Umuhimu wa Kuandikwa Historia ya Kweli ya TANU

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
MUHIMU WA KUWA NA HISTORIA YA KWELI YA UHURU WA TANGANYIKA

Kaandika aliyeandika:

"Lakini bado katika kuunganisha vugu vugu la ukombozi, utapungukiwa sana maarifa ukishindwa kujua Mwl. Nyerere ndo alikuwa Master Planner."

Nimejitahidi kumjibu kumueleza ukweli wa historia ya ukombozi:
Kweli Nyerere ndiye Master Planner?

Uko ushahidi au maneno matupu?

Hebu iangalieni historia ya harakati kuanzia mwanzo Kleist Sykes (1894 - 1949)alipokutana na Dr. Kwegyir Aggrey 1924?

Mnawajua waasisi wa African Association 1929?

Mnajua mchango wa Hamza Mwapachu (1913 - 1962) baada ya WWII alipoanza kuwakusanya vijana wasomi kuleta mabadiliko ndani ya TAA?

Kati ya vijana hawa ni Paul Bomani na Julius Nyerere.

Unaujua mchango wa Abdul Sykes (1924 - 1968), Hamza Mwapachu na Schneider Abdillah Plantan kuleta uongozi mpya TAA 1950?

Katika kipindi hiki kuanzia 1949 unaujua mchango wa madaktari watano: Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Luciano Tsere, Dr. Vedasto Kyaruzi, Dr. Michael Lugazia na Dr. Wilbard Mwanjisi katika harakati za TAA?

Hili kundi la madaktari likijiita "Action Group," na historia yao ipo katika mswada, "The Muhaya Doctor," alioandika Dr. Kyaruzi baada ya uhuru.

Unaweza kusoma yaliyomo katika mswada huo katika kitabu cha Judith Listowel, "The Making of Tanganyika," (1965).

Kuna mapendekezo ya katiba yaliyoandikwa na TAA Political Subcommittee na kupelekwa kwa Gavana Edward Twining 1950.

Mnawajua wajumbe wa kamati hiyo?

Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Mshauri wa TAA Political Subcommittee kuhusu ukoloni wa Muingereza alikuwa Earle Seaton.
Mnaujua mchango wake katika suala la UNO na katiba ya TANU?

Mnaujua uzito wa mapendekezo yaliyokuwa ndani ya waraka huo?
Unaweza ukausoma katika kitabu cha Cranford Pratt, "Critical Phase in Tanzania."

Yako mengi ya kueleza.
Katika hayo hapo juu yupo Nyerere?

Sasa wapi unakutana na Nyerere na ukamjua?
Nyerere unakutananae 1952 nyumbani kwa Abdul Sykes TAA Act. President na Secretary.

Je, kaja na mpango wowote wa kuanzisha chama cha siasa?
Hakuwa na mpango wowote.

Master Planner atakuwaje ikiwa hana plan?

1695876329987.png

1695876378583.png

1695876408020.png

1695876432709.png

Earle Seaton, Hamza Mwapachu na Abdul Sykes​
 
Washindi ndio huandika historia,failuers huja baadae kujifanya wanarekebisha historia.

Historia ya Tanu na Tanganyika ilikwisha andikwa,hii ya huyu mzee ni historia yake na ukoo wake sio ya watanganyika.
 
Wakati hiyo historia inaandikwa hao wahusika ambao tunaaminishwa hawakutajwa walikua wapi?

Nani aliandika hii historia iliyopo saivi?

Hiyo tunayotaka kuandika tukiamini ni ya kweli nani ataiandika na tutajuaje ni ya kwel?
 
Washindi ndio huandika historia,failuers huja baadae kujifanya wanarekebisha historia.

Historia ya Tanu na Tanganyika ilikwisha andikwa,hii ya huyu mzee ni historia yake na ukoo wake sio ya watanganyika.
Jiwe...
Historia ya TANU hakika iliashaandikwa lakini ilikuwa na makosa.
Kuwa nimeandika historia ya ukoo wangu kwa kiasi fulani umesema kweli.

Babu yangu Salum Abdallah alishiriki katika harakati za uhuru kuanzia African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Historia hiyo ya TANU uliyoitaja wewe kuwa imeandikwa babu yangu hakuwemo pamoja na wazalendo wengine wengi.

Historia niliyoandika mimi imebadili historia hiyo ambayo wewe unaiamini.
Historia hii niliyoiandika mimi iko katika Cambridge Journal African History (1998).

Historia hii niliyoandika mimi iko katika Dictionary of African Biography (DAB) (2011).

Ipo vilevile katika Julius Nyerere A Biography (2020) na katika kitabu hiki Jopo la Waandishi wakiongozwa na Prof. Issa Shivji walinihoji mara mbili kuhusu historia ya Mwalimu Nyerere.

Ndani ya kitabu hiki wamesema kuwa katika utafiti wao maktaba tatu ndizo walizokuta zina taarifa nyingi za Mwalimu Nyerere na zimewekwa vyema: Maktaba ya Dr. Salim Ahmed Salim, Maktaba ya Mohamed Said na Maktaba ya Brig. General Hashim Mbita uk. xii.

Haiwezekani kwa haya niliyoandika hapo juu ikawa mzee mimi nimeandika historia ya wazee wangu na si historia ya Tanganyika.

Ila ningependa ufahamu kuwa nimeandika historia hii nikiwa kijana angalia picha hiyo hapo chini nimepiga Nairobi Muthaiga Club nikiwa na Ally Sykes:

1695908611489.png

1989​
 
Wakati hiyo historia inaandikwa hao wahusika ambao tunaaminishwa hawakutajwa walikua wapi?

Nani aliandika hii historia iliyopo saivi?

Hiyo tunayotaka kuandika tukiamini ni ya kweli nani ataiandika na tutajuaje ni ya kwel?
Mpaji...
Naanza kwa kukuwekea majina ya waasisi wa African Association 1929:

Cecil Matola (President), d. 1934, Kleist Sykes (Secretary) d. 1949, Mzee bin Sudi d. 1972, Ibrahim Hamisi, Zibe Kidasi, Suleiman Majisu, Ali Said Mpima, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Katika hawa waasisi aliyeandika historia ya African Association ni Kleist Sykes.

Historia hii ambayo ni historia ya maisha yake mswada wake ukaandikwa na mjukuu wake Aisha ''Daisy'' Sykes mwaka wa 1968 kama Seminar Paper wakati akiwa mwanafunzi University of East Africa.

Unaweza ukasoma hii Seminar Paper Makataba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana.
Mswada huu ukaja kuchapwa ndani ya kitabu aichohariri John Ilife: ''Modern Tanzanians,'' (1973).

Naamini wengi katika hawa waasisi wa AA walikuwa wamekufa wakati historia ya AA inatoka kama kitabu katika ''Modern Tanzanians.''

Historia ya TANU imeandikwa na Kimambo na Temu (1969), Abubakar Olotu, Chuo Cha Kivukoni na waandishi wengine lakini hawa wote hakuna aliyetaka kuwahoji akina Sykes.

Mimi nimeandika historia ya TANU kwa kutumia Nyaraka za Sykes na kuwahoji wazalendo wengine nje ya Dar es Salaam waliohusika na kuaisisi TANU.

Ukweli wa kinachoandikwa kinathibitishwa ushahidi wa nyaraka na mahojiano na waasisi wenyewe na walioshuhudia.

Angalia picha hizi:

1695910264895.png

Julius Nyerere TANU Card No. 1 na Ally Sykes TANU Card No, 2
1695910388694.png

Dome Okochi Budohi TANU Card No. 6 na Mwandishi
Nairobi 1972
(Picha kutoka kitabu: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' London 1998)​
 
Washindi ndio huandika historia,failuers huja baadae kujifanya wanarekebisha historia.

Historia ya Tanu na Tanganyika ilikwisha andikwa,hii ya huyu mzee ni historia yake na ukoo wake sio ya watanganyika.
Kabisa.
 
Ngongo,
Ikiwa hutaki kuunali ukweli hakuna wa kukulazimisha.
Historia ya Tanganyika inaanzia kwa Mwl Nyerere na kumalizikia kwa Mwl Nyerere.

Historia nyingine hakuna labda historia ya Wazee wako ambayo haina uhusiano na historia ya nchi yetu tukufu.

Historia ya Zanzibar inaanzia kwa Okello wengine wanadandia.

Bila mkono wa Kanisa hasa Catholic nchi yetu ingekuwa bado inatawaliwa na Mwingereza.

Mchango wa Kanisa hasa kupitia elimu na afya uliharakisha upatikanaji wa uhuru wa Tanganyika.

Ukitaka kuthibitisha hilo,Soma waraka wa kanisa kuhusu bandari halafu wasikilize wale masheikh wanaotaka Bandari zetu zimilikiwe na waarabu kisa uislam.

Tanganyika bila ukristo ingekuwa Somalia nyingine.
 
Historia ya Tanganyika inaanzia kwa Mwl Nyerere na kumalizikia kwa Mwl Nyerere.

Historia nyingine hakuna labda historia ya Wazee wako ambayo haina uhusiano na historia ya nchi yetu tukufu.

Historia ya Zanzibar inaanzia kwa Okello wengine wanadandia.

Bila mkono wa Kanisa hasa Catholic nchi yetu ingekuwa bado inatawaliwa na Mwingereza.

Mchango wa Kanisa hasa kupitia elimu na afya uliharakisha upatikanaji wa uhuru wa Tanganyika.

Ukitaka kuthibitisha hilo,Soma waraka wa kanisa kuhusu bandari halafu wasikilize wale masheikh wanaotaka Bandari zetu zimilikiwe na waarabu kisa uislam.

Tanganyika bila ukristo ingekuwa Somalia nyingine.
Ngongo,
Historia iliyoanza kwa Mwalimu Nyerere na kuishia kwa Mwalimu Nyerere ilikuwapo na hadi leo ipo katika vitabu.

Lakini baada ya kuandika kitabu cha Abdul Sykes historia ambamo ndani yake kuna historia ya Julius Nyerere historia iliyokuweko haina tena ithibati.

Leo waalimu wanaposomesha historia ya utaifa wa Tanganyika kupitia African Association wanafanye rejea kuu mbili moja ni kitabu cha Abdul Sykes (1998)na Dictionary of African Biography (2011).

Katika kitabu cha Abdul Sykes mwanafunzi atasoma historia ya Kleist Sykes na Dr. Kwegyir Aggrey vipi Dr. Aggrey alimshawishi Kleist kuunda umoja wa Waafrika wa Tanganyika.

Katika Dictionary of African Biography (DAB) mwanafunzi atamsoma kwanza Dr. Aggrey historia yake na nafasi yake katika historia ya Bara la Afrika na pili atamsoma tena Kleist.

Mwalimu atawaelekeza wanafunzi wake kurejea tena katika kitabu cha Abdul Sykes kumsoma Julius Nyerere.

Leo hakuna chuo kinasomesha historia inayoanza na Nyerere na kumalizikia na Nyerere.
 
MUHIMU WA KUWA NA HISTORIA YA KWELI YA UHURU WA TANGANYIKA

Kaandika aliyeandika:

"Lakini bado katika kuunganisha vugu vugu la ukombozi, utapungukiwa sana maarifa ukishindwa kujua Mwl. Nyerere ndo alikuwa Master Planner."

Nimejitahidi kumjibu kumueleza ukweli wa historia ya ukombozi:
Kweli Nyerere ndiye Master Planner?

Uko ushahidi au maneno matupu?

Hebu iangalieni historia ya harakati kuanzia mwanzo Kleist Sykes (1894 - 1949)alipokutana na Dr. Kwegyir Aggrey 1924?

Mnawajua waasisi wa African Association 1929?

Mnajua mchango wa Hamza Mwapachu (1913 - 1962) baada ya WWII alipoanza kuwakusanya vijana wasomi kuleta mabadiliko ndani ya TAA?

Kati ya vijana hawa ni Paul Bomani na Julius Nyerere.

Unaujua mchango wa Abdul Sykes (1924 - 1968), Hamza Mwapachu na Schneider Abdillah Plantan kuleta uongozi mpya TAA 1950?

Katika kipindi hiki kuanzia 1949 unaujua mchango wa madaktari watano: Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Luciano Tsere, Dr. Vedasto Kyaruzi, Dr. Michael Lugazia na Dr. Wilbard Mwanjisi katika harakati za TAA?

Hili kundi la madaktari likijiita "Action Group," na historia yao ipo katika mswada, "The Muhaya Doctor," alioandika Dr. Kyaruzi baada ya uhuru.

Unaweza kusoma yaliyomo katika mswada huo katika kitabu cha Judith Listowel, "The Making of Tanganyika," (1965).

Kuna mapendekezo ya katiba yaliyoandikwa na TAA Political Subcommittee na kupelekwa kwa Gavana Edward Twining 1950.

Mnawajua wajumbe wa kamati hiyo?

Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Mshauri wa TAA Political Subcommittee kuhusu ukoloni wa Muingereza alikuwa Earle Seaton.
Mnaujua mchango wake katika suala la UNO na katiba ya TANU?

Mnaujua uzito wa mapendekezo yaliyokuwa ndani ya waraka huo?
Unaweza ukausoma katika kitabu cha Cranford Pratt, "Critical Phase in Tanzania."

Yako mengi ya kueleza.
Katika hayo hapo juu yupo Nyerere?

Sasa wapi unakutana na Nyerere na ukamjua?
Nyerere unakutananae 1952 nyumbani kwa Abdul Sykes TAA Act. President na Secretary.

Je, kaja na mpango wowote wa kuanzisha chama cha siasa?
Hakuwa na mpango wowote.

Master Planner atakuwaje ikiwa hana plan?

Mzee Mohamed Said, kwanini unahoji juu ya mchango wa mwal. Nyerere kuhusu Uhuru wa Tanganyika? Litakuwa jambo jema sana utuambie malengo mahususi na mikakati waliyokuwa nayo wazee wetu walipoanzisha vyama vya awali ulivyovitaja "AA", "TAA" na baadae TANU.

Vyama vya mwanzo vilikuwa na malengo ya kupigania maslahi na vilihusisha watu wache wenye maslahi binafsi hadi pale malengo hayo yalipobadilishwa na kugeuka kuwa chama cha kupigania Uhuru. Kwa maana hiyo mzee Said, unaweza kuwa unataja majina ya watu ambao pamoja na kuanzisha hivyo vyama vya awali lakini hawakuwa na lengo la kupigania Uhuru. Historia inajieleza yenyewe siyo lazima mhusika mwenyewe kama vile Sykes ajiandikie historia mwenyewe.

Ni bahati mbaya umekuwa bias kidini kwenye maandiko yako mengi. Hii inapunguza Imani kwenye kile unachokiandika wewe kuhusu historia ya Uhuru wa Tanganyika.

Kuna maswali mengi ya kujiuliza: wakati wa Uhuru na baada ya Uhuru, hawa watu uliowaoredhesha walikuwepo, kwann hawakujitokeza kuusema huu ukweli? Jibu ni moja, pamoja na sababu nyingine, wengi wao waliishia njiani baada ya TAA kubadili malengo ya awali na kuwa chama cha kupigania Uhuru na baadae kuundwa kwa TANU. Nina hakika unaelewa vizuri lakini kwasababu unazozijua unaweza kutuaminisha vinginevyo.
 
Mzee Mohamed Said, kwanini unahoji juu ya mchango wa mwal. Nyerere kuhusu Uhuru wa Tanganyika? Litakuwa jambo jema sana utuambie malengo mahususi na mikakati waliyokuwa nayo wazee wetu walipoanzisha vyama vya awali ulivyovitaja "AA", "TAA" na baadae TANU.

Vyama vya mwanzo vilikuwa na malengo ya kupigania maslahi na vilihusisha watu wache wenye maslahi binafsi hadi pale malengo hayo yalipobadilishwa na kugeuka kuwa chama cha kupigania Uhuru. Kwa maana hiyo mzee Said, unaweza kuwa unataja majina ya watu ambao pamoja na kuanzisha hivyo vyama vya awali lakini hawakuwa na lengo la kupigania Uhuru. Historia inajieleza yenyewe siyo lazima mhusika mwenyewe kama vile Sykes ajiandikie historia mwenyewe.

Ni bahati mbaya umekuwa bias kidini kwenye maandiko yako mengi. Hii inapunguza Imani kwenye kile unachokiandika wewe kuhusu historia ya Uhuru wa Tanganyika.

Kuna maswali mengi ya kujiuliza: wakati wa Uhuru na baada ya Uhuru, hawa watu uliowaoredhesha walikuwepo, kwann hawakujitokeza kuusema huu ukweli? Jibu ni moja, pamoja na sababu nyingine, wengi wao waliishia njiani baada ya TAA kubadili malengo ya awali na kuwa chama cha kupigania Uhuru na baadae kuundwa kwa TANU. Nina hakika unaelewa vizuri lakini kwasababu unazozijua unaweza kutuaminisha vinginevyo.
Mbussi,
Hayo uliyoandika si kweli.
 
Back
Top Bottom