Umwamba wa nchi za Magharibi wazuia nchi za Afrika kushiriki kwa haki kwenye upunguzaji wa utoaji wa kaboni

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG31N1644742391.jpg


Tangu mwaka huu uanze, dunia nzima imeshuhudia majanga mbalimbali yaliyosababishwa na hali mbaya ya hewa, na mabadiliko ya tabianchi yamekuwa msukosuko wa kweli. Ikilinganishwa na sehemu nyingine duniani, utoaji wa kaboni barani Afrika siku zote ni wa kiwango cha chini zaidi duniani, na jumla ya kiasi hicho ni chini ya 2% -3% ya dunia. Lakini athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi ni kubwa hasa barani Afrika, majanga kama ya nzige, ukame na mafuriko yametokea mara kwa mara, na kutishia moja kwa moja uchumi, usalama na utulivu wa Afrika.

Katika Mkutano wa Kilele wa Hali ya Hewa barani Afrika wa mwaka 2023, uliomalizika hivi karibuni mjini Nairobi, Kenya, viongozi wa Afrika walitoa wito tena kwa jumuiya ya kimataifa kuzingatia zaidi matakwa na taabu za Afrika katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuisaidia Afrika kutafuta maendeleo endelevu ya kijani.

Kwa muda mrefu, zikiwa watoaji wakuu wa hewa chafu, nchi za Magharibi zimechanganya michango na wajibu wao katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi duniani, na ni vigumu kwa nchi zinazoendelea hasa nchi za Afrika kushiriki kwenye mchakato huo kwa haki, ambapo kauli yenye uwakilishi mkubwa ni ile iliyotolewa na mjumbe maalumu wa rais wa Marekani anayeshughulikia mabadiliko ya tabia nchi Bw. John Kerry kwenye mkutano wa mazingira wa Afrika ngazi ya mawaziri nchini Senegal, Septemba mwaka jana. Bw. Kerry alisema: “Mazingira ya asili hayajali ni wapi hewa chafu inakotoka...Afrika inapaswa kuungana na nchi za Magharibi kupunguza hewa chafu duniani.”

Kwanza kabisa, mpango wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi unaokuzwa na nchi za Magharibi haswa Marekani hauendani na hali halisi ya Afrika. Moja ya mapungfu ya mpango wao ni kwamba nchi hizo zinazingatia tu upunguzaji wa utoaji wa kaboni, na kusisitiza wajibu sawa wa kupunguza utoaji wa kaboni kwa nchi zote duniani, na kuzibebesha nchi zinazoendelea mzigo mkubwa, wakati taabu halisi za nchi zisizoendelea zikiwemo nchi za Afrika bado hazijakuwa ajenda kuu. Kwa maana fulani, sera ya kutegemea magharibi ni sababu ya moja kwa moja ya kutengwa kwa muda mrefu kwa Afrika katika ajenda ya kimataifa ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Pili, Marekani na nchi nyingine za Magharibi zinatumia suala la mabadiliko ya tabia nchi kujinufaisha. Kushughulikia mabadiliko ya tabianchi kumekuwa kanuni mpya ya nchi za Magharibi kuzilenga nchi za Afrika. Ushirikiano wao na nchi za Afrika ni kwa ajili ya kuimarisha maslahi yao ya jadi ya siasa za kijiografia. Kwa mfano, nchi za Afrika zinazochaguliwa na Marekani kama washirika wa ushirikiano wa mabadiliko ya tabia nchi ni zile zinazokubali maadili ya Marekani katika masuala ya haki za binadamu na demokrasia; na Ufaransa inazichukulia nchi za Afrika zinazozungumza Kifaransa kuwa wadau wa ushirikiano.

Kwa hivyo, ni nchi za Afrika zinazokubaliwa na Marekani na Ufaransa kwenye siasa za kijiografia ndizo zinazostahiki ushirikiano wa nchi za magharibi. Hatua hii sio tu inafanya suala la mabadiliko ya tabianchi kuwa la kisiasa, bali pia kuigawa Afrika katika makundi, jambo ambalo linakinzana na matakwa ya Afrika ya kuwa na umoja katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kudhoofisha nafasi ya Afrika katika mazungumzo ya mabadiliko ya tabia nchi kati ya nchi za Kaskazini na Kusini.

Vilevile, nchi za magharibi zinaweka vikwazo vya kijani na kutafuta faida za kiuchumi. Kwa kutegemea nguvu yao ya kiteknolojia, nchi za Magharibi zimeunda viwango vingi vya biashara na lebo za eti “urafiki na mabadiliko ya tabia nchi”, zikijaribu kuongeza faida zao za kiuchumi kutoka Afrika. Kwa mfano, Umoja wa Ulaya ulitoa "Utaratibu wa Marekebisho ya Mipaka ya Carbon" mwaka 2021 ili kutoza kodi kwa bidhaa "zisizo za kijani" zinazoagizwa kutoka nje. Utaratibu huu unatarajiwa kuleta faida ya ziada ya Euro bilioni 5 hadi 14 kwa Umoja wa Ulaya, lakini kwa gharama ya kudhoofisha kwa kiasi kikubwa faida za nchi za Afrika kwa mauzo ya nje ya bidhaa kwa EU, na kutuhumiwa kuwa "vita vya biashara".

Katika Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Copenhagen uliofanyika mwaka 2009, nchi zilizoendelea ziliahidi kutoa angalau dola bilioni 100 kila mwaka ili kusaidia nchi zinazoendelea kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi, lakini hadi sasa zimeshindwa kutekeleza ahadi zao. Ukuaji wa kijani wa Afrika ni muhimu kwa maendeleo na utulivu wa Magharibi.

Nchi za Magharibi lazima zitambue michango ya Afrika katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kutoa misaada ikiwa ni pamoja na fedha kwa Afrika, na kuhakikisha kuwa Afrika inaweza kushiriki kwa haki katika mabadiliko ya kijani duniani. Kama mshirika muhimu wa mabadiliko ya kijani barani Afrika, China inashirikiana na nchi za Afrika kujenga "Ukanda Mmoja, Njia Moja " wa kijani, na kupitia utaratibu kama Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC na Ushirikiano wa Kusini-Kusini kuhimiza ujenzi wa Afrika ya kijani, na kutekeleza kivitendo wazo la “Afrika haiwezi kukosekana katika maendeleo endelevu duniani."
 
Back
Top Bottom