Umuhimu wa kufunga vyumbani kwetu

Umuhimu wa kufunga vyumbani kwetu

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,304
Reaction score
12,997
Habari za mchana mabibi na mabwana...

Naomba uzoefu wenu kuhusu ufungaji wa vyumba vya kulala hasa kwa wale tunaoishi na madada / makaka wa kazi "Masterbedroom" je tunafunga kwa ajili ya usalama?

Je, tunafunga ili kwamba kuna mwenye nia mbaya asipate mwanya?

Kwa mfano una house girl, unaondoka na kumuachia nyumba nzima pekeyake huku ukiwa umefunga chumbani kwako. Ukiamini usalama upo, lakini akafanya ujanja wa kutafuta ufunguo wa ziada akawa anafanya mambo yake.

Mfano mwingine. House boy anashirikiana na house girl wanavunja mlango na kuiba usalama uko wapi hapo?

Mfano mwingine. Iwapo house girl analengo lakini baya je kufunga mlango wa chumbani ni kumdhibiti ikiwa yeye huandaa chakula cha familia wakati haupo?

Karibuni kwa michango, maoni, nyongeza.
 
madhara ya kuacha waz master bedroom ni kwamba kule ndiko zinakaa nyaraka mbalimbali kama hati na document nyengne kuacha waz ina maana zinaweza kupotea bila wewe kugundua kwa mapema cz si kila siku tunaangalia document zetu binafs ila ukifunga pakivunjwa ni rahs kujua kama tayari umeshaibiwa na ujue wap pa kuanzia....
 
Master bedroom is a "holy place", eneo ambalo hakuna mtu anaingia ovyo, unless kuwe na sababu za msingi...

Kaka Elly kama HG au HB ana nia mbaya na ninyi wanandoa je atashindwa kwa kufunga masterbedrrom
 
madhara ya kuacha waz master bedroom ni kwamba kule ndiko zinakaa nyaraka mbalimbali kama hati na document nyengne kuacha waz ina maana zinaweza kupotea bila wewe kugundua kwa mapema cz si kila siku tunaangalia document zetu binafs ila ukifunga pakivunjwa ni rahs kujua kama tayari umeshaibiwa na ujue wap pa kuanzia....

Asante kwa point yako... Nimepata kitu!
 
tunafunga ili kuwe salama ... na ikitokea wamevunja basi nitakuwa najua kuna jambo limefanyika
 
Kaka Elly kama HG au HB ana nia mbaya na ninyi wanandoa je atashindwa kwa kufunga masterbedrrom
Point yangu hailengi kwenye HG kutuwazia mabaya au kuwa na nia mbaya na sisi coz akitaka atafanya tu..
...Binafsi naamini chumba changu ni kwa ajili yangu na mke wangu basi...
...Ikiwezekana hata newborn asilale na mama yake, akitaka kumnyonyesha aende kwa mtoto huko..
 
Point yangu hailengi kwenye HG kutuwazia mabaya au kuwa na nia mbaya na sisi coz akitaka atafanya tu..
...Binafsi naamini chumba changu ni kwa ajili yangu na mke wangu basi...
...Ikiwezekana hata newborn asilale na mama yake, akitaka kumnyonyesha aende kwa mtoto huko..

Mmmmhhh.. Kaka Elly hata kwa newborn jamani??? Sasa joto la mama atalipata wapi???
 
Kufunga kama kufunga bedrum kunaweza kudhibit nia mbaya za aina fulani fulani mfano wizi, au urahis wa kumuiba mumeo

Ila kuna nia mbaya nyingne kuzidhibit kwake huwez kuishia kwa kufunga masterbedrum mfano chakula, mtoto na vinginevyo.

Hayo ndio yale ambayo ni kumuomba mungu tuu,
 
Kufunga kama kufunga bedrum kunaweza kudhibit nia mbaya za aina fulani fulani mfano wizi, au urahis wa kumuiba mumeo

Ila kuna nia mbaya nyingne kuzidhibit kwake huwez kuishia kwa kufunga masterbedrum mfano chakula, mtoto na vinginevyo.

Hayo ndio yale ambayo ni kumuomba mungu tuu,

Shukrani kwa maoni....
 
Halafu usipofunga masterbedroom anaweza kupewa kamera na shigongo akaziweka room yenu kesho ukajikuta uko front page ya gazeti la udaku huku heading inasema "mke wa kigogo aonekana gesti na mbunge,OFM ina mkanda mzima"
 
Binafsi nina maoni yafuatayo kuhusu kufunga au kuacha wazi Master Bedroom pindi ninapokuwa sipo nyumbani.Hakika, Kila mtu ana stahili faragha (privacy) kwa namna moja au nyingine katika maisha. Sababu kubwa ya kufunga Master bed room ni kuhakikisha usalama wa chumba chenyewe kwa si tuu mfanyakazi bali hata mtu yeyote yule zaidi ya watumiaji wa chumba husika. Ila yapo madhara ya kufunga Master Bedroom. Kuna wanaofunga na kumwachia dada(mfanyakazi) ufunguo,kuna wanao funga na kuondoka na funguo.Kuna ambao hatufungi kabisa na kwa utashi wa dada ameamua kufunga yeye na kuhifadhi funguo hizo. Na pindi ninaporejea nyumbani ananikabidhi. Kikubwa ni kuwa ninaishi na familia yangu kwa maana (mimi) ni baba nina mke (mama) na watoto watatu.Siishi na ndugu,jamaa wala rafiki.Na hivyo swala la utawala na uthibiti linakuwa rahisi sana. Kwa uchache wetu huo,utaona kuwa kufunga chumba si swala kubwa sana. Naamini pia kuwa kila nyumba ina miiko yake na utaratibu wake.Hatuwezi kuwa sawa na daima hatutakuwa sawa.Kwa mantiki hiyo, kila chumba kwenye nyumba yangu kina umuhimu wake.Nilichofanya ni kwamba nimemfundisha dada aelewe na atambue wajibu wake katika familia yangu.Swala la kulinda na kuheshimu mali za mimi boss wake ni jukumu lake pia.Yote kwa yote mada hii inafungua mjadala mwingine tena kuhusu namna na jinsi tunavyoishi na wafanyakazi wetu huko majumbani kwetu.Thamani ya MTU ni UTU.................
 
Ngoja sisi tunaoishi stoo tunyamaze.
Yaani chumba hicho hicho ndo kuna jiko,kitanda,ndoo za maji, meza, kabati, friji, subwoofer, vyombo vya chakula e.t.c

WAISHI STOO WENZANGU HOYEEEEEE....
 
Binafsi nina maoni yafuatayo kuhusu kufunga au kuacha wazi Master Bedroom pindi ninapokuwa sipo nyumbani.Hakika, Kila mtu ana stahili faragha (privacy) kwa namna moja au nyingine katika maisha. Sababu kubwa ya kufunga Master bed room ni kuhakikisha usalama wa chumba chenyewe kwa si tuu mfanyakazi bali hata mtu yeyote yule zaidi ya watumiaji wa chumba husika. Ila yapo madhara ya kufunga Master Bedroom. Kuna wanaofunga na kumwachia dada(mfanyakazi) ufunguo,kuna wanao funga na kuondoka na funguo.Kuna ambao hatufungi kabisa na kwa utashi wa dada ameamua kufunga yeye na kuhifadhi funguo hizo. Na pindi ninaporejea nyumbani ananikabidhi. Kikubwa ni kuwa ninaishi na familia yangu kwa maana (mimi) ni baba nina mke (mama) na watoto watatu.Siishi na ndugu,jamaa wala rafiki.Na hivyo swala la utawala na uthibiti linakuwa rahisi sana. Kwa uchache wetu huo,utaona kuwa kufunga chumba si swala kubwa sana. Naamini pia kuwa kila nyumba ina miiko yake na utaratibu wake.Hatuwezi kuwa sawa na daima hatutakuwa sawa.Kwa mantiki hiyo, kila chumba kwenye nyumba yangu kina umuhimu wake.Nilichofanya ni kwamba nimemfundisha dada aelewe na atambue wajibu wake katika familia yangu.Swala la kulinda na kuheshimu mali za mimi boss wake ni jukumu lake pia.Yote kwa yote mada hii inafungua mjadala mwingine tena kuhusu namna na jinsi tunavyoishi na wafanyakazi wetu huko majumbani kwetu.Thamani ya MTU ni UTU.................


Shukrani mkuu kwa maoni yako.... Umemaliza
 
ngoja sisi tunaoishi stoo tunyamaze.
Yaani chumba hicho hicho ndo kuna jiko,kitanda,ndoo za maji, meza, kabati, friji, subwoofer, vyombo vya chakula e.t.c

waishi stoo wenzangu hoyeeeeee....

hoyeeeeeeeeeee.................!!!!!!!!!
 
madhara ya kuacha waz master bedroom ni kwamba kule ndiko zinakaa nyaraka mbalimbali kama hati na document nyengne kuacha waz ina maana zinaweza kupotea bila wewe kugundua kwa mapema cz si kila siku tunaangalia document zetu binafs ila ukifunga pakivunjwa ni rahs kujua kama tayari umeshaibiwa na ujue wap pa kuanzia....

Well said......!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom