uhuru, haki, utulivu, usawa, uwazi na uwajibikaji wake katika kuongoza nchi kwa misingi ya utawala wa sheria na kwa kuzingatia katiba ya nchi?

Au ni kwasababu ya matumani makubwa waliyo nayo Watanzania kwake, kwamba ndie pekee kiongozi wa kisiasa nchini, anae weza kutimiza ndoto na matarajio yao, ya maisha bora?

Kwa maoni yako, unadhani ni kwanini Samia Suluhu Hassan, anapendwa na kuaminika kiasi hiki, kitaifa na kimataifa?
 
Rais Samia anapendwa na kukubalika na mamillioni ya watanzania kwa sababu amekidhi matarajio ya watanzania na kukata kiu waliyokuwa nayo juu ya aina ya kiongozi waliyekuwa wanamuhitaji.

Kwa ufupi Mama yetu mpendwa na kipenzi cha watanzania ni jibu na jawabu kwa mahitaji ya watanzania.
 
Hivi wewe mtoa uzi, Huwa unatoa wapi hivi VICHEKESHO???🤣🤣
Hivi kweli wewe unaishi TZ??

Dalali anayeuza rasilimali za nchi???

Fanya simple research, Huwa anakubalika zaidi na CHAWA aina ya akina Luke.😅😅

Akiwa na busara mwisho inapaswa iwe 2025.

Amezungukwa na genge la KUSIFU NA "KUABUDU "
Waimba pambio hao wanajua, Kuwa hana kibali, wanafanya hivyo kujioendekeza na kulinda maslahi binafsi.

Nimekukumbuka, mama anaupiga mwingi sana,
1.Bandari ameweka rehani.

2.Mbuga za wanyama kaweka rehani, kawapa wajomba, misiti, na amewafukuza wamasai kwenda MSOMERA, kawaondoa katika ancestral land.
Hapaswi kupewa nafasi ,ataauza nchi zaidi ya hapo.

Nchi unaweza kupigwa Mnada.
Mama hana kibali, bahati mbaya hakuna ambaye anaweza kumwambia.

Cc:Lucas Mwashambwa
Cc:Kipara Kipya
Cc:Magonjwa Mtambuka
Cc:Faiza Foxy
 
Back
Top Bottom