Nov 01, 2023 12:18 UTC
Hii ni kauli ya Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu, OCHA, Martin Griffiths aliyoitoa kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa X. Griffiths amezungumza Jumanne kwa njia ya simu na familia zilizoko Ghaza akiwa Quds (Jerusalem) Mashariki, familia ambazo zimemsimulia kile wanachopitia tangu utawala haramu wa Israel uanzishe mashambulizi ya kinyama Oktoba 7.
Naye James Elder, msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF, amenukuliwa akisema kwamba Wizar Aya Afya ya Palestina imethibitsha kuwa hadi sasa watoto 3,450 wameuawa katika hujuma za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza.
Ofisi ya OCHA nayo imeripoti kuwa watoto wengine 1,000 Ghaza hawajulikani waliko na pengine wamenasa au wamefukiwa wakiwa tayari wamekufa kwenye vifusi vya majengo yaliyobomolewa kwa mashambulizi.